Kiiza, Kavumbagu wamng’oa Kaseja •Yanga yamnasa Javu wa Mtibwa.
WAKATI wengi wakijiuliza sababu za kuachwa kwa kipa namba moja wa
Simba, Juma Kaseja kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, habari
kutoka ndani ya klabu
hiyo, zinasema kisa ni kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Yanga katika
mechi ya kufunga pazia la Ligi Kuu iliyochezwa Mei 18.
Kaseja akiwa langoni katika mechi hiyo iliyochezeshwa na Martin
Saanya, mabao ya Yanga yalifungwa na Didier Kavumbagu dakika ya tano na
Hamis Kiiza dakika ya 62.
Habari za kuaminika toka ndani ya uongozi wa Simba zinaeleza kuwa
kipigo hicho kiliwakera viongozi wa klabu hiyo kukiwa na madai kuwa
kilitokana na uzembe au makusudi.
Kiongozi mmoja wa Simba alisema kwamba pamoja na
upungufu mwengine ambao kipa huyo amekuwa akihusishwa nao, mazingira ya
mabao mawili dhidi ya Yanga, ndiyo yamemwondoa Msimbazi.
“Hivi unavyomfahamu wewe Kaseja anaweza kufungwa mabao kama yale? Kwa
kweli hilo limetuacha na maswali mengi kichwani, imetukera sana, mwache
aende zake,” alisema.
Akienda mbali zaidi, kiongozi huyo alisema ingekuwa vizuri zaidi kama
Kaseja angeweza kuonesha umahiri wake na kuondoa dhana mbovu dhidi yake,
lakini kitendo cha kukubali nyavu zake kutikiswa kilitoa jawabu juu ya
maswali waliyokuwa nayo.
Siku za karibuni kumekuwa na utata juu ya Kaseja kubaki Msimbazi baada
ya mkataba wake kufikia mwisho huku akizua mgawanyiko miongoni mwa
wajumbe wa Kamati ya Usajili kwa wengine kutaka asajiliwe na wengine
wakitaka aachwe.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa klabu hiyo Alhaj Ismail Aden Rage, Kaimu
Makamu Joseph Itang’are ‘Kinesi’ na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili,
Zakaria Hanspoppe, kwa nyakati tofauti walisema Kaseja hawezi kuongezewa
mkataba.
Viongozi hao walitoa kauli hizo bila ya kueleza wazi sababu za
kumuacha kipa huyo namba moja wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ ambaye
ameitumikia klabu hiyo karibu miaka 10.
Hayo yakiendelea, Kaseja mwenyewe ameendelea kuwa kimya kwani katikati
ya wiki alitafutwa na mwandishi wa habari hizi na hakuwa tayari kusema
lolote, ingawa kuna habari kuwa huenda akatua Coastal Union ya Tanga au
Mtibwa Sugar ya Turiani.
Aidha, Yanga imemnasa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Husssein Javu ambaye pia alikuwa akiwaniwa na Simba.
Habari kutoka Yanga, zinasema nyota huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo.
Aidha, Yanga pia imemnyakua kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ ambaye
anafanya timu hiyo kuwa na makipa watatu; Ali Mustafa ‘Barthez’ na Yusuf
Abdallah ambaye amepandishwa toka timu ya Vijana ya Yanga.
Imeelezwa kwamba, Yanga imeamua kufuta mpango wa kumuongeza mkataba
kipa wa kimataifa, Mghana Yaw Berko baada ya kocha mkuu wa timu hiyo,
Ernie Brandts kumkataa

Post a Comment