MANJI AENDELEA KUSOTA CHINI YA ULINZI, AHOJIWA TENA UHAMIAJI
Huku
 kikosi cha Yanga kikishuka dimbani leo kuivaa Simba, Mwenyekiti wake, 
Yusuf Manji jana alikuwa akihojiwa na Jeshi la Uhamiaji kuhusu tuhuma za
 kuwa na hati za kusafiria za nchi mbili.
Habari
 zinasema kwamba, Manji jana alitumia karibu kutwa nzima katika ofisi za
 Uhamiaji akihojiwa na hakukuwa na taarifa yoyote ile kuhusu kufikishwa 
mahakamani au vinginevyo. Hadi saa 9:00 alasiri chanzo chetu kilidai 
Manji alikuwa bado anahojiwa. Hii ni mara ya pili anahojiwa ndani ya 
wiki moja.
Mmoja
 wa watu wa karibu wa Manji amesema kuwa, Manji jana alianza kuhojiwa na
 Uhamiaji asubuhi halafu kukawepo na taarifa taarifa za kufikishwa 
mahakamani lakini Uhamiaji haikutoa taarifa yoyote kuhusu suala hilo 
hadi jana usiku.
“Manji
 amepelekwa Uhamiaji kwa mahojiano labda akitoka huko ndipo anaweza 
kwenda mahakamani, lakini Uhamiaji hawajatueleza jambo lolote lile,” 
alisema.
Baada ya gazeti hili kusubiri kwa muda mrefu kujua hatima ya Manji, tulipokitafuta tena chanzo chetu kilisema;
“Bado
 anahojiwa na Uhamiaji na hatujui nini kitatokea lakini leo na 
ataendelea kuwa chini ya ulinzi kwani atarudi tena hospitalini.”
Hii
 ina maana Manji atabaki Hospitali ya Aga Khan chini ya uangalizi wa 
Uhamiaji hivyo leo hatokuwepo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuishuhudia
 Yanga ikicheza dhidi ya Simba katika Ligi Kuu Bara.
SOURCE: CHAMPIONI

Post a Comment