ad

ad

UKIWACHUKIA BARCELONA, MESSI LAZIMA UKONDE, AC MILAN YATUPWA NJE CHAMPIONS LEAGUE …HISTORIA MPYA YAANDIKWA

VILLA THRILLER ... David Villa hails Messi
DAKIKA ya 5 Lionel Messi anaifungia Barcelona bao kwanza, AC Milan wanachukulia poa na kujiona bado wako mchezoni, dakika ya 40 Messi tena linakuwa bao la pili, timu zinakwenda mapumziko 2-0.
Kipindi cha pili kinaanza, Barcelona wanagonga pasi za ajabu, Messi anafanya atakavyo, dakika ya 55 anatoa pasi iliyosababisha goli lililofungwa na David Villa, AC Milan wanacharuka lakini wanakuwa wamechelewa, wanapigwa bao la nne katika dakika ya mwisho ya mchezo kupitia kwa beki wa kushoto Jordi Alba.
David Villa
Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika dimba la Nou Camp palipochezwa mchezo mkali wa marudiano wa ligi ya Mabingwa Ulaya na kutoa matokeo yaliyowaduwaza wengi.
Ukichanganya magoli 2-0 ya AC Milan katika mchezo wa kwanza uliofanyika San siro, Barcelona wanasonga mbele kwa jumla ya mabao 4-2.
Barcelona wanaandika historia na kuwa timu ya kwanza katika michuano ya klabu bingwa Ulaya kuingia uwanjani wakiwa nyuma 2-0 na kasha kusonga mbele. Hakuna timu iliyowahi kufanya hivyo.
Barcelona walihesabiwa kama wameshatolewa wiki mbili zilizopita, lakini juzi Messi alitoa tahadhari kuwa kwa wale wote wanaodhani kuwa wamesambaratika basi wajue wanajidanganya.
Chanzo saluti 5-Tanzania
Powered by Blogger.