Lulu Diva Atambulisha Wimbo Wake wa ‘Milele’ Global TV
MUUZA sura kwenye video za
Kibongo, Lulu Abbas ‘Lulu Diva, amegeukia upande wa pili wa Bongo Fleva
kwa kuibuka na ngoma yake ya kwanza aliyomshirikisha Barnabas Elias maarufu ‘ Barnaba.
Wimbo wake huo umetungwa na msanii wa Bongo
Fleva, Barnaba na kutengeneza katika studio ya Barnaba. Katika
mahojiano na Global TV Lulu Diva amesema mashabiki wake waliomzoea
kumuona katika video mbalimbali kwa sasa watarajie ngoma kali kutoka
kwake kwa sasa ameanza na Milele na hivi karibuni ataachia video ya
wimbo wake aliyoitengenezea Afrika Kusini. Ametumia zaidi ya milioni 40
kutengeneza ngoma hiyo.
Pia amewaomba mashabiki wa Bongo Fleva ndani na nje ya nchi kudownload wimbo wake kupitia Mkito au Youtube.
Post a Comment