Wema Sepetu Aibua Sitofahamu Kisa Tindu Lissu
Wema Sepetu.
Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa Wema ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, taarifa hizo zilimchangaya hasa ukizingatia kuwa Lissu ni ndugu yake na pia ni wakili wake katika kesi inayomkabili ya matumizi ya madawa ya kulevya.
“Taarifa za Lissu kupigwa risasi zilimchanganya sana Wema. Tangu apate taarifa hizo amekuwa akilia sana hadi kila mtu akaogopa. Tulihisi anaweza akapoteza fahamu au akapata ugonjwa hivyo tulitaka kumpeleka hospitalini, akapumzishwe,” kilisema chanzo hicho.
Tundu Lissu.
“Huwezi kuamini, sasa Wema amekuwa ni mtu wa kusali tu akimuomba Mungu ampe Lissu ahueni na hali yake ilirudi kama zamani,” kilisema chanzo.
Katika kutafuta ukweli wa ishu hiyo, Ijumaa Wikienda lilimsaka Wema ili kuthibisha madai hayo ambapo alisema kuwa, hakuna kitu kilichomuuma kama hicho na bado kitaendelea kumuumiza hadi aone hali ya Lissu inatengemaa na kurudi kwenye majukumu yake ikiwemo kumtetea kwenye kesi yake.
“Naendelea kuumia hadi nitakapomuona Lissu akiwa katika hali nzuri kama mwanzoni,” alisema Wema.
Stori: IMELDA MTEMA | IJUMAA WIKIENDA|DAR
Post a Comment