Singidani (A Story From My Heart) - 12

ILIPOISHIA...
"...lakini inanipasa nikubali
kuwa nimeshatekwa na ninampenda. Nitahakikisha nampata Chris, lazima, "
aliwaza Laura.
SASA ENDELEA...
SAA 10:00 alasiri, Basi la Beffe
lilifunga breki katika kituo cha Mkalama - Shuleni. Dk. Chris alishuka na
mizigo yake. Akakodisha baiskeli iliyomfikisha nyumbani kwao.
Alipokelewa kwa shangwe na bibi yake
aliyekuwa akisuka jamvi kwa kutumia ukindu kiambazani mwa nyumba yao
mpya. Walikuwa na eneo kubwa lililozungushwa kwa uzio wa michongoma. Maboma
mawili makubwa ya mifugo yalikuwa pembeni mwa nyumba zao.
Walifuga ng’ombe, mbuzi na kondoo.
Nyumba yao mpya iliyojengwa kwa matofali ya kuchoma na kuezekwa kwa bati
haikuwafanya wabomoe nyumba yao ya asili ambayo ilijengwa kwa fito na udongo na
kuezekwa kwa tembe.
“Aaaah! Mume wangu huyoo...” bibi
alitamka kwa sauti kuu, akijaribu kumkimbilia mjukuu wake.
Alikuwa ajuza hasa, akiwa na umri wa miaka themanini na tatu, alimudu kufanya shughuli zake ndogondogo za kila siku. Aliishi na wanaye wawili; Shamakala ambaye alikuwa na mke na watoto wawili na Maria aliyekuwa na mtoto mmoja.
Alikuwa ajuza hasa, akiwa na umri wa miaka themanini na tatu, alimudu kufanya shughuli zake ndogondogo za kila siku. Aliishi na wanaye wawili; Shamakala ambaye alikuwa na mke na watoto wawili na Maria aliyekuwa na mtoto mmoja.
Ilikuwa famili yenye upendo mkubwa.
Dk. Chris aliongeza mwendo na walipokutana na bibi yake alimpokea na kumlaza
kifuani mwake.
“Ooh! Daktari wangu huyo... karibu sana baba,” bibi alisema, akishindwa kuficha furaha yake.
“Ahsante bibi, shikamoo.”
“Ooh! Daktari wangu huyo... karibu sana baba,” bibi alisema, akishindwa kuficha furaha yake.
“Ahsante bibi, shikamoo.”
“Marhaba mume wangu, habari za
nyumbani?”
“Nzuri kabisa.”
Pamoja na kuzaliwa na kukulia kijijini Mkalama, bibi huyo alimudu vizuri sana kuzungumza Kiswahili japo kuna wakati huchanganya na lugha yao ya Kinyiramba.
“Nzuri kabisa.”
Pamoja na kuzaliwa na kukulia kijijini Mkalama, bibi huyo alimudu vizuri sana kuzungumza Kiswahili japo kuna wakati huchanganya na lugha yao ya Kinyiramba.
Mara moja bibi aliingia ndani,
akatoka na kipeyu kilichojaa togwa kisha akamkabidhi Dk. Chris apooze koo na
kinywaji hicho cha asili. Salamu zikaendelea.
***
Sura ya mwanamke mrembo ilimchanganya Dk. Chris, alimwangalia umbo lake. Akatazama hipsi zilizochomoza vyema pembeni ya mapaja yake, akazidi kutibuka! Matiti madogo yaliyosimama yenyewe kifuani kama embe bolibo, ilikuwa kishawishi kingine kwa Chris.
***
Sura ya mwanamke mrembo ilimchanganya Dk. Chris, alimwangalia umbo lake. Akatazama hipsi zilizochomoza vyema pembeni ya mapaja yake, akazidi kutibuka! Matiti madogo yaliyosimama yenyewe kifuani kama embe bolibo, ilikuwa kishawishi kingine kwa Chris.
Nyongo ya huba ikapasuka. Alikiri
kweli mwanamke yule alikuwa mrembo. Chris aliumia moyoni alipogundua kuwa,
hawezi kumpata mwanamke yule tena. Ni Laura alikuwa akimjia mawazoni kwa kasi
sana.
Akiwa amekaa chini ya mti, Chris alidongosha machozi kwa kumbukumbu za mwanamke huyo. Alitamani sana kubadilisha ukweli, awe hajaolewa lakini haikuwezekana.
“Vipi wewe?” Shamakala, baba yake mdogo alitamka akimgusa begani.
Akiwa amekaa chini ya mti, Chris alidongosha machozi kwa kumbukumbu za mwanamke huyo. Alitamani sana kubadilisha ukweli, awe hajaolewa lakini haikuwezekana.
“Vipi wewe?” Shamakala, baba yake mdogo alitamka akimgusa begani.
Chris alishtuka na kugeuza
shingo kumwangalia aliyemgusa. Hapo akakutana na sura ya baba yake mdogo.
Shamakala akashangazwa na machozi ya Chris.
“Vipi, mbona unalia?” Shakamala akamwuliza.
“Vipi, mbona unalia?” Shakamala akamwuliza.
Shamakala na Chris walipishana
kidogo sana kiumri. Alikuwa kitindamimba katika uzao wa babu na bibi yake.
Sababu hiyo iliwafanya wawe marafiki na kuelezana siri zao zote. Chris hakuona
sababu ya kumficha. Alimweleza kila kitu kuhusu kisa cha Laura.
“Tulia Chris, imekuwa vizuri umegundua mapema.”
“Lakini kuna tatizo lingine kubwa zaidi.”
“Tulia Chris, imekuwa vizuri umegundua mapema.”
“Lakini kuna tatizo lingine kubwa zaidi.”
“Lipi?”
“Mke. Baba amesema natakiwa kurudi Dar na jibu linaloeleweka. Ameniagiza nije huku kutafuta mke, amesisitiza kwamba lazima nioe huku kwa sababu mke bora anapatikana huku kijijini.”
“Uamuzi wako ni nini juu ya hili?” akauliza Shamakala.
“Mke. Baba amesema natakiwa kurudi Dar na jibu linaloeleweka. Ameniagiza nije huku kutafuta mke, amesisitiza kwamba lazima nioe huku kwa sababu mke bora anapatikana huku kijijini.”
“Uamuzi wako ni nini juu ya hili?” akauliza Shamakala.
“Sitaki kuongozwa katika suala hili.
Natakiwa kutafuta na kuamua mwenyewe nimuoe nani na wapi. Hata hivyo
nilipokutana na huyo Laura, nikaona ndiye mke wangu, imekuwa tofauti.
“Si neno sana, maana siwezi kubadili ukweli ila baba sitaki kuoa huku kwa sasa, lazima nitulie kwa muda, nirudi mjini nitafute mwanamke mwingine,” akasema Chris.
“Si neno sana, maana siwezi kubadili ukweli ila baba sitaki kuoa huku kwa sasa, lazima nitulie kwa muda, nirudi mjini nitafute mwanamke mwingine,” akasema Chris.
“Wazo zuri, lakini mzee atakuelewa?
Maana Joseph namjua vizuri sana misimamo yake.”
“Hapo ndipo ninapohitaji msaada wako baba mdogo. Itabidi tufanye mchezo. Mimi nitamwambia baba nimeshapata mke, wewe ndiye uliyenitafutia. Muda huo nitautumia kuanza kutafuta mwanamke mwingine. Unaonaje?”
“Hapo ndipo ninapohitaji msaada wako baba mdogo. Itabidi tufanye mchezo. Mimi nitamwambia baba nimeshapata mke, wewe ndiye uliyenitafutia. Muda huo nitautumia kuanza kutafuta mwanamke mwingine. Unaonaje?”
“Sawa kabisa, nipo upande wako. Kaka
naye pamoja na kusoma kote huko bado ana mawazo ya kizamani sana. Nitakusaidia,
nipo kwa ajili yako!”
“Ahsante sana baba mdogo.”
“Ahsante sana baba mdogo.”
Kilichompeleka kijijini ni kama
alikuwa ameshakamilisha. Kilichokuwa mbele yake kwa wakati huo ilikuwa ni
kupanga safari ya kurudi Dar. Alitakiwa kurudi haraka kwa sababu alikuwa
ameshasaini mikataba miwili ya filamu na alitakiwa kurekodi.
“Inabidi nirudi Dar keshokutwa.”
“sawa ila unaniachaje?”
“Usijali.”
***
“Jambo moja muhimu ninalohitaji kujua kutoka kwako ni kama umefanikiwa nilichokuagiza kijijini au lah!” mzee Joseph Shila alimwambia mwanaye Chris, alipomkuta nyumbani usiku huo baada ya kurudi kutoka kazini.
“sawa ila unaniachaje?”
“Usijali.”
***
“Jambo moja muhimu ninalohitaji kujua kutoka kwako ni kama umefanikiwa nilichokuagiza kijijini au lah!” mzee Joseph Shila alimwambia mwanaye Chris, alipomkuta nyumbani usiku huo baada ya kurudi kutoka kazini.
“Nimefanikiwa baba,” akajibu Chris,
akitengeneza tabasamu la uongo usoni mwake.
“Vizuri sana. Moyo wangu sasa una amani. Bila shaka sasa tunatakiwa kufikiria kuhusu mipango ya ndoa tu!” mzee Shila akauliza tena.
Chris hakujibu!
“Vizuri sana. Moyo wangu sasa una amani. Bila shaka sasa tunatakiwa kufikiria kuhusu mipango ya ndoa tu!” mzee Shila akauliza tena.
Chris hakujibu!
Post a Comment