Video: Dar yasimama kwa muda Lowassa akielekea NEC kuchukua fomu ya urais

Hatimaye mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Waziri Mkuu mstaafu Edward Ngoyai Lowassa leo amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Awali, mgombea huyo alianzia Makao Makuu ya Chama cha Wananchi (CUF), Buguruni, Dar es Salaam kisha kuelekea Tume yaTaifa ya Uchaguzi kwa kupitia barabara ya Uhuru, Bibibti Mohamed hadi Makao Makuu ya Tume hiyo.
Baada ya hapo, msafara wake ulipititia Barabara ya Ocean Road kisha Umoja wa Mataifa, Ally Hassan Mwinyi hadi Makao Makuu ya CHADEMA yaliyopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Katika msafara huo, umati mkubwa wa wapenzi na wakereketwa wa mgombea huyo walijitokeza kumsindikiza .
Post a Comment