HAKUNA KAMA MESSI …ATWAA TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA KWA MARA YA 4 MFULULIZO
LIONEL Messi ameweka rekodi mpya ya kuwa mtu wa kwanza katika historia ya soka kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia ‘Ballon d'Or’ kwa mwaka wa nne mfululizo.
Messi akipokea tuzo yake ya nne mfululizo
Messi
mwenye umri wa miaka 25 ametwaa tuzo hiyo iliyokuwa pia inawaniwa na
Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Andres Iniesta wa Barcelona.
Kwa kushinda tuzo hiyo, Messi ambaye hivi karibuni alivunja rekodi ya miaka 40 ya Gerd Muller kwa
kufunga magoli 91 ndani ya mwaka mmoja, anafanikwa kuwaacha nyuma nyota
wa zamani wa Uholanzi Johan Cruyff na Marco Van Basten pamoja na
mfaransa Michel Platini (Rais wa sasa wa UEFA) walioshinda tuzo ya
Ballon d'Or mara tatu.
Ronaldo, Iniesta, Messi wakiwa katika picha ya pamoja
“Kusema kweli, kushinda tuzo hii mara nne ni jambo la kustaajabisha, ni heshima kubwa ambayo siwezi kuizungumzia” alisema Messi
“Napenda
kutoa shukrani zangu kwa wachezaji wenzangu wa Barcelona, Andres
Iniesta imekuwa ni faida sana kucheza na kufanya mazoezi pamoja nawe,
nakushukuru sana.
“Pia
nawashukuru wenzangu katika timu ya taifa ya Argentina, kuanzia
wachezaji, makocha na wote niliofanya nao kazi” alisema Messi.
Kocha
wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente Del Bosque alishinda tuzo ya
kocha bora na kuwashinda Pep Guardiola na Jose Mourinho wa Real Madrid
ambaye hakuhudhuria sherehe hizo.
Messi katika tuzo zake tatu zilizopita
Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo alisema kama atashinda itakuwa poa, akishindwa hakuna noma, maisha yanaendelea.
“Hata
hivyo lazima nikiri kuwa ningependa kushinda tuzo hii, nisiwe mnafiki
juu ya hilo” alisema Nyota huyo wa zamani wa Manchester United muda
mfupi kabla ya tuzo hizo kutolewa.
“Iwe
kihalali au kinyume chake, matokeo yataendelea kusimama kama yalivyo,
naweza nikawa mtu wa furaha au huzuni, hayo ndio maisha” aliongeza.
Kikosi cha wachezaji 11 bora wa dunia
Katika
sherehe hizo zilizofanyika nchini Uswisi, kilitajwa kikosi cha
wachezaji 11 bora wa dunia ambako hakuna hata mchezaji mmoja aliyetoka
nje ya ligi kuu ya Hispania.
Kikosi hicho ni: Casillas
(Real Madrid), Alves (Barcelona), Pique (Barcelona), Ramos (Real
Madrid), Marcelo (Real Madrid), Xavi (Barcelona), Alonso (Real Madrid),
Iniesta (Barcelona), Messi (Barcelona), Ronaldo (Real Madrid), Falcao
(Atletico Madrid).
Post a Comment