ad

ad

KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 09


ILIPOISHIA

”Hivi, yule Fuko aliniambia kuhusu kununua dawa ya meno, wakati napiga mswaki asubuhi ile dawa ilikuwa mpya au ya zamani? Mbona kama sikumbuki kitu chochote pale,” alisema moyoni baba Joy.
Alisita kwanza kufanya jambo lolote lile na kuwaza kuhusu hilo la dawa ya meno...
”Noo! Pale hapakuwa na dawa mpya, ingawa sina uhakika na hili, oke, nitalifanyia kazi.
***
Mama Joy alisimama nje akiangaza kulia, kushoto na sehemu nyingine mbalimbali za eneo alilosimama...
”Sijui kama ataweza kuja tena kwangu, maana jana aliponea kwenye tundu la sindano. Na angekutwa na baba Joy hakiyamungu angemtoa sikio na risasi, mi baba Joy namfahamu vizuri sana yule mwanaume, ana hasira kama mkizi,” alisema moyoni mama Joy.
Alihisi mwili ukimnyevunyevua hasa akizingatia kuwa, jana yake akiwa katka hatua za mwisho za ’kutibiwa’ na mzoa taka ndipo mumewe alipoingia. Halafu mbaya zaidi, usiku baba Joy hakumgusa...
”Mh! Akija atagonga geti bwana,” alisema moyoni mama Joy na kuanza kuingia ndani. Lakini kabla hajazama, kwa mbali kulia kwake alimwona mwanaume anakuja, akasita, akarudi ili kumsubiria. Kwa bahati mbaya hakuwa mzoa taka, lakini alikuwa kijana wa palepale mtaani, ni nyumba ya tano tu kutoka nyumbani kwake...

”Hujambo Bonny..?”

”Sijambo, shikamoo mama Joy...”

”Asante, unakwenda wapi..?”

”Kule kwa mzee Mdenga na Madi...”

”Kufanya nini..?”

”Nimeutwa na baba...”

”Halafi siku hizi  Bonny mbona unajazia hivyo, unafanya mazoezi nini..?”

”Eee, nanyanyua vyuma siku hizi mama Joy...”

”Huko kwa Mdenga na Madi unarudi muda gani?”

”Sasa hivi...”

”Basi ukirudi pitia hapa tuongee kitu...”

”Sawa mama Joy.”

Bonny alitembea akiwaza kuhusu kauli ya mwanamke huyo, hasa ya kumwambia akirudi apitie kwake amwambie kitu...

 ”Huko kwa Mdenga na Madi unarudi muda gani?”

”Sasa hivi...”

”Basi ukirudi pitia hapa tuongee kitu.”

 Bonny aliyarejea mazungumzo yale huku akiwa hajui ni ya nini. Yeye alizaliwa mtaani hapo, lakini mpaka kufikia umri alionao hajawahi kuingia kwenye nyumba hiyo. Siku moja tu aliishia getini akiwa anaongea na Joy mwenyewe ambaye kwa wakati huo alikuwa shuleni sekondari ya boding...

”Tutaona nikirudi,” alisema moyoni hivyo na kuendelea na safari yake.



***

”Mama leo mbona safari za nje ni nyingi?” mlinzi alimuuliza mama Joy...

”We mume wangu..?”

”Kwani kukuuliza lazima niwe mumeo..?”

”Sasa kibali unapata wapi..?”

”Siku ile chumbani kwako si ulisema nikuite mke wangu na wewe ukaniita mume wangu, nilijua bado kibali kinafanya kazi...”

”Fuko umechoka kazi siyo..?”

”Hapana bosi...”

”Sasa ujasiri huo unaupata wapi?”

”Bosi nilikuuliza nikiwa na maana, nilijiua labda unatoka kumwangalia mzoa taka...”

”Wewe anakuhusu nini mzoa taka,” mama Joy alimkatisha...

”Nilitaka kukwambia alikuja asubuhi sana leo, nikamwambia mzee bado yumo ndani ajaribu baadaye.”

Mama Joy aliyekuwa akitembea kuelekea ndani, alisimama, akageuza na kuanza kutabasamu...

”Fuko...”

”Ndiyo bosi...”

”Ni kweli..?”

”Kweli bosi...”

”Kwa hiyo atarudi..?”

”Alisema saa tano...”

”Ngo ngo ngooo,” geti liligongwa...

”Ni yeye nini? Hebu mfungulie.”

Mlinzi alikwenda kufungua geti, lakini huyo aliyefunguliwa hakuingia, aliulizia kwa nje kiasi kwamba, mama Joy hakumwona...

”Marhaba hujambo...eee yupo....nimwambie nani?” mlinzi alijibizana na huyo mtu aliyegonga geti. Akamgeukia mama Joy...

”Bosi kuna kijana anaitwa Bonny anakuulizia wewe...”

”Mwingize apite. Karibu sana Bonny...”

”Asante sana mama Joy.”

Mama Joy alinyoosha mkono na kuushika mkono wa Bonny na kuanza kutembea naye kuelekea ndani...

”Hivi mama alirudi ile safari yake ya China..?” aliuliza mama Joy...

”Alirudi lakini amekwenda tena.”

Kule nyuma, mlinzi aliwatumbulia macho na kutingisha kichwa...

”Bosi bwana, sasa huyu kijana naye sijui amemtoa wapi? Na sijui ana shida naye gani?”

Mama Joy na Bonny walifikia sebuleni, Bonny alipokaa, mama Joy alikwenda jikoni kwanza, aliporudi naye akakaa kwenye sofa lilelile alilokaa Bonny...

”Niambie kijana wangu, chuo ulimaliza vile..?”

”Bado mwaka mmoja...”

”Sasa mbona uko hapa?”

”Nimefuata ada...”

”Mh! Ada shilingi ngapi kwani?”

”Iliyobaki ni laki mbili, sasa wakati nakwenda baba si alikuwa Marekani na mama China, baba amerudi jana, nadhani kesho nitaondoka...”

”Oke, sasa na mimi hapo kwenye laki mbili nitakuchangia shilingi laki moja, umesikia..?”

Bonny alifurahi sana si kwa sababu attachangiwa ada kwani baba yake ana uwezo sana, ila alijua kwenye bajeti yake ya shule atakuwa na laki moja ya ziada kwa hiyo akiwa chuo ataweza kwenda klabu na masela wenzake...

”Sawa mama Joy...”

”Nikupe sasa hivi au..?”

”Hata sasa hivi maana nadhani kesho asubuhi ndiyo naondoka, hatutaonana tena.”

Mama Joy alimwangalia kwa macho ya mlegezo huku akijilambalamba ulimi kama mtu anayeonja chumvi kwenye mapishi...

”Njoo uchukue,” alisema mama Joy akisimama, Bonny naye akasimama na kumfuata mwanamke huyo hadi kwenye mlango wa chumbani, akasimama...

”Ingia tu Bonny...”

”Hapana mama Joy, si vizuri niingie chumbani kwa baba...”

”Hamna neno Bonny, ingia tu.”

”Mama panatosha hapa...”

”Noo bwana, ingia, nitakupa laki mbili zote,” mama Joy alichombezea, Bonny akalainika, akazama chumbani. Mama Joy akafunga mlango nyuma ya Bonny huku akivua nguo chapchap...

”Bonny umejazia vizuri sana hakuna haja ya kupoteza muda, tufanye kweli, wala usione aibu haya mambo ya kawaida sana hapa duniani,” alisema mwanamke huyo akiwa ameshavua nguo zote.

Bonny aliweka kiganja cha mkono kwenye uso wake ili kuficha macho yake yasimwone mwanamke huyo ambaye kiuhalisia ni sawasawa na mama yake mzazi, mama Bonny...

”Bonny njoo sasa, tafadhali njoo kitandani, we mwanaume bwana, tena kijana rijali kabisa, ona ulivyo na kifua cha mazoezi, teh..! Teh..! Teh..! Teh..!  Bonny bwana...”

Bonny alijikuta akivutiwa na shilingi laki mbili, badala ya kuyaangalia mapenzi kwa mama Joy alivuta picha ya matanuzi atakapokuwa chuoni, alimsogelea mama Joy...

”Jamani, ona kifua chako kijana, kimejengeka vizuri sana, unafanya mazoezi gani Bonny?”

”Ya kunyanyua vyuma mama Joy...”

“Tu basi..?”

“Tu basi.”

Mama Joy alimvutia kifuani kwake, akamkumbatia wakiwa wamesimama wakitazamana. Ilifika mahali, mama Joy akapenyeza mkono ndani ya kifua cha Bonny na kuanza kukipapasapapasa huku akisema…

“Garden love hizo, daa kijana wewe bwana, girlfriend wako anafaidi sana eee..?”

Bonny alitamani kumwambia ampe sasa hizo laki mbili badala ya kupoteza muda…

“Anafaidi kawaida tu, si sana…”

“Acha bwana, mmh! Ona kazi, angalia ulivyo mpana…”

“Mama Joy…”

“Niambie kijana mtanashati…”

“Hizo laki mbili vipi?”

“Utapata wala usiwe na wasiwasi, hutaki kupumzika kidogo kwanza..?”

“Kupumzikaje..?”

“Kitandani…”

“Haa! Mimi mama Joy nipumzike kwenye kitanda chako..?”

“Kwani kuna nini, si kitanda cha mama mwenye nyumba.”

Mara mlango uligongwa…”

“Nani..?”

“Mimi,” aliitikia mlinzi…

“Unasemaje?” mama Joy alimuuliza baada ya kufungua mlango. Hakuwa na shaka kwamba aliyegonga ni mumewe kwa sababu alijua hawezi kutoka ofisini baada ya kutokuwepo kwa siku mbili…


ITAENDELEA SIKU YA KESHO

No comments

Powered by Blogger.