ad

ad

JAMANI DADA MARTHA LOOO!-26

 


www.facebook.com/2jiachie
ILIPOISHIA :“Mimi na Martha wajina wangu, nani unampenda zaidi?”

“Martha wewe.”
“Basi mtumie meseji kwamba umeamua kuwa na mimi, hivyo jioni utakwenda kuchukua nguo zako tu.”
“Mh! Atakuibulia ugomvi wewe.”
“Mimi nipo tayari.”
Wakati wakizungumza hayo, mara Martha akaingia...
SASA TAMBAA NAYO MWENYEWE...
“Anhaaa! Mungu kweli mkubwa. Leo nimeamini. Kumbe hii ndiyo biashara yenu siyo?” aliuliza Martha kwa sauti yenye kujiamini...
“Hebu kaa kwanza hapo,” alisema Roi huku akitetemeka. Mama Anna alitetemeka lakini si sana.
Martha alivuta kiti, akakaa na kusema...
“Unasemaje wewe mwanaume mwenye majina mengi. Maana nimesikia una majina kama matatu hivi wewe peke yako. Kila mtu mtaani anakufahamu kwa jina lake.”
Roi alishtuka kusikia hivyo. Kwani ni kweli mtaani ana majina mengi...
“Mh!” aliguna Roi huku akimtumbulia macho ya aibu Martha. Lakini hakujibu hoja ya kuwa na majina mengi.
“Sikia nikwambie baby wangu Martha. Huyu si mpenzi wangu, ni sista‘angu ila sijawahi kukwambia,” alianza kusema Roi...
“Mimi dada yako mimi?” mama Anna alikuja juu kumuuliza Roi...
“Aaa! Jamani dada Martha...looo! yaani unanikataa kaka yako hivihivi naona jamani?”
“We wajina...sikia, mimi si dada yake wala yeye si kaka yangu. Mipango yetu ni kufunga ndoa. Huyu si wa kumtegemea wewe kwani mapenzi yake ameyahamishia kwangu...we ulie tu,” alisema mama Anna kwa macho yaliyokosa aibu.
Martha alidondoka palepale, akapoteza fahamu, hali ikawa tete. Roi huku akiogopa, alimtupia lawama mama Anna...
“Unaona sasa? Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumwambia wewe. Si ningemwambia mimi mwenyewe...
“Na haikuwa lazima kumwambia sasa hivi, hata nyumbani ningemwambia...”
“Baby, mimi tatizo langu sipendi kukatishakatisha. Niko moja kwa moja sana. Nisamehe kwa hilo. Ndiyo maana nilikuuliza awali unampenda nani. Mtu akifiwa hakuna haja ya kufichaficha, ni kumwambia tu ili kama kulia alie,” alisema mama Anna.
Roi na mama Anna walimzoa Martha na kumkimbiza hospitali ambako alilazwa. Mama Anna aliwapa taarifa wale wapangaji wengine kuhusu kuugua ghafla kwa mwenzao huyo.
***
Ilikuwa saa kumi na mbili jioni, Martha alikuwa kwake baada ya kutoka hospitali. Wapangaji wenzake waliingia kumpa pole kasoro mama Anna tu ambaye muda huo alikuwa nyumbani kwa Roi...
“Pole mwaya! Yaani tuliposikia umelazwa tukashangaa sana. Da! Sasa tatizo lilikuwa wapi Martha?” mpangaji mmoja alimuuliza...
“Jamani ni hadithi ndefu sana. lakini kifupi nilikuwa sijui kama jamaa yangu anatoka na mama Anna. Nilihisi wakati f’lani nikafuatilia, jana usiku nikanasa meseji zao za mahaba.
“Leo asubuhi nikasema niende kazini kwake kufika namkuta mama Anna ndani. Yeye jamaa yangu akasema mama ni dada yake, japo nilijua ni uongo, lakini mama Anna mwenyewe akanipasulia kwamba wao si ndugu bali ni wachumba na wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni,” alitiririka Martha...
***
Kule nyumbani kwa Roi, mama Anna alimtaka Roi amruhusu awaite wale wapangaji wenzake wawili ili awatambulishe rasmi kwake...
“Aaaa...eeee...oke, waite basi,” alisema Roi ambapo awali alianza kwa kutaka kukataa.
“Mbona baby kama unasita? Au mipango yetu imekufa nini?” aliuliza mama Anna...
“Aaa! Noo...iko palepale. Basi waite.”
Mama Anna alimpigia simu mmoja wa wapangaji wenzake, akampa maelekezo ya namna ya kufika hapo.
Wakati wanaondoka, wakamuaga Martha...
“Basi twendeni wote na mimi nataka kupeleka nguo za Roi.”
Wale ilibidi wamjulishe mama Anna kwanza ambapo naye alikubali bila kumuuliza Roi...
“Aje tu, hakikisheni amebeba hizo nguo za Roi ili asije kupata kisingizio kingine baadaye,” alisema mama Anna.
Wakati anazungumza hivyo, Roi ndiyo akasikia na kuhoji ni nini, mama Anna akamwambia, Roi akatingisha kichwa tu kukubaliana naye.
Kutoka moyoni mwake, Martha alishakubaliana na hali iliyotokea, akajilaumu sana kwa uamuzi wake wa kung’ang’ania yeye na Roi wasiwe kaka na dada na badala yake wawe wapenzi...
“Ningeusikiliza moyo siku zile haya maumivu yalikuwa yanakwepeka,” alisema moyoni wakiwa wanakaribia nyumbani kwa Roi yeye akiwa kiongozi maana alishafika.
Waliingia ndani watatu, wale wapangaji wawili na Martha.
Mama Anna aliwakaribisha kwa mbwembwe akijifanya mama mwenye nyumba huku Roi akionekana kukosa amani...
Karibuni jamani...karibuni sana,” alikaribisha mama Anna kwa sauti ya ‘mimi ndiye mmiliki halali wa mwanaume huyu’, yaani Roi sasa.
“Tunashukuru sana,” waliitikia wale wapangaji wawili kasoro Martha ambaye yeye alifikia kuweka begi chini kisha akamwambia Roi...
“Ungeangalia kama nguo zako zote zipo maana nimehakikisha siachi nguo yako hata moja.”
“Naamini zote zipo bila hata ya kuhakikisha,” alisema Roi kwa sauti iliyojaa dharau, mkono mmoja ulipita kiunoni kwa mama Anna huku mkono mwingine ukishughulika na rimoti ya televisheni.
Bila kukaa, Martha akageuza kutoka lakini kabla hajafika mlangoni, ikasikika hodi...
“Hodi,” hodi hiyo ilipigwa huku aliyepiga akisukuma mlango kuingia sebuleni.
Roi alishtuka sana, akatumbua macho huku akisimama na kusema...
“Mama Neema...mbona umekuja bila taarifa mke wangu? Umeona sasa umenikuta katika mazingira tata. Lakini kifupi hapa hakuna mwanamke wangu mama Neema.”
Je, nini kilitokea? Ili kuyajua yote hayo,Tukutane siku ya Jumamosi wiki hii hapa hapa
Baada ya kusoma simulizi hii tunaomba Ushare ili iwafikie wanaofuatilia simulizi hii tunaomba sana sana
Powered by Blogger.