ad

ad

KIFO CHA MTU ASIYE NA HATIA - 08

 
Miaka minne baadaye:
Rufaa ilishakatwa na kesi ilikuwa bado  ikiunguruma  mahakamani kwa miaka minne!   Belinda aliendelea kutumia pesa  aliyokuwa nayo kuhakikisha Prosper anatoka gerezani, wakili wake alimhakikishia ni lazima angeshinda na kuwa huru.
 Maisha ya Belinda yalishabadilika   alinawiri na kupendeza, mtoto wake Alicia  alisoma shule ya watoto wadogo ya Modern Daycare Centre iliyoko Kijitonyama, ilikuwa ni shule nzuri iliyomfanya aongee kiingereza kizuri! wanaume wengi walimfuata Belinda na kumsumbua wakitaka kumuoa lakini yeye alikataa kwa sababu mbili kwanza aliamini  alikuwa ameambukizwa lakini kubwa zaidi mapenzi yake yalikuwa kwa Prosper kuliko mwanaume mwingine yeyote.
“Mom when is dad coming home? Why does he stay there all the time?”(Mama, baba atakuja lini nyumbani? Kwanini anakaa huko muda wote?) hilo ndilo lilikuwa swali la  Alicia kwa mama yake kila siku iliyokwenda kwa Mungu,  alikuwa ni mtoto mzuri wa sura lakini afya yake haikuwa nzuri sana, aliugua mara kwa mara na ugonjwa  wake haukujulikana! Homa hazikukatika katika maisha yake, Belinda alielewa kilichomsumbua mwanae, alijua ni lazima mtoto huyo alikuwa navyo virusi ambavyo alikuwa na uhakika vilimpata  kutoka kwa baba yake kupitia kwa  wakati wa kujifungua.
          *********************
Tarehe 22 mwezi wa Desemba  ndiyo siku ambayo hukumu ya Prosper ilitegemewa kutolewa baada ya muda wa miaka minne,   ilisikilizwa na jopo la Majaji   Belinda na mtoto wake walikuwepo mahakamani siku hiyo, tegemeo lao lilikuwa Prosper kuachiwa huru lakini tofauti na walivyotegemea walijikuta wakiondoka mahakamani wakilia machozi kwani Prosper alishindwa tena hivyo hukumu ya kunyongwa iliyotolewa miaka minne kabla  ikabaki palepale na alitegemewa kunyongwa siku mbili   baadaye! Belinda alilia mno.
“Belinda tafadhali nakuomba uje gerezani kesho tuongee vizuri juu ya jambo hili ,kuna kitu nataka kukueleza nataka kuongea na wewe kabla ya kifo changu na ninaomba uje na mwanangu!”
“Sawa!” Alijibu Belinda huku akilia machozi.
“Mom why are you crying?”(Mama kwanini unalia?) Alicia alimuuliza mama yake lakini hakupewa jibu.
Siku iliyofuata Belinda alikwenda gerezani  kuonana na  Prosper, alielezwa  kila kitu kilichotokea mpaka Prosper akawa muuaji, Belinda hakuamini alichokisikia kwa masikio yake.
“Sikuua Belinda naomba uniamini  ni mama na dada zangu waliofanya jambo hilo mimi nilikuwa shuleni!”
“Sasa kwanini ulikiri?”
“Nilimpenda sana mama  yangu na ninajua aliua kwa sababu ya kuteswa na baba!”
Habari hiyo ilimsikitisha sana Belinda usiku wa siku hiyo hakulala na  asubuhi ya Desemba 24 siku  ambayo   Prosper alitegemewa kuchomwa sindano ya sumu  majira ya saa 4:30  Belinda aliondoka asubuhi na mapema kwenda ofisini kwa wakili wake na wote waliondoka hadi kwa mwanasheria wa serikali na kumweleza kila kilichotokea mpaka Prosper akatiwa hatiani.
Mwanasheria alisikitika sana na kumpigia simu Rais ikatolewa barua ya kuzuia hukumu hiyo ilitakiwa  kuwahishwa gerezani kabla Prosper hajachomwa sindano ya  kifo, wakati wanapewa barua hiyo tayari ilikuwa saa 4:10 na Prosper alitegemewa kuchomwa sindano  dakika ishirini baadaye.
Kwa msaada wa gari alilopewa na mwanasheria mkuu  walifika gerezani saa 4:29:30 zikiwa zimebaki sekunde 30 tu  Prosper afe, Belinda alimkabidhi askari magereza mmoja barua hiyo.
“Imetoka wapi?”
“Kwa mwanasheria mkuu!”
“Ya nini?”
“Msimchome Prosper sindano ya sumu hana hatia!”
“Mh! Mh! Mh! Mmechelewa sana hivi sasa ni saa 4:30 kasoro sekunde  20 na anachomwa sindano saa 4:30 hatuwezi kuwahi!”
“Mzee jaribu kuwahi unaweza kumwokoa!” Belinda alisema akiwa amepiga magoti chini.
“Haya ngoja nijaribu lakini matumaini ni kidogo!”
Aliondoka askari huyo akikimbia mbio kwenda ndani ya gereza huku akipiga kelele! Alijua muda huo lazima mzee nyonganyonga alikuwa akijiandaa kumchoma Prosper sindano!
          ***********************
“Kijana nakuonea huruma sana lakini inabidi tu nitimize wajibu wangu wa kukuchoma sindano hii ya sumu, nisamehe sana kukuondoka duniani, haya si mapenzi yangu!” Alisema mzee nyonganyonga kabla hajamchoma sindano hiyo.
“Choma tu mzee!” Prosper alisema kwa sauti ya unyonge lakini mawazo yake yalikuwa kwa Belinda na mwanae alijua kifo chao kingekuwa cha mateso kuliko chake!
“Haya moja! Mbili….tat….!”

Prosper alilala juu ya kitanda cha chuma pembeni yake akiwa amesimama mzee Nyonganyonga ambaye kazi yake ilikuwa ni kuondoa uhai wa binadamu wenzake! Alilipwa mshahara mkubwa kwa kazi hiyo, prosper alishangaa kuona mzee huyo hamchomi sindano ingawa alikuwa nayo mkononi mwake na muda wa yeye kuchomwa ulishafika alishindwa kuelewa ni kwanini mzee huyo alishindwa  kutelekeza wajibu wake.
Prosper alitamani kufa hakutaka kuishi zaidi aliogopa sana kupambana na tatizo la ugojwa wa Ukimwi uliokuwa mbele yake, aliamini hakuwa na uwezo wa kuyastahimili matatizo yanayoambatana na ugonjwa huo!Alijilaumu kwa uamuzi wake wa kukubali kushiriki maisha ya kishoga na mfungwa mwenzake  Savimbi ambaye ndiye aliyemwambukiza ugonjwa huo.
“Natamani nisife! Napenda niishi na familia yangu lakini sipo tayari kushuhudia nikikonda taratibu hadi kifo changu!”Aliwaza prosper na aliponyanyua uso wake kumwangalia mzee nyonganyonga alishangaa kukuta sindano ikiwa imezama tumboni kwake mwenyewe.
“Nime…cho….shwa na ….kazi ya ku…..ua ….bina…damu wenza…..ngu! Nita…..mwe..leza nini Mu….ngu ni heri nife sitaki kuitoa roho yako wa sababu huna hatia!” alisema mzee nyonganyonga akiangakua chini na mwili wake kukakamaa na ulimi kutoka nje.
“Mzee nyonganyonga umefanyua nini sasa? Kwanini umejiua wewe wakati ni mimi ninayestahili kufa?”Aliuliza prosper huku akipiga kelele alishindwa kufanya lolote kwa sababu alibanwa na mashine mikononi na miguuni, alianza kupiga kelele kuomba msaada na muda mfupi baadaye waliingia maaskari wawili mmoja akiwa na barua mkononi.
“Vipi kimetokea nini tena?”
“Hata mimi nashangaa nilikuwa nimefumba macho nikisubiri kuchomwa sindano lakini mzee nyonganyonga hakufanya hivyo na nilipofumbua nilikuta sindano imezama tumboni mwake na akaanguka chini!”
“Kweli?”
“Ndiyo! Sasa mnafikiri ni mimi ndiye nimemchoma?”
“Hapana siyo hivyo ila….!”
“Ila nini?”
”Basi tuyaache hayo kakueleza kitu chochote kabla hajajichoma?”
“Alipaanguka chini alianza kusema maneno ingawa kwa shida!”
“Alisema maneno gani?”
“Alisema amechoshwa  na kazi ya kuua binadamu wenzake na hakuwa na jambo la kumjibu Mungu!”
“Mungu wangu! Sasa kwanini asingesema tu akabadilishiwa kazi?”
Prosper alibaki ameduwaa akiwashangaa maaskari walionekana kupigwa na mshangao mkubwa na hawakujua ni nini cha kufanya, mzee nyonganyonga alikuwa amelala chini sakafuni, mikono na miguu yake ikiwa imenyooka kuelekea darini! Macho na ulimi wake yakiwa yametoka nje alitisha na picha hiyo ilimuonyesha prosper ni kifo cha aina gani ambacho angekufa.
Aliogopa kupita kiasi na kujikuta akitetemeka mwili mzima lakini kwa sababu alishaamua kufa ili kukwepa mateso ya gonjwa la Ukimwi prosper aliamua kuipuuzia picha aliyoiona sakafuni na kuwageukia maaskari waliokuwa ndani ya chumba hicho.
“Afande!” Aliita na maaskari wote waliokuwa  wameinamisha nyuso zao chini wakiushangaa mwili wa mzee nyonganyonga uliolala sakafuni waligeuka kumwangalia.
“Unasemaje prosper?”Wote waliuliza kwa mpigo.
“Sasa mtafanya nini?”
“Kuhusu?”
”Mimi nataka kufa!”
“Hautakufa tena prosper bado una siku nyingi sana za kuishi!”
”Si uchukue hilo bomba la sindano uvute dawa nyingine unidunge kipi kinachokushinda kama mnaogopa basi nitoeni hapa kwenye mashine nijidunge mwenyewe!”
“Haiwezekani tena prosper serikali imeamua kusitisha hukumu ya kifo uliyopewa tena una bahati nafikiri Mungu alikuwa hajapanga ufe kwa sababu mkeo amefika hapa na barua zikiwa zimebaki sekunde ishirini tu! Hapakuwa na njia yoyote ya kuwahi kama mzee Nyonganyonga asingejiua mwenyewe!” alisema mmoja wa maaskari.
“Ni nini mnasema nini nyinyi mbona siwaelewi?”
“Barua ni hii hapa imetoka kwa mwanasheria mkuu wa serikali hivyo haiwezekani kukuchoma sindano tena!”
“Hebu niione hiyo barua!”Alisema prosper kwa ukali kiasi kwamba maaskari walishindwa kumwelewa kwa sababu alitakiwa kufurahia kukwepa kifo akiwa juu ya kitanda cha mauti.
Askari aliyekuwa na barua hiyo mikononi alimsogezea prosper na kuifungua, prosper alianza kuipitia taratibu tangu mwanzo  hadi mwisho wa barua lakini badala ya kufurahia alianza kupiga kelele.
“NATAKA KUFA!NATAKA KUFA! MIMI NATAKA KUFA SITAKI TENA KUISHI!” aliongea kwa sauti ya juu huku akijaribu kujitoa kwenye mashine iliyoshika mikono na miguu yake.
Maaskari waliamua kumfungua prosper akatoka kitandani na kusimama wima, wakiwa hawa hili wala lile maaskari walishtukia prosper anatimua mbio kulifuata bomba lililokuwa chini lengo lake likiwa ni kujichoma  nalo ili afe alilifikia na kulishika lakini kabla hajalinyanyua na kutimiza azma yake mguu wa askari ulisimama juu ya kiganja chake prosper alipiga kelele sababu ya maumivu aliyoyapata.
“Kwanini unataka kufanya hivyo lakini yaani badala ya kufurahia amenusurika kifo kimiujiza unataka kufanya ujinga?”
“Braza mimi ni mtu mzima na akili zangu ukiona nataka kufanya jambo jiulize mara mbili kuna tatizo gani, hakuna mtu anayetaka kufa binadamu wote tunapenda kuishi! Kwa hiyo niache mimi nifanye ninavyotaka!”
“Haiwezekani! Afande hebu mtoe huyu chumbani mpeleke katika chumba cha washauri nasha nafikiri utakuwa na tatizo ambalo ni vyema tukalifahamu!”
Askari magereza alimshika mkono prosper ambaye wakati huo aliendelea kulia mfululizo na kutoka naye hadi nje ya chumba cha kifo mbele kidogo  aliingia naye katika chumba kilichoandikwa mlangoni “Ushauri Nasaha!” ambao walimkuta mama wa makamo akiwa amekaa nyuma ya meza kubwa.
“Vipi tena?”
“Hukumu yake ya kifo imesitishwa na serikali baada ya kugundulika dakika chache kabla ya kifo kuwa hakutenda kosa lililopelekea apewe hukumu hiyo!”
“Hongera sana kijana nakushauri ukitoka hapa uwe mwema mbele za Mungu kwani amekupa nafasi nyingine ya kunyoosha njia zako unasikia?”
“Usinipe hongera mama mimi sitaki kuishi  na kama kuna uwezekano wa kuniua sasa hivi fanyeni hivyo haraka kwani nitajiua mwenyewe!”
Jipu la prosper lilimshtua mtoa ushauri nasaha, aligundua prosper alikuwa na tatizo kubwa lililohitaji muda mrefu wa kuongea naye!
“Kwanza hebu tufahamiane mimi naitwa mama  Mpelumbe wewe mwenzangu unaitwa nani?” Mama huyo alianzaia mbali kidogo.
“Naitwa prosper!”
“Aisee wewe ndiye prosper?”
“Ndiyo mama ni vizuri ukiniita marehemu prosper sababu tayari nimeshakufa! Mimi ni maiti inayotembea!”
”Unamaanisha nini mwanangu?”
“Yaani mama hunielewi ninaposema mimi ni maiti inayotembea!”
‘Sikuelewi hata kidogo!”
“Na si mimi tu hivi sasa vijana wengi ni maiti zinazotembea! Ndiyo maana nataka kufa kwa sababu yaliyoko mbele yangu sitaweza kuyahimili!”
”Unamaanisha nini?”
Badala ya kujibu swali prosper aliyekuwa ametulia alianza kulia machozi.


Belinda alikaa nje ya gereza na mtoto wake mgongoni akiendelea kulia machozi!Alishangaa ni kwanini maaskari walichelewa kiasi hicho kurudi kutoka ndani, alijua kwa vyovyote mume wake alikuwa amekufa! Mawazo hayo yalimzidishia huzuni aliamini asingeweza kupambana na maisha peke yake aliumia juhudi zake zote za kumuokoa prosper zilikuwa zimegonga mwamba.
Ndani na nje ya moyo wake Belinda hakutaka kabisa prosper anyongwe alitaka aendelee kuishi tena wakiwa pamoja na mtoto wao wakisubiri kifo chao ifike n aikiwezekana wafe siku moja! Hakuwa tayari  kubaki peke yake duniani akiteseka kumuuguza mtoto wao Alicia pia hakutaka kufa na kumwacha Alicia peke yake duniani kama yeye ndiye angetangulia.
Kifo ni kifo  lakini sitaki Prospar afe ghafla  kiasi  hicho  nataka niwe naye niteseke naye  hadi mwisho  wa maisha  yangu! Prospar  hana hatia na hastahili kunyongwa!” aliwaza Belinda .
Mom where  is dady? Whay  is not coming? I wanna talk  to  him please  mom tell  them  to call him  for us”(mama baba yuko wapi? Kwa nini  haji?  Nataka kuongea naye  waambie basi wamwite!) Alicia aliyekuwa  mgongoni kwa mama  yake  alisema maneno  yaliyomuumiza moyo mama yake.
 Badala  ya  kujibu  swali lake  Belinda  aliangua  kilio  kilichomfanya  mtoto wake bila  kujua  kilichomliza mama  yake naye aanze  kulia. Alicia  alimpenda mno mama yake hakuwa tayari kumwona akilia.
“Mom stop Craying! Remember Christimas  is just  one day  from to day  and dady will be home  to celeblate  with us,  that   is what he told  me the  last time  we came  here! He also peomised  to buy me a  new  dress!”  (Mama acha  kulia! Kumbuka krisimasi ni siku moja tu kuanzia leo  na baba  aliahidi kuja nyumbani  kusherekea pamoja nasi! Aliniambia  hivyo mara ya mwisho  tulipokuja na aliniahidi  ataninunulia gauni jipya!) Alicia  alisema  hayo bila kujua siku hiyo ndio baba yake alikuwa ananyongwa.!
Kufungwa na kuhukumiwa kifo cha prosper ndicho Belinda hakutata kabisa mtoto wake akijue aliamua kulifanya jambo hilo siri kwa sababu hakutaka kumuumiza moyo mtoto wake aliyeonekana kumpenda sana baba yake, siku zote alimwambia baba yake alikuwa gerezani kufanya kazi na alikuwa hapewi likizo sababu ya kazi nyingi.
Ghafla akiwa katika mawazo hayo Belinda alitupa macho yake upande wake wa kulia kupitia katika dirisha lenye nondo nene lililokuwa pembeni yake, alishuhudia mwili wa mtu ukiwa umebebwa na maaskari wasiopungua wanne ukitolewa ndani  ya chumba na kupelekwa upande wa pili kulikokuwa na kijumba kidogo, ukutani mwa kijumba hicho kuliandikwa maneno “Mortuary!”
Picha hiyo ilimwonyesha Belinda wazi kuwa tayari mume na baba wa mtoto wake tayari alishaaga dunia, aliiona dunia imekuwa giza mwili wake ukalegea na ghafla alianguka chini akiwa na mtoto wake mgongoni.
“Mom!Mom! Mom! What has happen with you? Have you fallen asleep? Please wake up mom is time to go home and do chrismas preparation remember dad will be here in no time!(Mama! Mama!Mama! nini kimekupata? Umelala usingizi? Amka basi muda wa kwenda nyumban kujiandaa na krismasi umefika na baba atakuja hapa muda si mrefu!)Alicia aliongea huku akimpiga piga  mama yake mgongoni lakini Belinda hakushtuka.

No comments

Powered by Blogger.