MGEJA, GUNINITA WAKITOSA CHAMA CHA MAPINDUZI, WAJIUNGA CHADEMA
Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislam, Sheikh, Rajab Katimba (kushoto) akiwa na aliyekuwa Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Shinyanga ambaye ameachana na chama hicho, Khamis Mgeja,
na aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita,
ambaye naye amehamia Chadema. 
Mgeja akionyesha ishara ya Chadema baada ya kutoa tamko la kujiuzulu. 
Wanahabari wakichukua matukio katika hafla hiyo. 
Baadhi ya makada wa CCM alioungana nao kujiunga na Chadema.
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, na aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Dar es Salaam, John Guninita, wametangaza kuachana na chama hicho na
kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Mwenyekiti huyo alitoa kauli hiyo leo
katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) alipokuwa akiongea na
wanahabari jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa umamuzi wa kuachana
na CCM ulitokana na kutoridhika na uteuzi wa mgombea kupitia chama
chake, John Pombe Magufuli, pamoja na mwenendo mzima wa chama hicho
kwa viongozi kufanya wanachokitaka wao.
Amesema kuwa uteuzi wa mgombea urais
uliofanyika Dodoma chini ya mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Mrisho
Kikwete, haukuzingatia taratibu na maadili ya chama ambapo alisema
ulijaa upendeleo na chuki dhidi ya aliyekuwa akimtegemea, yaani waziri
mkuu aliyejiuzulu, Edward Ngoyayi Lowassa.
Aidha Mgeja alisema amekuwa ndani ya CCM
zaidi ya miaka 20 na haoni haja ya kuendelea nacho kwani hakijaonesha
mapenzi mema kwa mgombea aliyekuwa akikubalika kwa wananchi.
Katika maelezo yake Mgeja alitumia kauli
ya hayati Julius Nyerere, aliyotoa mwaka 1995 kwamba: “Watanzania
wanahitaji mabadiliko na wasipoyapata ndani ya (CCM) watayatafuta nje ya
CCM.”
NA DENIS MTIMA/GPL

Post a Comment