ad

ad

SERENGETI WAKO SAWA, WAANZA KWA SARE DHIDI YA MALI, MABINGWA WA AFCON



Timu ya soka ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti imeanza vizuri michuano ya Kombe la Mataifa Afrika baada ya sare ya bila kufungana dhidi ya mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Mali.

Boys walionyesha kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu huku wakijilinda katika kila idara katika mechi hiyo ya Afcon, michuano inayofanyika nchini Gabon.

Mashambulizi ya Boys yalikuwa ni yale ya kushitukiza lakini wakatumia muda mwingi kujilinda kwa mipango dhidi ya Mali ambao wachezaji wake walikuwa na maumbo makubwa zaidi.


Sare hiyo, inaifanya Serengeti kuanza vizuri michuano hiyo ikiwa imekujikusanyia pointi ya kwanza.

No comments

Powered by Blogger.