CATHY, KUBADILI JINA KISA LINA MKOSI
Staa wa filamu bongo Sabrina Rupia ‘Cathy'.
MKONGWE wa filamu kitambo,
Sabrina Rupia ‘Cathy’ amesema kuwa jina analotumia katika sanaa lina
mkosi hivyo yuko kwenye mkakati wa kulibadilisha na kujipa jina lingine
labda linaweza kumkaa vizuri.
Akizungumza na mwandishi wetu, Cathy alisema anaona jina hilo lina
mkosi kwa sababu linazungumzwa vibaya na baadhi ya wasanii wenzake hata
kama kuna kitu ambacho hakijui ni lazima lihusishwe jina lake kitu
ambacho anakiona kama jina hilo lina nuksi.“Unajua naona jina hili lina mkosi kwa sababu kitu kifanyika labda mimi nimepita tu basi litatajwa jina langu kitu ambacho mimi sikipendi na kuona labda lina matatizo jamani, haliko sawa kuendelea kuwa nalo,” alisema Cathy huku akidai yuko katika mikakati ya kutafuta jina lingine zuri ambalo anaona linamfaa. zaidi.
Post a Comment