ad

ad

Kajala Amkimbia Zari Ukumbini Kisa Wivu wa Mapenzi!

BAADA ya kuenea taarifa kwa muda mrefu kuwa hawapikiki chungu kimoja, staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja amedhihirisha msemo huo baada ya kumkimbia ukumbini mjasiriamali maarufu Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. 

Kwa mujibu wa chanzo kilichokuwepo eneo la tukio hilo lililojiri katika Ukumbi Cardinal Rugambwa Hall maeneo ya Oysterbay hivi karibuni, Kajala alikuwa mmoja kati ya mastaa waalikwa katika sherehe ya harusi na alipofika ukumbini alikaa siti ya nyuma. 


“Hatukuwa tukijua kama Kajala naye amealikwa. Aliingia ukumbini na kusalimiana na mastaa wenzake kadhaa kisha akaenda kuketi siti ya nyuma kabisa akifuatilia sherehe inavyoenda,” kilisema chanzo hicho. 


Chanzo kiliendelea kupenyeza ubuyu kuwa, wakati shangwe zikiendelea ukumbini hapo ilifika muda wa kufungua shampeni ambapo mastaa kibao walienda mbele akiwemo msanii wa Bongo Fleva pamoja na mzazi mwenziye, Zari na baada ya muda MC alimuita Kajala naye ajumuike nao. 


“Hapo ndipo Kajala akaona isiwe tabu, akainama na kupitia mlango wa nyuma kisha akaondoka zake na kuwaacha na mshangao,” kilimaliza chanzo. 


Baada ya kunasa ubuyu huo, Ijumaa lilimnyanyulia simu Kajala kumuuliza kama kuna ukweli ndani yake ambapo alijibu;
“Ni kweli nilikwenda kwenye hiyo harusi na nikaitwa mbele lakini niliamua kuondoka zangu kwa sababu sikutaka kuonana na baadhi ya watu (Zari).”

No comments

Powered by Blogger.