ad

ad

Bahanuzi arudi Bongo kama alivyoondoka


MSHAMBULIAJI wa Yanga, Said Bahanuzi amemaliza majaribio yake ya wiki moja aliyokwenda kufanya nchini Malaysia katika Klabu za Teregganu na T-Team ambapo amerejea nchini.

Bahanuzi aliondoka nchini Alhamisi iliyopita kuelekea nchini humo kwenda kufanya majaribio ya wiki moja kwa ajili ya kucheza soka la kulipwa.

Akizungumza  Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema Bahanuzi alifanya majaribio katika timu mbili tofauti alipokuwa Malaysia katika timu za Teregganu na T-Team.
 
“Bahanuzi amemaliza leo (Jumatano) majaribio na usiku ataanza safari ya kurudi Tanzania kwa ajili ya kujiunga na wenzake mara baada ya kuwasili. Timu zote hizo zipo nchini Malaysia zinashiriki Super League lakini majibu ya majaribio bado sijayapata,” alisema Baraka.
CREDIT: GPL

Powered by Blogger.