NILIUA KUMLINDA MAMA YANGU - 16 (MWISHOOO)

Hapo, mambo yakaanza upya, kesi ikaanza
kusikilizwa mahakamani huku waandishi wa habari wakiifuatilia kwa umakini
kabisa. Madai ya Anita yaliwashangaza watu wengi, wengi wakashtuka kwani
hawakutegemea kama kuna siku kungekuwa na mwanamke angeibuka na kudai kwamba
mali zote alizokuwa nazo bwana Kambani ambazo kwa wakati huo zilikuwa chini ya
familia yake zilikuwa zake.
“Una uhakika nitashinda kesi hii?” aliuliza
Anita, alikuwa akimuuliza mumewe.
“Utashinda tu, wala usihofu.”
“Nashukuru kwa kunitia moyo!”
“Nashukuru kwa kunitia moyo!”
“Tupo pamoja.”
Kesi iliendelea kuunguruma, walichokifanya
mahakimu ni kupitia mafaili ya kipindi cha nyuma kabisa, jinsi mafaili
yalivyoonyesha, kulionekana kuwa na mianya mingi ya rushwa hivyo kuanza
kuisimamia tena kesi ile.
Mawakili kutoka pande zote mbili wakawasilisha
hati za umiliki wa nyumba na biashara mbalimbali, hati hizo zikafikishwa kwa
hakimu ambaye alitaka kuangalia pamoja na baraza lake la wazee.
Siku hiyo, kesi ikaahirishwa tena na kutakiwa
kusomwa tena baada ya wiki mbili. Kila siku ilikuwa ni kuahirisha kesi hiyo ila
baada ya miezi miwili, hukumu ikatolewa kwamba zile hati ambazo familia ya
bwana Kambani iliziwakilisha mahakamani, zilionekana kuwa na kasoro nyingi na
hazikuwa halali kabisa, ila hizi ambazo alizipeleka Anita, zilikuwa ni za
halali na zilionyesha kwamba yeye ndiye alikuwa mmiliki halali wa mali hizo.
“Mmiliki halali wa mali hizo ni bi Anita
Philip..” alisema hakimu, bi Anita akashindwa kuvumilia, hapohapo akaanza
kurukaruka kwa furaha.
Maisha yakaanza upya, mali hizo aliachiwa Anita
aziendeleze kama kawaida huku mume wake, bwana Philip akiendelea kuwa nchini
Madagaska. Hakutaka kurudi tena nchini Tanzania, kila kitu, hasa maisha yake
yangeendelea kuwa hukohuko nchini Madagaska.
*****
“Kweli duniani wawiliwawili...”
“Kwa nini?”
“Mmh! Nilikutana na msichana kama wewe!”
“Kwa nini?”
“Mmh! Nilikutana na msichana kama wewe!”
“Wapi?”
“Kwa bosi wangu! Yaani kama wewe...”
“Yupo wapi?”
“Sikumfuatilia sana mara baada ya bosi mwenye kuuawa, nilichanganyikiwa ati mpaka nikawa namuita kwa jina lako...” Joshua alimwambia Cynthia.
“Kwa bosi wangu! Yaani kama wewe...”
“Yupo wapi?”
“Sikumfuatilia sana mara baada ya bosi mwenye kuuawa, nilichanganyikiwa ati mpaka nikawa namuita kwa jina lako...” Joshua alimwambia Cynthia.
Muda wote waliokuwa Joshua alionekana kuwa na
furaha, kila alipomwangalia msichana wake, Cynthia, kumbukumbu za msichana
aliyekutana naye kwa bwana Kambani zilimjia kichwani mwake.
Alikuwa Cynthia huyohuyo lakini hakuweza
kuligundua hilo kwa kuwa mpenzi wake huyo aliamua kumficha. Kilichotokea baada
ya kukaa kwenye uhusiano kwa muda wa mwaka mzima, hapo ndipo wawili hao
walipopanga kuoana kama walivyopanga kipindi cha nyuma.
Hilo halikuwa tatizo, kila mmoja alikuwa tayari
na baada ya kutambulishana kwa wazazi, wawili hao wakafunga ndoa kwenye kanisa
la St. Patrick lililokuwa Masaki jijini Dar es Salaam.
Siri ya kuwa mpelelezi kutoka nchini Madagaska
iliendelea kubaki moyoni mwake, hakutaka kumwambia mumewe. Kwa upande wa pili, mpelelezi
Cosmas aliendelea kupeleleza lakini kila alipokuwa akifikia, hakuweza
kuendelea, hakupata ushahidi wowote ule, kila sehemu aliyokuta mwili wa marehemu,
hasa wale mabilionea, hakukuwa hata na alama za vidole.
Alichanganyikiwa, baada ya miaka miwili ndipo
akapokea barua pepe iliyomwambia kwamba alitakiwa kuachana na kila kitu kwani
kuuawa kwa watu hao kulikuwa na mpango kabambe nyuma, hasa kuua mizizi ya
biashara ya madawa ya kulevya.
Hakujua barua pepe hiyo ilitoka wapi ila
alipoifuatilia sana, aliona ikiwa imetoka katika shirika kubwa la kijasusi
nchini Marekani, CIA hivyo akaamua kufunga mafaili yake na kusafiri tena kwenda
nchini Marekani kula bata kama kawaida yake.
Huku nyuma, kila kitu kilichotokea
kilisahaulika, mapenzi motomoto kati ya Philip na Anita yalirudi tena, binti
yao aliwafanya kuwa na furaha siku zote, kazi kubwa aliyokuwa amepewa,
aliifanya kwa kiasi kikubwa na hakutaka kujishughulisha na bwana Marimba ambaye
alikuwa nyumba ya nondo.
Yote hayo, mauaji aliyofanya, alifanya kwa kuwa
alimlinda mama yake ili hapo baadaye asije kuuawa na watu hao walioonekana kuwa
na roho mbaya.
Cynthia na mumewe waliishi nchini Tanzania kwa
miaka miwili kabla ya kuamua kuhama na kuhamia nchini Madagaska ambapo wanaishi
huko mpaka leo hii.
MWISHOOO
Post a Comment