ad

ad

EXCLUSIVE: NGASSA ASAFIRI KIMYAKIMYA KWENDA MBEYA, ANAWEZA KUMALIZANA NA MBEYA CITY



NGASSA AKIWA NDANI YA NDEGE KWENDA MBEYA, LEO.

Mrisho Ngassa leo amekweda pipa la Fastjet kwenda mjini Mbeya ambako inaelezwa atamalizana na klabu ya Mbeya City.

Ngassa ambaye hivi aliachana na Free State Star ya Afrika Kusini na kwenda kujiunga na Fanja ya Oman ambako aliondoka na kurejea Dar es Salaam kimyakimya.

Dirisha la usajili linafungwa kesho na taarifa za ndani kutoka Mbeya City zimeeleza, mazungumzo kati ya Ngassa na Mbeya City inayonolewa na Kocha Mmalawi, Kinnah Phiri yanakwenda vizuri na huenda leo au kesho wakamalizana.

Phiri ndiye alimsajili Ngassa Free State, lakini siku chache kocha huyo aliondoka katika klabu hiyo ya Afrika Kusini.


Kama atasaini kujiunga na Mbeya City itakuwa ni timu yake ya sita kuichezea katika Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya Toto African, Kagera Sugar, Yanga, Azam FC na Simba. 

No comments

Powered by Blogger.