ad

ad

SEMINA YA FURSA YAWAONYESHA NJIA WAKAZI WA DODOMA


 
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group, Ruge Mutahabaakiongea na baaddhi ya wakazi wa Dodoma mjini waliyohudhuria kwenye Semina ya Kamata Fursa ndani ya Ukumbi wa Royal Villege mapema leo,ambapo aliweze kuongea nao na kuwapatia mbinu mbalimbali za kujikwamua kupitia lasilimali zilizopo kwenye mazo yapatikanayo ndani ya mkoa huo.
 
Msemaji kutoka G5 One, Pius Mikongoti akiwalezea wakazi wa Dodoma namna ya kunufaika kupitia huduma zitolewazo na GS One hasa katika kutumia Barcode.
 
Msanii wa kughani Mashairi, Mrisho Mpoto naye akijaribu kuwapa historia yake ya mafanikio na namna alivyoweza kutumia fursa hadi kufikia hapo alipo kwa sasa.
 
Afisa Utekelezaji na mipango wa NSSF, Ally Mkulemba akitoa semina kwa wakazi wa Dodoma huku akiwapa mbinu za kutumia fursa katika kusongesha mafanikio kupitia mikopo mbalimbali itolewayo na Shirika hilo mapema leo ndani ya Ukumbi wa Royal Villege.
 
Mrisho Mpoto akimkabidhi kifaa cha kupimia magari mmoja wakazi wa Dodoma Beatrice Chilewa (kulia), muda mfupi baada ya kujishindia moja ya swali lililoulizwa na msemaji wa GS One Pius Mikongoti, ambalo lilikuwa likimtaka ataje nchi tatu za Kusini mwa Jangwa la Sahara zinazotoa Barcode na namba za utambulisho wa nchi hizo, wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa kampuni ya Josekazi Auto Garage ambaye ndiye mimiliki wa kifaa hicho cha kupimia magari.
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Josekazi Auto Garage, Joseph Mgaya akiwaeleza wakazi wa Dodoma namna alivyotumia fursa na kumnya aweze kumiliki kampuni hiyo inayojishugurisha na huduma za kutengeneza A/C za magari na Ndege na nanamna alivyo wekeza hadi leo anakifaa kinachoweza kupima magari yote na kujua matizo yote kwa halaka.
 
Baadhi ya wakazi wa Dodoma waliyojitokeza kusikiliza mafunzo mbalimbali kwenye Semina ya Kamata Fursa iliyokuwa ikifanyika ndani ya Ukumbi wa Royol Villege.
 
Msanii wa Bongo Fleva Mwasiti Almasi akijaribu kuwaonyesha wakazi wa Dodoma namna alivyotumia Fursa iliyopo kwenye muziki na kufanikiwa kuwekeza baadhi ya vitu kupitia mafao mbalimbali yatolewayo na Shirika la NSSF.
 
Sehemu ya watu waliyojitokeza kwenye Semina ya Kamata Fursa iliyokuwa ikifanyika ndani ya Ukumbi wa Royal Village.
 
Mmoja wa wanasemina hao akiuliza swali lililotokana na mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na wasemaji mbalimbali wa Semina ya Kamata Fursa muda mfupi kabla ya kumalizika kwa semina hiyo.
 
Mtangazaji wa Kipindi cha Leo tena, Gea Habib akizungumza jambo kwenye semina ya Kamata Fursa.
 
Meza kuu ya watoa mada ya Kamata Fursa wakijadiliana baadhi ya mambo yaliyokuwa yakiendelea mahali hapo.
Habari/Picha: Musa Mateja/ GPL/Dodoma

No comments

Powered by Blogger.