MAMIA WALIVYOMZIKA GWIJI WA TAARAB KHAMIS MZINGA
MAMIA ya watu wamejitokeza kumzika Khamis
Mzinga, mwimbaji gwiji wa taarab kupitia kundi kongwe la Egptian Musical Club,
aliyefariki usiku wa kuamkia leo.
Khamis Mzinga amezikwa
katika makaburi ya Tambaza jijini Dar es Salaam saa 11 alasiri ambapo licha ya
kuzikwa na watu wengi, lakini wasanii wa taarab walikuwa wa kuhesabika.
Marehemu Khamis Mzinga alijijengea himaya kubwa kwenye muziki wa taarab akiwa
mwimbaji bingwa, mtunzi, mtaalam wa kupanga muziki, fundi wa kupiga vyombo
kadha wa kadha vya taarab na mwalimu aliyewafundisha muziki wasanii wengi wa
taarab.
Lakini marehemu pia
kifamilia alikuwa na mzunguko mkubwa uliokaa kitaarab, kama vile; baba yake
mdogo, Aboubakar Mzinga aliyekuwa mwanamuziki gwiji wa taraab.
Pia baba yake mzazi, mama
yake mzazi wote walikuwa waimbaji wa taarab, huku bintiye Asia Mzinga, mzazi
mwenzake, Mwanamtama Amir, shemeji yake Hassan Soud wakiwa ni wanamuziki wa
taarab.
Kwa sifa hizo, utaona
kuwa Khamis Mzinga alipaswa kuzikwa na wasanii wengi wa taarab wa rika zote,
lakini haya siku zote ndiyo yamekuwa maisha ya wasanii wa taarab – kuzikana ni
kama dhambi kwao.
Khamis Mzinga amezikwa
pembeni ya kaburi la baba yake mzazi pamoja na baba yake mdogo.
Pata picha 25 za mazishi
ya Khamis Mzinga yalivyofanyika kwenye makaburi ya Tambaza jirani na hospitali
ya Muhimbili.
Jeneza lililobeba mwili wa Khamis Mzinga likiwasili makaburi ya Tambaza
Kaburi la Khamis Mzinga
Baadhi ya wahudhuriaji wakiwa makaburini wa tano kutoka kulia mwenye kanzu ni mkurugenzi wa Melody Ashraf Mohamed
Jeneza lineza limewasili kwenye kaburi
Mwili unaingizwa kaburini
Wahudhuriaji wakiwa kwenye utulivu wa hali ya juu
Mwili tayari umewekwa kaburini
Mazishi yanaendelea
Meneja wa Mashauzi Classic Ismail Sumaragar akishiriki mazishi
Mpiga kinanda wa wa Mashauzi Classic (mwenye fulana ya njano) akimwaga mchanga kaburini
Kushoto ni Aboubakar mtoto wa marehemu Khamis Mzinga akizungumza na mtangazaji wa Magig FM Mwinyiami Maftah
Wasaa wa kupata kisomo
Wasaa wa dua, huyu ni mpiga solo wa zamani wa Dar Modern Mridu Ally
Mdau wa taarab Hamad Mmanga
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria mazishi ya Khamis Mzinga
Kutoka kushoto ni Feruz mmoja wa maboss wa Ogopa Kopa, mwimbaji mkongwe wa taarab Mustapha Ramadhan na mtangazaji Mwinyiami Maftah "Stazo"
Kushoto ni Sheikh Mohamed Idd akiwa makaburini
Afisa habari wa Simba SC Hajj Manara
Mpiga kinanda Hassan Soud mmoja wa wanafunzi wa Khamis Mzinga
Mheshimiwa Zungu mbunge wa Ilala naye alikuwepo
Umati mkubwa ulijitokeza kumzika Khams Mzinga
Kaburi la Khamis Mzinga (ambalo halijajengewa), mbele yake ni makaburi ya baba yake mdogo na baba yake mzazi
Kushoto ni Aboubakar mtoto wa Khamis Mzinga
Ndugu na jamaa wakifanya kisomo baada ya mazishi kukamilika
CHANZO: SALUTI 5.COM

























Post a Comment