DAVINA AMWANGUKIA MUMEWE
Sorry! Staa wa sinema za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’
anadaiwa kumwangukia mumewe, Abdallah Shakoor ili kurejesha uhai wa ndoa
yao ‘iliyokwaruzwa na makucha ya shetani’ ikiwa ni njia ya kurudisha
heshima na hadhi yake kwenye familia na jamii kwa jumla.
“Davina amekubali yaishe, unajua anampenda sana mumewe, ‘so’ anahaha kwa ndugu ili wamuombee msamaha,” alisema ‘kikulacho’ huyo wa Davina.
Staa wa sinema za Kibongo Halima Yahya ‘Davina’.
Habari kutoka kwa chanzo makini kilieleza kwamba, mara kadhaa Davina
amekuwa akiomba msaada kwa ndugu, jamaa na marafiki wamsaidie kumuombea
msamaha kwa mumewe ili waendelee na maisha kama ilivyokuwa awali.“Davina amekubali yaishe, unajua anampenda sana mumewe, ‘so’ anahaha kwa ndugu ili wamuombee msamaha,” alisema ‘kikulacho’ huyo wa Davina.
Halima Yahya ‘Davina’ akiwa katika pozi.
Baada ya kuudaka ‘ubuyu’ huo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na
Davina ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Hayo ni maisha yangu binafsi,
hayamhusu mtu, kwanza nipo kwenye kikao, niache.”
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Post a Comment