ad

ad

JAMANI DADA MARTHA LOOO!-7

 

ILIPOISHIA
“Daa! Sista nakushukuru sana mama. Hakuna jina nalipenda kama la Martha kuliko Liz, nashukuru kwa kuniruhusu...”
“Oke usijali baby bro...uko wapi sweetheart kaka?”
“Nipo nyumbani darling sista...”
“Oke! Mtoto mzuri kumbe, wewe ndiye kaka wa kweli.”
“Hata wewe ni dada wa kweli. Good sista...hujalala?”
“Ndiyo nataka kulala sasa. Nimechokaaaa!”
“Umechokeshwa na nini sista jamani?”
SASA ENDELEA...
“Kwani hujui bro?”
“Sijui chochote.”
“Aaah! Si kule tulikokuwa,” alisema Martha lakini akilini mwa Roi alijua kilichomchokesha sista wake ni nini!
“Kule gesti?” aliuliza Roi...
“Ndiyo kulekule bro...daa!”
“Daa! Ila sista uko vizuri unajua?”
“Teh! Teh! Mh! Wewe je kaka? Mbona uko vizuri zaidi...”
“Mh! Kweli...?”
“Kweli bro...”
“Uliipenda chenga ipi pale uwanjani?”
“Mmh! Kaka bwana...chenga zote zilikuwa nzuri sana kaka, wewe ni kiboko.”
“Hamna! Lazima kuna chenga moja uliipenda sana...iseme tu sista jamani...”
“Ha! Ha! Ha! Niliipenda ile ulipokaribia golini ukawa unapiga chenga za zigzaga. Halafu hata ile ya mimi kuchunga ng’ombe ilikuwa nzuri...”
“Nyingine, lazima kuna nyingine...”
“Nyingine ni ile uliponiambia una hamu ya kula mboga ya matembele, si ikabidi nikachume.”
“Mh! Sista...”
“Nini tena braza..?”
“Mwenzio hoi hapa...”
“Mimi je? We acha tu! Hivi hapa nataka kwenda kuoga.”
“Umechafuka na vumbi?”
“Kumbe je?”
“Kwa hiyo? Nije nini?”
“Ha! Ha! Mbali...halafu ukaka si unaendelea kama kawa au?”
“Laa! Aisee...huu ukaka na udada halafu tunapeana njaa si mzuri...nataka kuruka  nije...”
“Njoo...”
“Kweli?”
“Kweli njoo.”
“Nikija?”
“Si utakula chakula kama mgeni.”
“Chakula gani?”
“Utakacho...kuna ndizi za kuiva na maandazi ya donati.”
 “Mh! Unanitamanisha sista...mimi nitakula donati...”
“Haya mimi nitakula ndizi za kuiva,” alisema Martha.
“Lakini sista...”
“Nini tena jamani kaka..?”
“Kwani umelala sista?”
“Nipo kitandani bro...”
“Umelalaje hapo kitandani?”
“Nahesabu paa...wewe bro?”
“Mimi nasoma kitabu.”
“Kumbe tupo sawa basi!”
“Basi acha kuhesabu paa.”
“Na wewe utaacha kusoma kitabu?”
“Nimeshakiweka pembeni.”
“Oke, mimi nimeshaacha kuhesabu paa.”
“Miguu ikoje?”
“Mashariki na Magharibi mwa nchi.”
“Basi mimi niko kanda ya kati nakuja kwako.”
“Njoo broo.”
“Ndiyo nakuja sasa...”
“Njoo tu. Na mimi nimeanza kukuona unavyokuja.”
“Kwa hiyo utanipokea..?”
“Ukifika nakupokea bro tena kwa mikono miwili kaka...njoo!”
“Nakaribia, nimeanza kukuona umesimama mlangoni unanisubiri...”
“Karibu broo...njoo...”
Roi alitumia meseji nyingine lakini hakujibiwa, akatuma nyingine, hakujibiwa, akapiga, Martha hakupokea...
“Jamani dada...nini tena?”
Baada ya dakika kumi na tano, meseji ikaingia, Roi akaisoma kwa haraka sana...
“Brooooo...”
“Sistaaa...”
“Nipo vibaya, please kama unaweza njoo kweli sasa hivi...chukua usafiri wowote ule nitakuelekeza kwangu please bro njoo tucheze...”
“Sista Martha...”
“Yes brooo...ooo!”
“Ukaka na udada je? Ufe?”
“Aaaah! Potelea mbali bwana...kwani lazima wakati mi nateseka?”
“Hapana dada...undugu ni bora kuliko mapenzi...tutagombana kila siku tukiwa wapenzi dada...”
“Hapana kaka...basi leo tu...”
“Baada ya leo?”
“Tusirudie tena bro...”
“Haya nakuja...kaa tayari...”
“Njoo kaka mpaka Kimara Mwisho, kuna barabara inaingia kulia, fuata hiyohiyo mpaka sehemu kuna pub, kuna muziki nje...nipigie...”
“Kwani saa hizi unafanyaje dada?”
“Natandika kitanda kaka, si unakuja kweli?”
“Nakuja dada...”
“Njoo kaka...”

***
Baada ya dakika kumi, Roi alimpigia simu Martha akiwa kwenye pub aliyomwelekeza...
“Nakuja kaka...”
“Poa dada.”
Usiku huo, Martha alivaa gauni la kulalia kwa hiyo lilimwonesha umbo lake kwa usahihi wote kiasi cha kumfanya Roi kuanza kufikiria upya kuhusu kuendelea na ukaka na udada baada ya tukio la muda huo...
Martha alikuwa akiishi na wapangaji wengine, wanawake wenzake ambapo kwa usiku huo walikuwa wamekaa nje jirani na dirisha la chumba cha Martha wakiongea...
“Karibu sana kaka...! Jamani huyu kaka ‘angu, anaitwa Roi...”
ITENDELEA HAPA KESHO

No comments

Powered by Blogger.