SAMATTA AWEKA REKODI NYINGINE YA EUROPA KWA WATANZANIA
Mshambuliaji wa KRC Genk, Mbwana Samatta ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Europa League hatua ya 32.
Hatua ya 32 ni ile hatua ya mtoano na timu zinalazimika kupamba kweli kufikia hapo.
Kikosi
cha Genk kutoka Ubelgiji kimefanikiwa kufuzu baada ya kuitwanga
Sassoulo ya Italia kwa mabao 2-0 licha ya timu hiyo kuwa ugenini.
Hivyo Genk inaungana na timu nyingine katika hatua ya mtoano ikiwemo Manchester United ya England.

Post a Comment