KIFO CHA MTU ASIYE NA HATIA - 05
“Na wewe hicho kitoto chako unakipeleka wapi?” Walimuuliza Belinda kwa kejeli lakini hakuwajibu kitu alizidi kusonga mbele kuelekea nyumba kubwa waliyoishi.
Alikuwa nyumbani kwao kwa mara nyingine baada ya kukaa na kuteseka nje kwa muda mrefu, hakujua ni kitu gani kingetokea baada ya kukutana na baba yake lakini hilo hakulipa nafasi sana, alichotaka ni kukutana na baba yake na kumuomba msamaha basi!
Kabla hajaingia ndani mlango ulifunguliwa na baba yake alitoka nje na kumkuta, palepale sura yake ilibadilika.

Belinda aliendelea kulia akiwa amemshika mtoto wake Alicia mkononi na Prosper aliendelea kumbembeleza asilie lakini hakusaidia kitu! Kadri alivyobembelezwa ndivyo Belinda alivyozidi kutokwa na machozi, alilia akimwangalia mtoto wake kwa macho ya huruma.
Alikuwa na wasiwasi na hofu kubwa sana moyoni mwake, alijua kama kweli kifo cha Savimbi kilisababishwa na Ukimwi basi hata Prosper alikuwa ameambukizwa! Na kama Prosper alikuwa ameambukizwa Belinda alikuwa na wasiwasi ni lazima na yeye pia alikuwa ameathirika kwa sababu alikutana naye kimwili na matokeo yake yakawa mimba iliyowapa mtoto wao Alicia.
Wasiwasi wake haukuishia hapo ulivuka mpaka hadi kwa mtoto wao, Belinda alijua kama yeye alikuwa ameathirika lazima na mtoto wao pia alikuwa katika hali hiyohiyo! Hakuna kitu alichokiogopa maishani mwake kama ugonjwa wa Ukimwi! Aliujua ulivyotesa watu kabla ya vifo vyao, roho ilimuuma sana Belinda na kujikuta akimwaga machozi na kumtupia lawama nyingi Prosper.
“Prosper kwanini ulijiingiza katika mchezo huo na Savimbi?” Belinda aliuliza.
Badala ya kujibu swali aliloulizwa Prosper aliinamisha kichwa chini na kuendelea kulia, moyoni mwake alikuwa na maumivu makali na alijuta kwa uamuzi aliouchukua, hakuwa na namna ya kujitetea mbele ya Belinda, aliyoambiwa yote yalikuwa kweli tupu!
“Prosper naomba unijibu swali langu!”
“Darling huu sio wakati wa kunilaumu ninahitaji msamaha wako na msaada mkubwa wa mawazo! Niliingia katika mtego bila kujua hata mimi ninajuta! Nina uhakika nimeambukizwa na mwisho wa maisha yangu upo karibu, ingawa najua nitanyongwa kwa kesi niliyonayo Mahakamani nisingependa hata kidogo kufa kwa Ukimwi! Nisamehe mke wangu” Alisema Prosper huku akilia.
Maneno ya Prosper yaliuchoma moyo wa Belinda na kumfanya agundue kuwa kweli hakutakiwa kumtupia lawama nyingi kiasi hicho kwa wakati mgumu aliokuwa nao! Hilo alilifahamu lakini bado maumivu yaliendelea kuwepo moyoni mwake, hakutaka kuukubali ukweli kuwa alikuwa ameambukizwa Ukimwi na hakuwa tayari kulipokea jibu hilo hata kama angepimwa.
Moyo wa Belinda haukuwa tayari kwa matokeo ya Ukimwi na alijua angekuwa marehemu siku moja baada ya kupewa majibu ya damu! Jambo ambalo hakutaka kabisa litokee kwa sababu kufanya hivyo kungemaanisha mateso kwa mtoto wake Alicia ambaye angekuwa Yatima tangu siku hiyo.
Alipenda sana kujua hali yake kiafya lakini aliogopa kupima damu! Alichofanya Belinda ni kumshawishi Prosper apime na majibu ambayo angepata ndiyo yangeonyesha kama alikuwa ameambukizwa au la!
“Lakini kuna watu huwa wanatembea na watu wenye virusi vya Ukimwi na hawaambukizwi, acha nisimtupie lawama nyingi sana Prosper mpaka apime damu yake inawazekana hakuambukizwa lakini hata kama ni hivyo nitawezaje kuwa na mwanaume shoga?” Alijiuliza Belinda bila kupata majibu ya maswali yake na machozi yaliendelea kumbubujika.
Muda mfupi baadaye huku Prosper na Belinda wakiendelea kulia mlango wa chumba ulifunguliwa na maaskari Magereza wawili wakaingia hadi ndani ya chumba walichokuwa wameketi Belinda na Prosper.
“Dada muda umekwisha tunakuomba sasa uondoke!” Alisema mmoja wa askari Magereza, mwanamke mwenye umri kati ya miaka ishirini na tano hadi thelathini aliyemwangalia Belinda kwa macho ya huruma.
“Ahsante dada naondoka sasa hivi!” Alijibu Belinda huku akinyanyuka na kumfunga mtoto wake mgongoni kwa kutumia khanga ndogo ya India.
“Belinda umenisamehe mke wangu?” Prosper aliuliza wakati maaskari wakimnyanyua kutoka sakafuni alipokaa.
Belinda hakulijibu swali hilo alianza kutembea kuelekea nje ya Gereza, kichwani kwake kulijaa mawazo mengi kupita kiasi! Mbele yake aliona giza, kimawazo alijiona tayari yupo kitandani hoi akiugua Ukimwi kwa sababu tu ya uzembe wa Prosper!
“Wanawake wengi sana wanaponzwa na wanaume zao katika suala hili la Ukimwi, nimejitahidi kadri ya uwezo kuwa mwaminifu kwa Prosper lakini ameniangusha!” Aliwaza Belinda akitembea kuelekea kituo cha basi.
Mwili wa Belinda ulikuwa bado ukitoa harufu kwa sababu ya tundu alilolipata wakati wa kujifungua, kabla hajafika kituo cha basi kumbukumbu juu ya matatizo yaliyompata katika mabasi aliyopanda zilimrejea kichwani mwake, hakutaka kuzomewa tena na hakutaka tatizo lake limsumbue wala kumkosesha raha mtu yeyote! Kwa sababu hiyo Belinda aliamua kutembea kwa miguu kuelekea mjini Tabora.
****************
Aliingia Tabora mjini saa nane mchana jua likiwa linawaka kweli kweli, alitafuta kivuli na kuketi huku akitafakari nini cha kufanya, alipofikiria kwenda hospitali ya Kitete moja kwa moja alishindwa kwa sababu zilikuwa zimebaki siku saba kutimiza mwezi kabla hajarudi, alijua manesi wasingempokea mpaka tarehe aliyopewa kurudi hospitali ifike!
Uamuzi uliomwijia akilini mwake wakati huo ni kwenda kijijini Tutuo kusubiri mpaka tarehe ifike ndiyo aende hospitali kurekebishwa tundu lake, alisubiri kwa hamu kubwa sana siku hiyo! Alitamani sana kupona na kurejea katika hali yake ya kawaida, alikuwa amechoshwa na kuzomewa pamoja na masimango aliyokuwa akiyapata.
“Na hili tundu ni kipimo tosha kama nina virusi vya Ukimwi au la! likipona nitakuwa sijaambukizwa lakini likikataa kupona nitakuwa navyo!” Belinda aliwaza kulingana na taarifa zilizokuwepo mitaani juu ya uponaji wa vidonda vya watu wenye Ukimwi.
Baada ya kuwaza kwa muda mrefu akiwa amekaa chini ya mti wa Mwembe karibu kabisa na shule ya sekondari ya Mihayo, Belinda alinyanyuka na kuamua kutembea hadi kituo cha basi ambako alipanda basi lililomfikisha hadi kijijini Tutuo, mtoto wake Alicia alilia kwa njaa lakini Belinda hakuwa na kitu cha kufanya ilikuwa ni mpaka afike nyumbani kwao na Prosper ndipo apike uji na kumpa.
Alisababisha usumbufu mkubwa sana ndani ya basi lakini hakuna mtu aliyegundua kuwa ni yeye aliyesababisha hali hiyo itokee, alipoteremka kituoni alitembea moja kwa moja hadi nyumbani kwao na Prosper, njiani watu wengi walionekana kumshangaa na hakuelewa sababu ilikuwa ni nini! Aliifananisha hali hiyo na mara ya mwisho alipokuja kijijini na kukuta mama yao Prosper amefariki.
“Sijui kimetokea nini tena leo?” Alijiuliza Belinda.
Mita chache kabla hajafika nyumbani alishangaa kuona ukuta mkubwa wa mabati ukiwa umekizunguka kiwanja chote cha nyumba ya akina Prosper! Belinda alishindwa kuelewa ni nini kilitokea ila alijua lazima kulikuwa na tatizo na aligundua ni kwanini watu walikuwa wakimshangaa.
“Nikusaidie dada?” Aliuliza mtu aliyemkuta mahali pale, aliyeonekana kama mlinzi.
“Nauliza waliokuwa wakiishi hapa wamehamia wapi?”
“Walikiuza kiwanja chao kwa mwarabu mzee Mohamed na sijui wamehamia wapi!”
Belinda aliishiwa nguvu miguuni na kujikuta amekaa chini bila kujua la kufanya, alishindwa kuelewa angekwenda nyumbani kwa nani na kuishi mpaka tarehe ya kwenda hospitali ifike! Kwa hali aliyokuwa nayo na harufu aliyoitoa alijua kusingekuwa na mtu ambaye si ndugu kijijini pale ambaye angevumilia kuishi naye ndani ya nyumba yake.
“Kwani vipi dada?”
“Kwani wewe hunifahamu mimi?”
“Ndiyo nilikuwa nakuona nyumbani kwa Mwarabu Mzee Mohamed lakini sikufahamu vizuri!”
“Nilikuwa naishi hapa na akina Nyamizi na Kasanda kabla sijaanza kazi nyumbani kwa Mwarabu mzee Mohamed, niliacha kazi nilipotakiwa kwenda kujifungua na baada ya hapo nilikwenda nyumbani kwetu Dar es Salaam na sasa nimerudi tena Tutuo nategemeo langu lilikuwa kufikia hapa hapa!” Alisema Belinda huku akimtoa mtoto wake aliyekuwa akilia mgongoni na kujaribu kumnyonyesha lakini maziwa hayakuwemo kifuani kwake.
“Ukweli ndio huo dada sasa sijui utafanya nini!”
“Kaka yangu nina matatizo makubwa nafikiri hata hapo ulipo unasikia harufu ninayotoa, ni kazi ngumu sana kwa mtu yeyote kuishi na mimi ndani! Ninatakiwa hospitali ya Kitete kutibiwa ugonjwa wangu siku saba kuanzia leo yaani tarehe nne, ninachokuomba kama binadamu mwenzangu mwenye huruma nisaidie niwe naishi hapa ndani mpaka siku hiyo ifike!”
“Dada lakini nyumba hii itabomolewa tarehe tatu! Ninaweza kukusaidia mpaka tarehe mbili baada ya hapo itabidi utafute utaratibu mwingine sababu mzee Mohamed anataka kuweka mashine zake za kusaga”
“Ahsante sana kaka na sijui nikushukuru vipi!”
“Usijali dada yangu matatizo ni ya wote, nyumbani kwangu ni kijiji jirani lakini nitakusaidia chakula mpaka hiyo tarehe mbili, kila nitakacholetewa na mke wangu tutakula pamoja!”
“Mungu akubariki sana kaka yangu!” Alisema Belinda huku akinyanyua mfuko wake wa rambo na kuingia ndani ya ngome ya mabati baada ya mlinzi kufungua mlango.
Nyumba ilikuwa haijabomolewa ila ndani yake hapakuwa na kitu chochote, si kitanda wala jamvi! Kasanda na Nyamizi walishachukua kila kitu, Belinda aliwashangaa sana wasichana hao kwa kitendo chao cha kuuza shamba na kumsahau kaka yao aliyekuwa gerezani.
Alichukua kitenge alichokuwa nacho ndani ya mfuko na kukitandika chini na yeye pamoja na mtoto wake wakalala na kujipumzisha, Alicia hakulala sababu ya njaa! Mlinzi ambaye baadaye Belinda alimtambua kwa jina la Juma alikuja ndani kuuliza ni nini kilikuwa kinasumbua.
“Ni njaa! Hajala kitu tangu jana na maziwa kifuani kwangu hayatoshi”
“Subiri nije!”
Mlinzi alitoka nje na aliporudi alikuwa na chupa ya maziwa na kumkabidhi Belinda.
“Mnyweshe hayo maziwa!”
“Ahsante sana kaka! Si ninahitaji kuyachemsha?”
“Ukiweza kufanya hivyo ni vizuri zaidi!”
Belinda aliipokea chupa na kuiweka pembeni alitamani kuyachemsha maziwa hayo lakini kwa sababu hakuwa na sufuria alishindwa na kulazimika kumnyesha Alicia maziwa ya baridi, alijua kulikuwa na magonjwa kama Kipindupindu, Kuhara, Kifua kikuu ambayo hutokana na kunywa maziwa yasiyochemshwa lakini yote hayo alimwachia Mungu.Baada ya kunywa maziwa hayo Alicia alitulia na kulala usingizi.
***************
Belinda alikaa ndani ya nyumba hiyo kwa msaada wa mlinzi Juma mpaka tarehe mbili nyumba ilipobomolewa! Hakuwa na mahali pa kuishi tena ilibidi ampe shukrani zake Juma na kupanda basi lililompeleka moja kwa moja hadi mjini Tabora, siku hiyo alishinda na kulala mtaani na siku iliyofuata saa kumi na mbili za asubuhi alikuwa ameshafika hospitali ya Kitete.
Saa mbili kamili aliingia katika chumba cha daktari aliyefurahi kumwona Belinda tena.
“Belinda mwanangu umerudi?”
“Ndiyo baba!”
“Pole sana najua umeteseka kiasi cha kutosha lakini mateso yako leo yanafikia mwisho!”
“Kweli baba?” Belinda alimuuliza daktari.
“Ndiyo mwanangu!” Alijibu daktari huku akiandika kitu fulani kwenye karatasi, alipomaliza alinyanyuka na kumwomba Belinda amfuate na waliongozana hadi katika chumba kilichoandikwa Laboratory! Wote wawili waliingia hadi ndani.
“Mzee Simba naomba umpime huyu binti damu!”
“Sawa daktari!”
“Daktari!” Belinda aliita.
“Naam Belinda!”
“Unataka kunipima damu?”
“Ndiyo! Ni lazima tujue!”
“Lakini mimi sitaki kufahamu!”
“Hutaki kufahamu nini?”
“Sitaki kufahamu kuwa nina virusi vya Ukimwi!”
“Siyo hivyo Belinda hatukupimi Ukimwi! Tunataka kufahamu una damu kiasi gani kwa sababu utafanyiwa operesheni leo”
“Kama ni hivyo sawa!” Aliitikia Belinda.
Daktari na mzee Simba wote waliangua kicheko kwa woga aliouonyesha Belinda.
“Kwanini mnaogopa sana kupimwa Ukimwi?” Daktari alimuuliza Belinda.
“Basi tu mimi sipendi!”
Usiku wa siku hiyo baada ya majibu kuwa mazuri Belinda alipelekwa chumba cha upasuaji na kurekebishwa kasoro yake akawa mwanamke kamili tena lakini wasiwasi wake uliendelea kuwa juu ya Ukimwi.
*****************
Mwezi mmoja baadaye:
Hali ya Belinda ilikuwa nzuri kabisa, hakuwa na harufu tena! Furaha ilijaa maishani mwake kasoro pekee iliyomchukulia sehemu ya furaha yake ni tatizo la Prosper! Lakini aliendelea kujipa moyo kuwa huenda Prosper hakuambukizwa virusi vya Ukimwi na Savimbi.
Uhakika pekee angeweza kuupata kwa kuongea na Prosper mwenyewe na kupata taarifa za majibu ya damu aliyomwomba apime! Baada ya kutoka hospitali aliamua kwenda moja kwa moja gerezani Isanga lengo lake likiwa kwenda kuyaona majibu ya damu ya Prosper.
*****************
Prosper alikuwa amekonda na alionekana mwenye mawazo mengi kupita kiasi na muda wote wakati wakiongea aliendelea kulia akimwomba Belinda msamaha kwa yote yaliyojitokeza.
“Prosper nieleze juu ya majibu yako ya damu!” Belinda aliuliza.
Walikuwa watu watatu tu ndani ya chumba Prosper alipoanza kueleza kila kitu kilichokuwa kikiendelea mwilini mwake.
“Nieleze kwanza juu ya majibu, hayo mambo ya homa na kuharisha yaache kwanza, nieleze kwanza juu ya majibu nataka kujua ukweli huo!” Belinda alizidi kumbana.
INAENDELEA
Alikuwa nyumbani kwao kwa mara nyingine baada ya kukaa na kuteseka nje kwa muda mrefu, hakujua ni kitu gani kingetokea baada ya kukutana na baba yake lakini hilo hakulipa nafasi sana, alichotaka ni kukutana na baba yake na kumuomba msamaha basi!
Kabla hajaingia ndani mlango ulifunguliwa na baba yake alitoka nje na kumkuta, palepale sura yake ilibadilika.

Belinda aliendelea kulia akiwa amemshika mtoto wake Alicia mkononi na Prosper aliendelea kumbembeleza asilie lakini hakusaidia kitu! Kadri alivyobembelezwa ndivyo Belinda alivyozidi kutokwa na machozi, alilia akimwangalia mtoto wake kwa macho ya huruma.
Alikuwa na wasiwasi na hofu kubwa sana moyoni mwake, alijua kama kweli kifo cha Savimbi kilisababishwa na Ukimwi basi hata Prosper alikuwa ameambukizwa! Na kama Prosper alikuwa ameambukizwa Belinda alikuwa na wasiwasi ni lazima na yeye pia alikuwa ameathirika kwa sababu alikutana naye kimwili na matokeo yake yakawa mimba iliyowapa mtoto wao Alicia.
Wasiwasi wake haukuishia hapo ulivuka mpaka hadi kwa mtoto wao, Belinda alijua kama yeye alikuwa ameathirika lazima na mtoto wao pia alikuwa katika hali hiyohiyo! Hakuna kitu alichokiogopa maishani mwake kama ugonjwa wa Ukimwi! Aliujua ulivyotesa watu kabla ya vifo vyao, roho ilimuuma sana Belinda na kujikuta akimwaga machozi na kumtupia lawama nyingi Prosper.
“Prosper kwanini ulijiingiza katika mchezo huo na Savimbi?” Belinda aliuliza.
Badala ya kujibu swali aliloulizwa Prosper aliinamisha kichwa chini na kuendelea kulia, moyoni mwake alikuwa na maumivu makali na alijuta kwa uamuzi aliouchukua, hakuwa na namna ya kujitetea mbele ya Belinda, aliyoambiwa yote yalikuwa kweli tupu!
“Prosper naomba unijibu swali langu!”
“Darling huu sio wakati wa kunilaumu ninahitaji msamaha wako na msaada mkubwa wa mawazo! Niliingia katika mtego bila kujua hata mimi ninajuta! Nina uhakika nimeambukizwa na mwisho wa maisha yangu upo karibu, ingawa najua nitanyongwa kwa kesi niliyonayo Mahakamani nisingependa hata kidogo kufa kwa Ukimwi! Nisamehe mke wangu” Alisema Prosper huku akilia.
Maneno ya Prosper yaliuchoma moyo wa Belinda na kumfanya agundue kuwa kweli hakutakiwa kumtupia lawama nyingi kiasi hicho kwa wakati mgumu aliokuwa nao! Hilo alilifahamu lakini bado maumivu yaliendelea kuwepo moyoni mwake, hakutaka kuukubali ukweli kuwa alikuwa ameambukizwa Ukimwi na hakuwa tayari kulipokea jibu hilo hata kama angepimwa.
Moyo wa Belinda haukuwa tayari kwa matokeo ya Ukimwi na alijua angekuwa marehemu siku moja baada ya kupewa majibu ya damu! Jambo ambalo hakutaka kabisa litokee kwa sababu kufanya hivyo kungemaanisha mateso kwa mtoto wake Alicia ambaye angekuwa Yatima tangu siku hiyo.
Alipenda sana kujua hali yake kiafya lakini aliogopa kupima damu! Alichofanya Belinda ni kumshawishi Prosper apime na majibu ambayo angepata ndiyo yangeonyesha kama alikuwa ameambukizwa au la!
“Lakini kuna watu huwa wanatembea na watu wenye virusi vya Ukimwi na hawaambukizwi, acha nisimtupie lawama nyingi sana Prosper mpaka apime damu yake inawazekana hakuambukizwa lakini hata kama ni hivyo nitawezaje kuwa na mwanaume shoga?” Alijiuliza Belinda bila kupata majibu ya maswali yake na machozi yaliendelea kumbubujika.
Muda mfupi baadaye huku Prosper na Belinda wakiendelea kulia mlango wa chumba ulifunguliwa na maaskari Magereza wawili wakaingia hadi ndani ya chumba walichokuwa wameketi Belinda na Prosper.
“Dada muda umekwisha tunakuomba sasa uondoke!” Alisema mmoja wa askari Magereza, mwanamke mwenye umri kati ya miaka ishirini na tano hadi thelathini aliyemwangalia Belinda kwa macho ya huruma.
“Ahsante dada naondoka sasa hivi!” Alijibu Belinda huku akinyanyuka na kumfunga mtoto wake mgongoni kwa kutumia khanga ndogo ya India.
“Belinda umenisamehe mke wangu?” Prosper aliuliza wakati maaskari wakimnyanyua kutoka sakafuni alipokaa.
Belinda hakulijibu swali hilo alianza kutembea kuelekea nje ya Gereza, kichwani kwake kulijaa mawazo mengi kupita kiasi! Mbele yake aliona giza, kimawazo alijiona tayari yupo kitandani hoi akiugua Ukimwi kwa sababu tu ya uzembe wa Prosper!
“Wanawake wengi sana wanaponzwa na wanaume zao katika suala hili la Ukimwi, nimejitahidi kadri ya uwezo kuwa mwaminifu kwa Prosper lakini ameniangusha!” Aliwaza Belinda akitembea kuelekea kituo cha basi.
Mwili wa Belinda ulikuwa bado ukitoa harufu kwa sababu ya tundu alilolipata wakati wa kujifungua, kabla hajafika kituo cha basi kumbukumbu juu ya matatizo yaliyompata katika mabasi aliyopanda zilimrejea kichwani mwake, hakutaka kuzomewa tena na hakutaka tatizo lake limsumbue wala kumkosesha raha mtu yeyote! Kwa sababu hiyo Belinda aliamua kutembea kwa miguu kuelekea mjini Tabora.
****************
Aliingia Tabora mjini saa nane mchana jua likiwa linawaka kweli kweli, alitafuta kivuli na kuketi huku akitafakari nini cha kufanya, alipofikiria kwenda hospitali ya Kitete moja kwa moja alishindwa kwa sababu zilikuwa zimebaki siku saba kutimiza mwezi kabla hajarudi, alijua manesi wasingempokea mpaka tarehe aliyopewa kurudi hospitali ifike!
Uamuzi uliomwijia akilini mwake wakati huo ni kwenda kijijini Tutuo kusubiri mpaka tarehe ifike ndiyo aende hospitali kurekebishwa tundu lake, alisubiri kwa hamu kubwa sana siku hiyo! Alitamani sana kupona na kurejea katika hali yake ya kawaida, alikuwa amechoshwa na kuzomewa pamoja na masimango aliyokuwa akiyapata.
“Na hili tundu ni kipimo tosha kama nina virusi vya Ukimwi au la! likipona nitakuwa sijaambukizwa lakini likikataa kupona nitakuwa navyo!” Belinda aliwaza kulingana na taarifa zilizokuwepo mitaani juu ya uponaji wa vidonda vya watu wenye Ukimwi.
Baada ya kuwaza kwa muda mrefu akiwa amekaa chini ya mti wa Mwembe karibu kabisa na shule ya sekondari ya Mihayo, Belinda alinyanyuka na kuamua kutembea hadi kituo cha basi ambako alipanda basi lililomfikisha hadi kijijini Tutuo, mtoto wake Alicia alilia kwa njaa lakini Belinda hakuwa na kitu cha kufanya ilikuwa ni mpaka afike nyumbani kwao na Prosper ndipo apike uji na kumpa.
Alisababisha usumbufu mkubwa sana ndani ya basi lakini hakuna mtu aliyegundua kuwa ni yeye aliyesababisha hali hiyo itokee, alipoteremka kituoni alitembea moja kwa moja hadi nyumbani kwao na Prosper, njiani watu wengi walionekana kumshangaa na hakuelewa sababu ilikuwa ni nini! Aliifananisha hali hiyo na mara ya mwisho alipokuja kijijini na kukuta mama yao Prosper amefariki.
“Sijui kimetokea nini tena leo?” Alijiuliza Belinda.
Mita chache kabla hajafika nyumbani alishangaa kuona ukuta mkubwa wa mabati ukiwa umekizunguka kiwanja chote cha nyumba ya akina Prosper! Belinda alishindwa kuelewa ni nini kilitokea ila alijua lazima kulikuwa na tatizo na aligundua ni kwanini watu walikuwa wakimshangaa.
“Nikusaidie dada?” Aliuliza mtu aliyemkuta mahali pale, aliyeonekana kama mlinzi.
“Nauliza waliokuwa wakiishi hapa wamehamia wapi?”
“Walikiuza kiwanja chao kwa mwarabu mzee Mohamed na sijui wamehamia wapi!”
Belinda aliishiwa nguvu miguuni na kujikuta amekaa chini bila kujua la kufanya, alishindwa kuelewa angekwenda nyumbani kwa nani na kuishi mpaka tarehe ya kwenda hospitali ifike! Kwa hali aliyokuwa nayo na harufu aliyoitoa alijua kusingekuwa na mtu ambaye si ndugu kijijini pale ambaye angevumilia kuishi naye ndani ya nyumba yake.
“Kwani vipi dada?”
“Kwani wewe hunifahamu mimi?”
“Ndiyo nilikuwa nakuona nyumbani kwa Mwarabu Mzee Mohamed lakini sikufahamu vizuri!”
“Nilikuwa naishi hapa na akina Nyamizi na Kasanda kabla sijaanza kazi nyumbani kwa Mwarabu mzee Mohamed, niliacha kazi nilipotakiwa kwenda kujifungua na baada ya hapo nilikwenda nyumbani kwetu Dar es Salaam na sasa nimerudi tena Tutuo nategemeo langu lilikuwa kufikia hapa hapa!” Alisema Belinda huku akimtoa mtoto wake aliyekuwa akilia mgongoni na kujaribu kumnyonyesha lakini maziwa hayakuwemo kifuani kwake.
“Ukweli ndio huo dada sasa sijui utafanya nini!”
“Kaka yangu nina matatizo makubwa nafikiri hata hapo ulipo unasikia harufu ninayotoa, ni kazi ngumu sana kwa mtu yeyote kuishi na mimi ndani! Ninatakiwa hospitali ya Kitete kutibiwa ugonjwa wangu siku saba kuanzia leo yaani tarehe nne, ninachokuomba kama binadamu mwenzangu mwenye huruma nisaidie niwe naishi hapa ndani mpaka siku hiyo ifike!”
“Dada lakini nyumba hii itabomolewa tarehe tatu! Ninaweza kukusaidia mpaka tarehe mbili baada ya hapo itabidi utafute utaratibu mwingine sababu mzee Mohamed anataka kuweka mashine zake za kusaga”
“Ahsante sana kaka na sijui nikushukuru vipi!”
“Usijali dada yangu matatizo ni ya wote, nyumbani kwangu ni kijiji jirani lakini nitakusaidia chakula mpaka hiyo tarehe mbili, kila nitakacholetewa na mke wangu tutakula pamoja!”
“Mungu akubariki sana kaka yangu!” Alisema Belinda huku akinyanyua mfuko wake wa rambo na kuingia ndani ya ngome ya mabati baada ya mlinzi kufungua mlango.
Nyumba ilikuwa haijabomolewa ila ndani yake hapakuwa na kitu chochote, si kitanda wala jamvi! Kasanda na Nyamizi walishachukua kila kitu, Belinda aliwashangaa sana wasichana hao kwa kitendo chao cha kuuza shamba na kumsahau kaka yao aliyekuwa gerezani.
Alichukua kitenge alichokuwa nacho ndani ya mfuko na kukitandika chini na yeye pamoja na mtoto wake wakalala na kujipumzisha, Alicia hakulala sababu ya njaa! Mlinzi ambaye baadaye Belinda alimtambua kwa jina la Juma alikuja ndani kuuliza ni nini kilikuwa kinasumbua.
“Ni njaa! Hajala kitu tangu jana na maziwa kifuani kwangu hayatoshi”
“Subiri nije!”
Mlinzi alitoka nje na aliporudi alikuwa na chupa ya maziwa na kumkabidhi Belinda.
“Mnyweshe hayo maziwa!”
“Ahsante sana kaka! Si ninahitaji kuyachemsha?”
“Ukiweza kufanya hivyo ni vizuri zaidi!”
Belinda aliipokea chupa na kuiweka pembeni alitamani kuyachemsha maziwa hayo lakini kwa sababu hakuwa na sufuria alishindwa na kulazimika kumnyesha Alicia maziwa ya baridi, alijua kulikuwa na magonjwa kama Kipindupindu, Kuhara, Kifua kikuu ambayo hutokana na kunywa maziwa yasiyochemshwa lakini yote hayo alimwachia Mungu.Baada ya kunywa maziwa hayo Alicia alitulia na kulala usingizi.
***************
Belinda alikaa ndani ya nyumba hiyo kwa msaada wa mlinzi Juma mpaka tarehe mbili nyumba ilipobomolewa! Hakuwa na mahali pa kuishi tena ilibidi ampe shukrani zake Juma na kupanda basi lililompeleka moja kwa moja hadi mjini Tabora, siku hiyo alishinda na kulala mtaani na siku iliyofuata saa kumi na mbili za asubuhi alikuwa ameshafika hospitali ya Kitete.
Saa mbili kamili aliingia katika chumba cha daktari aliyefurahi kumwona Belinda tena.
“Belinda mwanangu umerudi?”
“Ndiyo baba!”
“Pole sana najua umeteseka kiasi cha kutosha lakini mateso yako leo yanafikia mwisho!”
“Kweli baba?” Belinda alimuuliza daktari.
“Ndiyo mwanangu!” Alijibu daktari huku akiandika kitu fulani kwenye karatasi, alipomaliza alinyanyuka na kumwomba Belinda amfuate na waliongozana hadi katika chumba kilichoandikwa Laboratory! Wote wawili waliingia hadi ndani.
“Mzee Simba naomba umpime huyu binti damu!”
“Sawa daktari!”
“Daktari!” Belinda aliita.
“Naam Belinda!”
“Unataka kunipima damu?”
“Ndiyo! Ni lazima tujue!”
“Lakini mimi sitaki kufahamu!”
“Hutaki kufahamu nini?”
“Sitaki kufahamu kuwa nina virusi vya Ukimwi!”
“Siyo hivyo Belinda hatukupimi Ukimwi! Tunataka kufahamu una damu kiasi gani kwa sababu utafanyiwa operesheni leo”
“Kama ni hivyo sawa!” Aliitikia Belinda.
Daktari na mzee Simba wote waliangua kicheko kwa woga aliouonyesha Belinda.
“Kwanini mnaogopa sana kupimwa Ukimwi?” Daktari alimuuliza Belinda.
“Basi tu mimi sipendi!”
Usiku wa siku hiyo baada ya majibu kuwa mazuri Belinda alipelekwa chumba cha upasuaji na kurekebishwa kasoro yake akawa mwanamke kamili tena lakini wasiwasi wake uliendelea kuwa juu ya Ukimwi.
*****************
Mwezi mmoja baadaye:
Hali ya Belinda ilikuwa nzuri kabisa, hakuwa na harufu tena! Furaha ilijaa maishani mwake kasoro pekee iliyomchukulia sehemu ya furaha yake ni tatizo la Prosper! Lakini aliendelea kujipa moyo kuwa huenda Prosper hakuambukizwa virusi vya Ukimwi na Savimbi.
Uhakika pekee angeweza kuupata kwa kuongea na Prosper mwenyewe na kupata taarifa za majibu ya damu aliyomwomba apime! Baada ya kutoka hospitali aliamua kwenda moja kwa moja gerezani Isanga lengo lake likiwa kwenda kuyaona majibu ya damu ya Prosper.
*****************
Prosper alikuwa amekonda na alionekana mwenye mawazo mengi kupita kiasi na muda wote wakati wakiongea aliendelea kulia akimwomba Belinda msamaha kwa yote yaliyojitokeza.
“Prosper nieleze juu ya majibu yako ya damu!” Belinda aliuliza.
Walikuwa watu watatu tu ndani ya chumba Prosper alipoanza kueleza kila kitu kilichokuwa kikiendelea mwilini mwake.
“Nieleze kwanza juu ya majibu, hayo mambo ya homa na kuharisha yaache kwanza, nieleze kwanza juu ya majibu nataka kujua ukweli huo!” Belinda alizidi kumbana.
INAENDELEA
Post a Comment