HAYA MANENO HAYA YA KOCHA WA AZAM KUHUSIANA NA YANGA, TUSUBIRI...

Kocha
Mkuu wa Azam FC, Zeben Hernandez, raia wa Hispania, amesema endapo
kikosi chake hakitakumbwa na majeruhi wengi katika mzunguko wa pili wa
Ligi Kuu Bara, basi wana asilimia kubwa ya kuivua Yanga ubingwa wa ligi
hiyo.
Azam
ambayo katika mzunguko wa kwanza imemaliza ikiwa nafasi ya tatu na
pointi 25 ikipitwa pointi kumi na vinara Simba, imejinasibu kutokana na
usajili ilioufanya.
Timu
hiyo katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo, imewaongeza
Waghana watatu ambao ni Samuel Afful, Yahaya Mohammed na Enock Agyei,
huku pia ikimsajili mzawa, Joseph Mahundi.
Zeben
amesema: “Kuna mabadiliko makubwa nimeyaona katika kikosi changu,
lakini kikubwa ambacho nahofia ni uwepo wa majeruhi, kama sitakuwa na
majeruhi wengi, basi mzunguko wa pili natarajia kufanya vizuri zaidi na
kuchukua taji la ligi.
“Kuachwa
mbali na waliopo juu yangu si tatizo kwani natambua kwamba mzunguko wa
pili tutacheza mechi nyingi nyumbani, hivyo tutahakikisha tunakusanya
pointi tatu katika kila mchezo wetu.”
Post a Comment