SERENGETI WAKO SAWA, WAANZA KWA SARE DHIDI YA MALI, MABINGWA WA AFCON
Timu
ya soka ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti imeanza vizuri
michuano ya Kombe la Mataifa Afrika baada ya sare ya bila kufungana
dhidi ya mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Mali.
Boys
walionyesha kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu huku wakijilinda katika
kila idara katika mechi hiyo ya Afcon, michuano inayofanyika nchini
Gabon.
Mashambulizi
ya Boys yalikuwa ni yale ya kushitukiza lakini wakatumia muda mwingi
kujilinda kwa mipango dhidi ya Mali ambao wachezaji wake walikuwa na
maumbo makubwa zaidi.
Sare hiyo, inaifanya Serengeti kuanza vizuri michuano hiyo ikiwa imekujikusanyia pointi ya kwanza.
Post a Comment