BABA KIUMBE WA AJABU - 12
SOMA SEHEMU YA 1- 10 ==>bit.ly/1rpZczK
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
#MTUNZI: ALLY MBETU
Wiki ilikatika tukiwa tumejificha na mpenzi wangu, hata simu niliamua kuizima ili kuondoa usumbufu wa ndugu zangu. Siku moja asubuhi tukiwa mgahawani tukipata kifungua kinywa niliamua kuwasha simu. Utafikiri kuna mtu alikuwa akisubiri kwa hamu nilipowasha tu simu iliingia. Kuangalia ilionesha namba ya kaka yangu, niliiangalia kwa muda bila kupokea mpaka ikakatika. Haikupita muda simu iliita tena alikuwa dada nayo niliiangalia bila kuipokea.
“Masalu mbona hupokei simu?”
“Achana nao.”
“Kina nani?”
“Si hawa wapuuzi.”
12
“Ndugu zako?”
“Ndiyo.”
“Hebu pokea uwasikilize kwa vile hujui wanataka nini?”
“Achana nao najua wanataka kunijua nilivyo.”
“Masalu si umeambiwa kuwa sasa hivi mtu hakusogelei, wasiwasi wako nini?”
“Sina wasiwasi ila sipendi kuwasikiliza kwa vile hakuna jipya la kuniambia.”
“Wasikilize.”
“Sitaki, wale sio watu siwezi kuwasikiliza watu wabaya kama wale.”
Mara simu ya mpenzi wangu iliita aliipokea na kuzungumza.
“Eeeh...Ndiyo...Shikamoo mama...Ndiyo...Hapana...Lini?..... Leo...Sawa nitamwambia....nitakujulisha....Hapana tupo Mwanza...Sawa mama nitamwambia....Haya mama.”
Baada ya kukata simu alinigeukia na kunitazama kwa muda.
“Vipi kuna usalama?”
“Kiasi.”
“Kuna tatizo nyumbani kwenu?”
“Hapana, kwenu.”
“Kwetu kuna tatizo gani?” nilishtuka.
“Ndoto yako imekuwa na ukweli.”
“Ina maana baba amefariki?”
“Ndiyo, inaonekana hata ndugu zako walikuwa wakikutafuta kukupa taarifa.”
“Mmh! Sasa itakuwaje?”
“Mmh! Kazi ipo nataka nikueleze kitu kimoja kabla ya kufanya lolote turudi kwanza kwa mganga.”
“Kweli hilo wazo zuri. “
“Vipi mbona unanyanyuka?”
“Mambo yameharibika, japo alinitenda vibaya lakini kifo cha baba yangu kimeniuma sana.”
“Utafanyaje imeshatokea!”
“Lakini mganga si alisema mpaka tukikutana kimwili! Sasa imekuwaje?”
“Ndiyo maana nikasema twende kwanza tukamuulize kabla hatujafanya lolote.”
“Naona tusipoteze wakati.”
“Subiri basi tumalize kunywa chai.”
“Chai haipandi tena,” nilisema huku nikinyanyuka kwenye kiti.
“Pole mpenzi wangu.”
“Bado sijapoa, kifo cha baba kimeniuma sana,” nilijikuta nikidondokwa na machozi.
“Pole mpenzi,“ mpenzi wangu alinisogelea na kunibembeleza, kitu kile kiliniongeza uchungu moyoni na kuangua kilio cha sauti kilichowashangaza waliokuwepo hotelini. Ilibidi mpenzi wangu anipeleke chumbani.
*****
Nilipofika hotelini niliendelea kulia kwa sauti ya chini huku mpenzi wangu akiendelea kunibembeleza. Pamoja na yote niliyotendewa na baba, lakini kifo chake kiliniuma sana. Niliweka pembeni ubaya wake na kuyakumbuka mapenzi yake kwangu kipindi chote cha kukua kwangu.
Nilijua kilichomponza baba yangu ni tamaa ya mali ambayo masharti yake yaliiathiri familia yetu. Nikiwa bado nimeinama nikiendelea kumlilia baba yangu, mpenzi wangu aliniuliza:
“Kwa hiyo utakwenda kwenye msiba?”
“Hata sijui nifanye nini?”
“Lakini jambo hili ni zito si la kukurupuka.”
“Ni kweli, najua kabisa kifo cha baba ndugu zangu wanajua mimi ndiye mhusika mkuu. Unafikiri nikienda itakuwaje kama siyo kutiana aibu msibani?”
“Lakini kwa nini tusirudi kwa mganga ili atueleze tufanye nini?”
“Lakini si mganga alisema mpaka tukutane kimwili, sasa nini kilichomuua baba yangu?”
“Masalu swali hilo mimi siwezi kukujibu.”
“Basi twende kwa huyo mganga.”
Tulikubaliana kwenda kwa mganga kumpa taarifa ya kifo cha baba, tulipofika tulikuta watu wengi, hivyo ilitupasa kusubiri zamu yetu japo niliamini itatuchukua muda mrefu kuonana na mganga. Hatukuwa na budi kusubiri, lakini mganga alipita na mgonjwa akienda naye nyuma ya nyumba, nilijua anakwenda kumfanyia matibabu.
Baada ya dakika kama ishirini alirudi peke yake na kuniona, alionesha ishara ya kuniita. Nilinyanyuka na kumfuata ndani ya kilinge cha kutibia, baada ya kukaa alisema:
“Vipi, mbona umerudi mapema?”
“Baba amefariki jana.”
“Sasa tatizo nini?”
Swali la mganga lilinishangaza, baba yangu amefariki yeye haoni tatizo.
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili ndipo baba angefariki, au hata kulala chumba kimoja?”
“Masalu sijakueleza hivyo kuwa muelewa, nilikueleza mpaka mkutane kimwili si kulala chumba kimoja.”
“Sasa kifo cha baba yangu kinatokana na nini?”
“Kwa amri ya Mungu.”
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili?”
“Eeh, lakini na Mungu ana nafasi yake, huamini kuna kifo?”
“Naamini.”
“Sasa?”
“Lakini ndugu zangu waliniomba niokoe hali ya baba, kama amekufa bila mimi kufika si nitaonekana ndiye niliyechangia.”
“Huo ni wasiwasi wako, baba yako amejiua mwenyewe kwa msaada wa ndugu zako.”
“Una maana gani kusema hivyo?”
“Baada ya kushindwa kukudhuru walijaribu uchawi mmoja ambao ni mbaya kuliko kitu chochote. Ule ukifanyiwa huchukui muda lazima ufe, baada ya kuonekana hujali na unajiamini waliamua jambo moja, kukufutilia mbali. Kama si kinga niliyokufanyia sasa hivi ungebaki jina.”
“Ni uchawi gani?” Kauli ya mganga ilinitisha.
“Kweli ndugu zako wamekupania vibaya, uchawi uliofanywa ni wa kinyonga, anakamatwa kinyonga mzima anapasuliwa na kuchunwa ngozi. Kisha ngozi yake inawambwa na kupakwa dawa huku likinuizwa jina lako. Ngozi ikikauka na wewe uhai huna.”
“Du!” Nilishtuka.
“Ndiyo walivyofanya, kazi hiyo ilifanywa saa sita usiku ili asubuhi ukiamka ukutwe umekufa. Baada ya kutega uchawi wao walikwenda kulala huku mganga akiwahakikishia kuwa asubuhi wakiamka watasikia habari za kifo chako.
“Lakini ilikuwa tofauti na walivyo fikiria, kinga niliyokuwekea ilifanya kazi, nilikueleza kila watakachokufanyia kitawarudia. Uchawi uliotaka kukuua ndiyo uliomuua baba yako. Ndio maana nilikuambia kifo cha baba yako alijitakia mwenyewe akishirikiana na ndugu zako.”
“Unataka kuniambia bila kinga nisingeiona leo?”
“Hilo ni jibu uliza swali.”
“Kuhusu kwenda msibani itakuwaje?”
“Ukitaka nenda hawawezi kukufanya lolote.”
“Hatuwezi kutiana aibu kuwa mimi ndiye niliyemuua baba?”
“Wataanzia wapi, kwa kitendo walichokitenda jana usiku na leo kukuona hai wamezidi kuchanganyikiwa. Kama wangejua kama ni mimi ndiye niliyekukinga, basi wangenipa pesa nyingi ili wakupoteze.”
“Kuna umuhimu wa kuongeza kinga mwilini maana kama kinyonga kashindwa lazima wataendelea kutafuta kitu kingine,” nilijikuta nikijihami baada ya kuona vita iliyopo mbele na ndugu zangu ni nzito.
“Kijana kama kinyonga ameshindwa hakuna kitu chochote kitaweza japo kwa dawa yangu walikuwa wakijisumbua, uchawi ule ni mbaya sana.”
“Kwa hiyo unaniambiaje?”
“Ondoa wasiwasi, chochote kitakachokupata si mkono wa mtu bali amri ya Mungu.”
“Nashukuru mzee wangu.”
“Basi ondoa hofu hakuna chochote kitakachokukuta, kila atakayekugusa kitamrudia.”
Niliagana na mganga kisha nilimpitia mpenzi wangu na kurudi hotelini kujiandaa na kwenda msibani. Tukiwa njiani simu ya dada iliita, nilitaka kuacha kuipokea lakini niliipokea ili nijue ana shida gani.
“Haloo,” nilipokea.
“Asante Masalu, asante sana.. njoo umle nyama baba,” dada alisema kwa sauti iliyoonesha analia.
“Tena wewe ndiye ninayekutafuta mchawi mkubwa, nakuapia sitakusamehe wewe na wote hata marehemu baba mpaka nakufa. Vitendo vyote mlivyonitendea hamkuridhika mpaka mnaitaka roho yangu kwa nguvu? Hivi nikifa mtafaidika nini?”
“Nani anataka kukuua?”
“Kitendo mlichofanya wiki moja iliyopita sitawasamehe mpaka nakufa, mnanilaumu nahusika na kifo cha baba. Hebu niambieni mimi nimefanya nini kuchangia ugonjwa mpaka kifo cha baba. Kinyonga mliyemtumia ili mniue ndiye aliyemmaliza baba kwa taarifa yenu.”
“Ha! Umejuaje?” Dada alishtuka.
“Nakuapia nilikuwa nina mpango wa kuwasamehe, lakini kwa kitendo mlichokitenda jana saa sita usiku sitawasamehe milele na mimi nitajua cha kuwafanya, endeleeni kuroga nami sasa naingia vitani tuona nani zaidi.”
Kauli yangu ya vitisho japo sikuwa na nia hiyo ilimfanya dada akate simu.
“Masalu vipi mbona sikuelewi?” Mpenzi wangu aliniuliza.
“Wee waache tu.”
“Nani huyo?”
“Dada.”
“Mbona mnatishana?”
“Namtisha namwambia ukweli!”
“Kwa nini umewaambia mapema?”
“Lazima waujue ubaya wao na tena nawafuata msibani wanieleze kisa na mkasa cha kuyatafuta maisha yangu,” nilijikuta nikipandwa na hasira.
“Punguza hasira tukifika hotelini tutalizungumza, umeshawajua wabaya wako kwa nini uchanganyikiwe?”
Nilikubaliana na mpenzi wangu kurudi hotelini, tulipofika nilikuwa bado na hasira kwa kauli za dada kuwa nitamla nyama baba yangu aliyefariki kwa ajili yao wenyewe. Nilijikuta njia panda katika maamuzi yangu ya kwenda kwenye msiba wa baba. Nilijikuta nikipata ujasiri wa kwenda kwenye msiba wa baba.
“Aisee wacha niende kwenye msiba wa baba,” nilimwambia mpenzi wangu.
“Masalu nakuomba usiende.”
“Hapana lazima niende.”
“Panaweza kutokea ugomvi.”
“Na utokee, tena nakwenda kuwapa makavu.”
“ Nakuomba usiende mtatiana aibu.”
“Nisipokwenda watu hawatanielewa.”
“Bora wasikuelewe kuliko aibu itakayowakuta.”
“Hakuna aibu, mganga amesema hawatafunua midomo yao kusema lolote kwa kuiogopa aibu.”
“Mmh! Lakini ningekuwa mimi nisingeenda.”
“Lazima niende na leo watanitambua, siwezi kuishi na maadui zangu na kuwachekea.”
”Hayo ndiyo ninayokukataza, kama huwezi kuzuia hasira zako hakuna haja ya kwenda.”
“Nitajitahidi lakini moyo unaniuma baada ya kujua ubaya waliotaka kunifanyia usiku wa kuamkia leo.”
“Lakini si umepata kinga?”
“Ni kweli, lakini kama nisingepata ingekuwaje?”
“Ungepotea, lakini nakuomba ulimalize jambo hili kwa busara.”
“Nimekuelewa.”
Nilijiandaa na baadaye tuliondoka na mpenzi wangu ambaye nilimuacha nyumbani kwao na mimi kwenda kwetu. Nilipofika nilikuwa watu wengi wamekusanyika nje ya nyumba yetu wakiwepo wafanyabiashara wenzetu.
Sehemu kubwa ilikuwa imejaa magari ya watu, nilipoteremka kwenye teksi na kutembea kwenda ndani, kila aliyenitazama alinishangaa. Wengi walinipa pole ya kifo cha baba, niliwaitikia na kuingia ndani. Nilipofika ndani ndugu zangu walishtuka kuniona.
Sikujali hali ile, niliingia chumba alichokuwa mama, aliponiona aliacha kulia na kunitazama kama kiumbe cha ajabu. Kwa vile kila kitu nilikuwa nakijua sikuijali hali ile na kumsalimia.
“Shikamoo mama.”
“Marahaba.”
“Poleni.”
“Asante.”
“Mnazika saa ngapi?”
“Sijajua mipango yote wanafanya ndugu zako.”
“Kwani Masalu ulikuwa wapi?” Mama wa jirani aliniuliza.
“Nilikuwa safari.”
“Ooh! Pole sana kwa kumpoteza kipenzi baba yako, najua kiasi gani alivyokuwa akikupenda.”
“Ni mapenzi ya Mungu.”
“Na kweli, ni yeye aliyetoa na ndiye aliyetwaa.”
“Kila neno litatimia.”
“Masalu,” sauti kali ya dada iliniita.
“Unasemaje?”
“Njoo nje.”
“Kufanya nini?”
“Nimekwambia njoo au nitakutoa kwa nguvu.”
“Jeuri hiyo huna.”
“Salome hebu zungumzeni kwa ustaarabu hamjui hapa ni msibani?” Mama aliingilia kati.
“Kafuata nini? Namuuliza kafuata nini, aliyotaka yamekuwa anataka nini tena?”
“Tena wewe malaya wa kike funga domo lako,” Kwa mara ya kwanza nilimvunjia heshima dada yangu.
“Jamani mama Salome ni maneno gani hayo?” Jirani alitushangaa.
“Samahani jirani naomba utupishe mara moja,” mama alimtoa nje jirani baada ya kuona tunataka kumwaga mtama kwenye kuku wengi.
Baada ya jirani kutoka nje, tulibakia watatu ndani, mama alisema kwa sauti ya kilio:
“Salome unafanya nini?”
“Mama hujui aliyofanya mwanao, kamuua baba kisingizio eti tulitaka kumuua jana.”
“Una uhakika gani nimemuua baba?” Nilimuuliza.
“Kumbuka ulipokuja kumuona baba alisema tukuondoe kwa vile unataka kumuua.”
“Sikiliza wee malaya,” nilimnyooshea kidole dada.
“Ha! We niliyekushika kinyesi chako unanivunjia heshima?”
“Tena shetani wa kike, yaani nakuapieni yote mliyoyafanya juu yangu hamkuridhika, mkaamua jana kunifutilia mbali kwa uchawi wa kinyonga? Mama nisikilize vizuri tena kwa makini. Sitaisamehe familia yako mpaka naingia kaburini.”
“Usitutishe mchawi mkubwa.”
“Nafahamu kila kitu mnakijua hata mama niliyekuwa nakuamini kwa ajili ya mali unakubali wanao tuishe kwa ajili ya tamaa ya wachache. Nilikuwa na huruma na ndugu zangu na kukubali kuteseka kwa ajili yao, lakini hili la kutaka kuniua sitawasamehe milele.”
“Muongo mkubwa, wewe ndiye uliyemuua baba.”
“Mama nimemuua vipi baba?”
Mama hakujibu alitazama chini kwa aibu, niliendelea kusema kwa hasira lakini sauti ilikuwa ya chini.
“Dada Salome unajua kila kitu wewe ndiye uliyempa dawa mpenzi wangu anipake ili kuua nguvu zangu za kiume mlifanikiwa. Lakini mlisahau mimi si mzimu wa familia nilijua mlitaka kunitoa kafara kama dada Monika lakini mambo hayakwenda hivyo.
“Niliweza kupita chini juu na kuweza kuidhibiti hali hiyo, baada ya hapo hamkuridhika mkataka kunigeuza ndondocha mkashindwa na mwisho mkataka kuniua matokeo yake mmemuua baba. Mnakosa haya kunishtumu, hivi uchawi wenu wa kinyonga ungefanikiwa mimi ningekuwa wapi?
“Nasema hivi naondoka si hamnitaki, naondoka ila nawatahadharisha mkiendelea na mchezo wenu mtapukutika wote kama mlivyomtanguliza baba. Mimi si Monika ni Masalu,” nilisema nikiwa nimebadilika, sikuwa Masalu wa kuonewa tena.
“Masalu,” Dada Monika alitaka kusema kitu.
“Kwanza kabla sijaondoka nataka niione maiti ya baba yangu kwa mara ya mwisho.”
“Hapana Masalu baba huwezi kumuona,” dada Monika aliweka ngumu.
“Unajua nawastahi sana, najua kila kitu, kama mnataka siri yote nikaitoe kwa watu nje nikatazeni,” nilipiga mkwara mzito.
“Maiti ya baba yako imeharibika,” mama alisema kwa sauti ya upole.
“Hata kama iweje ni baba yangu nina haki ya kumuona.”
“Masalu acha tu baba yako azikwe, ameharibika sana,” mama aliendelea kunibembeleza.
“Mama mimi si mtoto wako?”
“Mtoto wangu.”
“Aliyekufa si baba yangu?”
“Baba yako.”
“Basi nipeleke nikamuone.”
Walitazamana kwa muda kisha mama alisema kwa sauti ya chini.
“Salome mpeleke mdogo wako akamuone baba yake.”
“Mama tulizungumza nini?”
“Salome sitaki ubishi hebu maliza hili kwa nini tuwafaidishe watu?”
Nilipelekwa chumba ulicholazwa mwili wa baba, nilikuta amefunikwa shuka, niliifungua upande wa kichwani. Kidogo nikimbie baada ya kukuta kiumbe cha ajabu kilichokuwa kama mnyama chenye manyoya na meno ya kutisha. Nililivuta shuka lote, sikuamini nilichokiona. Baba alikuwa amebadilika na kuwa kiumbe wa ajabu, mwili mzima akiwa na manyoya kama mnyama.
Nilimgeukia dada Salome.
“Baba yupo wapi?”
“Si huyo mbele yako.”
“Hapana huyu si baba yangu, naomba unioneshe baba yangu,” nilijikuta nikipandwa na hasira.
“Masalu huyu ndiye baba, tangu alipoanguka kila siku alikuwa akibadilika na kuwa kiumbe cha ajabu mpaka mauti yalipomkuta,” dada Salome alinipa maelezo ya sababu ya hali ya baba kuwa vile.
“Jamani mmeona mwisho wa ubaya aibu kama hii.”
Mara mlango ulifunguliwa na kuingia kaka zangu walioonekana wanatoka kunywa.
Jamani huyu mchawi amefuata nini?”
“Mama ndiye kampokea,” dada Salome alijibu.
“Toka nje, hebu kalete panga amfuate baba.”
“Kama jana mlishindwa kuniua kwa uchawi wa kinyonga na matokeo yake mkamuua baba, hamtaweza kuniua kamwe. Nitaondoka kwa kupenda si kwa kulazimishwa na familia ya wanga.”
Baada ya kusema vile niligeuka na kutoka nje, bila kuzungumza na mtu niliwapita watu ambao hawakuelewa kinachoendelea. Nilielekea barabarani na kukodi teksi iliyonipeleka nyumbani. Nilimpigia simu mpenzi wangu anifuate nyumbani. Alishangaa na kuniuliza:
“Vipi mbona unasema upo nyumbani kwako wapi, msibani?”
“Noo, kwangu kabisa.”
“Utani huo, si ulikwenda msibani au baba yako hakufa?”
“Amekufa.”
“Sasa mbona upo nyumbani?”
“Ni hadithi ndefu njoo mara moja nyumbani.”
“Nakuja.”
Nilikata simu na kujilaza kwenye kochi nikiwa bado hasira imenijaa moyoni. Baada ya muda mpenzi wangu alifika nyumbani na kunikuta katika dimbwi la mawazo. Hata alipoingia sikumuona alinishtua kwa kuniita.
“Masalu....Masalu.”
“Ee..eeh.”
“Jamani mbona hivyo?”
“Aah, umekuja saa ngapi?”
“Ndiyo naingia, mbona umerudi mapema mmeshazika?”
“Bado.”
“Sasa mbona umerudi?”
“Wee acha tu.”
“Kuna nini tena?” Aliniuliza kwa mshtuko kidogo.
“Wee acha tu.”
“Niache nini Masalu! Hebu nieleze kuna nini?”
Sikuwa na budi kumueleza niliyokutana nayo msibani, mpenzi wangu aliniangalia kwa huruma na kusema:
“Lakini Masalu we mbishi sana, si nilikueleza usiende ukabisha.”
“Ilikuwa lazima niende kwenye msiba wa baba yangu kwa vile unanihusu.”
“Japo unakuhusu lakini mazingira yake hayakuwa mazuri.”
“Yawe mazuri vipi ikiwa aliyekufa ni mzazi wangu?”
“Sawa mzazi wako lakini unajua kifo chake kilitokana na nini, Na dada yako baada ya kifo cha baba yenu maneno aliyokuambia, sasa nini kigeni kwako?”
“Nimekuelewa, lakini watanitambua.”
INAENDELEA...
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
#MTUNZI: ALLY MBETU
Wiki ilikatika tukiwa tumejificha na mpenzi wangu, hata simu niliamua kuizima ili kuondoa usumbufu wa ndugu zangu. Siku moja asubuhi tukiwa mgahawani tukipata kifungua kinywa niliamua kuwasha simu. Utafikiri kuna mtu alikuwa akisubiri kwa hamu nilipowasha tu simu iliingia. Kuangalia ilionesha namba ya kaka yangu, niliiangalia kwa muda bila kupokea mpaka ikakatika. Haikupita muda simu iliita tena alikuwa dada nayo niliiangalia bila kuipokea.
“Masalu mbona hupokei simu?”
“Achana nao.”
“Kina nani?”
“Si hawa wapuuzi.”
12
“Ndugu zako?”
“Ndiyo.”
“Hebu pokea uwasikilize kwa vile hujui wanataka nini?”
“Achana nao najua wanataka kunijua nilivyo.”
“Masalu si umeambiwa kuwa sasa hivi mtu hakusogelei, wasiwasi wako nini?”
“Sina wasiwasi ila sipendi kuwasikiliza kwa vile hakuna jipya la kuniambia.”
“Wasikilize.”
“Sitaki, wale sio watu siwezi kuwasikiliza watu wabaya kama wale.”
Mara simu ya mpenzi wangu iliita aliipokea na kuzungumza.
“Eeeh...Ndiyo...Shikamoo mama...Ndiyo...Hapana...Lini?..... Leo...Sawa nitamwambia....nitakujulisha....Hapana tupo Mwanza...Sawa mama nitamwambia....Haya mama.”
Baada ya kukata simu alinigeukia na kunitazama kwa muda.
“Vipi kuna usalama?”
“Kiasi.”
“Kuna tatizo nyumbani kwenu?”
“Hapana, kwenu.”
“Kwetu kuna tatizo gani?” nilishtuka.
“Ndoto yako imekuwa na ukweli.”
“Ina maana baba amefariki?”
“Ndiyo, inaonekana hata ndugu zako walikuwa wakikutafuta kukupa taarifa.”
“Mmh! Sasa itakuwaje?”
“Mmh! Kazi ipo nataka nikueleze kitu kimoja kabla ya kufanya lolote turudi kwanza kwa mganga.”
“Kweli hilo wazo zuri. “
“Vipi mbona unanyanyuka?”
“Mambo yameharibika, japo alinitenda vibaya lakini kifo cha baba yangu kimeniuma sana.”
“Utafanyaje imeshatokea!”
“Lakini mganga si alisema mpaka tukikutana kimwili! Sasa imekuwaje?”
“Ndiyo maana nikasema twende kwanza tukamuulize kabla hatujafanya lolote.”
“Naona tusipoteze wakati.”
“Subiri basi tumalize kunywa chai.”
“Chai haipandi tena,” nilisema huku nikinyanyuka kwenye kiti.
“Pole mpenzi wangu.”
“Bado sijapoa, kifo cha baba kimeniuma sana,” nilijikuta nikidondokwa na machozi.
“Pole mpenzi,“ mpenzi wangu alinisogelea na kunibembeleza, kitu kile kiliniongeza uchungu moyoni na kuangua kilio cha sauti kilichowashangaza waliokuwepo hotelini. Ilibidi mpenzi wangu anipeleke chumbani.
*****
Nilipofika hotelini niliendelea kulia kwa sauti ya chini huku mpenzi wangu akiendelea kunibembeleza. Pamoja na yote niliyotendewa na baba, lakini kifo chake kiliniuma sana. Niliweka pembeni ubaya wake na kuyakumbuka mapenzi yake kwangu kipindi chote cha kukua kwangu.
Nilijua kilichomponza baba yangu ni tamaa ya mali ambayo masharti yake yaliiathiri familia yetu. Nikiwa bado nimeinama nikiendelea kumlilia baba yangu, mpenzi wangu aliniuliza:
“Kwa hiyo utakwenda kwenye msiba?”
“Hata sijui nifanye nini?”
“Lakini jambo hili ni zito si la kukurupuka.”
“Ni kweli, najua kabisa kifo cha baba ndugu zangu wanajua mimi ndiye mhusika mkuu. Unafikiri nikienda itakuwaje kama siyo kutiana aibu msibani?”
“Lakini kwa nini tusirudi kwa mganga ili atueleze tufanye nini?”
“Lakini si mganga alisema mpaka tukutane kimwili, sasa nini kilichomuua baba yangu?”
“Masalu swali hilo mimi siwezi kukujibu.”
“Basi twende kwa huyo mganga.”
Tulikubaliana kwenda kwa mganga kumpa taarifa ya kifo cha baba, tulipofika tulikuta watu wengi, hivyo ilitupasa kusubiri zamu yetu japo niliamini itatuchukua muda mrefu kuonana na mganga. Hatukuwa na budi kusubiri, lakini mganga alipita na mgonjwa akienda naye nyuma ya nyumba, nilijua anakwenda kumfanyia matibabu.
Baada ya dakika kama ishirini alirudi peke yake na kuniona, alionesha ishara ya kuniita. Nilinyanyuka na kumfuata ndani ya kilinge cha kutibia, baada ya kukaa alisema:
“Vipi, mbona umerudi mapema?”
“Baba amefariki jana.”
“Sasa tatizo nini?”
Swali la mganga lilinishangaza, baba yangu amefariki yeye haoni tatizo.
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili ndipo baba angefariki, au hata kulala chumba kimoja?”
“Masalu sijakueleza hivyo kuwa muelewa, nilikueleza mpaka mkutane kimwili si kulala chumba kimoja.”
“Sasa kifo cha baba yangu kinatokana na nini?”
“Kwa amri ya Mungu.”
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili?”
“Eeh, lakini na Mungu ana nafasi yake, huamini kuna kifo?”
“Naamini.”
“Sasa?”
“Lakini ndugu zangu waliniomba niokoe hali ya baba, kama amekufa bila mimi kufika si nitaonekana ndiye niliyechangia.”
“Huo ni wasiwasi wako, baba yako amejiua mwenyewe kwa msaada wa ndugu zako.”
“Una maana gani kusema hivyo?”
“Baada ya kushindwa kukudhuru walijaribu uchawi mmoja ambao ni mbaya kuliko kitu chochote. Ule ukifanyiwa huchukui muda lazima ufe, baada ya kuonekana hujali na unajiamini waliamua jambo moja, kukufutilia mbali. Kama si kinga niliyokufanyia sasa hivi ungebaki jina.”
“Ni uchawi gani?” Kauli ya mganga ilinitisha.
“Kweli ndugu zako wamekupania vibaya, uchawi uliofanywa ni wa kinyonga, anakamatwa kinyonga mzima anapasuliwa na kuchunwa ngozi. Kisha ngozi yake inawambwa na kupakwa dawa huku likinuizwa jina lako. Ngozi ikikauka na wewe uhai huna.”
“Du!” Nilishtuka.
“Ndiyo walivyofanya, kazi hiyo ilifanywa saa sita usiku ili asubuhi ukiamka ukutwe umekufa. Baada ya kutega uchawi wao walikwenda kulala huku mganga akiwahakikishia kuwa asubuhi wakiamka watasikia habari za kifo chako.
“Lakini ilikuwa tofauti na walivyo fikiria, kinga niliyokuwekea ilifanya kazi, nilikueleza kila watakachokufanyia kitawarudia. Uchawi uliotaka kukuua ndiyo uliomuua baba yako. Ndio maana nilikuambia kifo cha baba yako alijitakia mwenyewe akishirikiana na ndugu zako.”
“Unataka kuniambia bila kinga nisingeiona leo?”
“Hilo ni jibu uliza swali.”
“Kuhusu kwenda msibani itakuwaje?”
“Ukitaka nenda hawawezi kukufanya lolote.”
“Hatuwezi kutiana aibu kuwa mimi ndiye niliyemuua baba?”
“Wataanzia wapi, kwa kitendo walichokitenda jana usiku na leo kukuona hai wamezidi kuchanganyikiwa. Kama wangejua kama ni mimi ndiye niliyekukinga, basi wangenipa pesa nyingi ili wakupoteze.”
“Kuna umuhimu wa kuongeza kinga mwilini maana kama kinyonga kashindwa lazima wataendelea kutafuta kitu kingine,” nilijikuta nikijihami baada ya kuona vita iliyopo mbele na ndugu zangu ni nzito.
“Kijana kama kinyonga ameshindwa hakuna kitu chochote kitaweza japo kwa dawa yangu walikuwa wakijisumbua, uchawi ule ni mbaya sana.”
“Kwa hiyo unaniambiaje?”
“Ondoa wasiwasi, chochote kitakachokupata si mkono wa mtu bali amri ya Mungu.”
“Nashukuru mzee wangu.”
“Basi ondoa hofu hakuna chochote kitakachokukuta, kila atakayekugusa kitamrudia.”
Niliagana na mganga kisha nilimpitia mpenzi wangu na kurudi hotelini kujiandaa na kwenda msibani. Tukiwa njiani simu ya dada iliita, nilitaka kuacha kuipokea lakini niliipokea ili nijue ana shida gani.
“Haloo,” nilipokea.
“Asante Masalu, asante sana.. njoo umle nyama baba,” dada alisema kwa sauti iliyoonesha analia.
“Tena wewe ndiye ninayekutafuta mchawi mkubwa, nakuapia sitakusamehe wewe na wote hata marehemu baba mpaka nakufa. Vitendo vyote mlivyonitendea hamkuridhika mpaka mnaitaka roho yangu kwa nguvu? Hivi nikifa mtafaidika nini?”
“Nani anataka kukuua?”
“Kitendo mlichofanya wiki moja iliyopita sitawasamehe mpaka nakufa, mnanilaumu nahusika na kifo cha baba. Hebu niambieni mimi nimefanya nini kuchangia ugonjwa mpaka kifo cha baba. Kinyonga mliyemtumia ili mniue ndiye aliyemmaliza baba kwa taarifa yenu.”
“Ha! Umejuaje?” Dada alishtuka.
“Nakuapia nilikuwa nina mpango wa kuwasamehe, lakini kwa kitendo mlichokitenda jana saa sita usiku sitawasamehe milele na mimi nitajua cha kuwafanya, endeleeni kuroga nami sasa naingia vitani tuona nani zaidi.”
Kauli yangu ya vitisho japo sikuwa na nia hiyo ilimfanya dada akate simu.
“Masalu vipi mbona sikuelewi?” Mpenzi wangu aliniuliza.
“Wee waache tu.”
“Nani huyo?”
“Dada.”
“Mbona mnatishana?”
“Namtisha namwambia ukweli!”
“Kwa nini umewaambia mapema?”
“Lazima waujue ubaya wao na tena nawafuata msibani wanieleze kisa na mkasa cha kuyatafuta maisha yangu,” nilijikuta nikipandwa na hasira.
“Punguza hasira tukifika hotelini tutalizungumza, umeshawajua wabaya wako kwa nini uchanganyikiwe?”
Nilikubaliana na mpenzi wangu kurudi hotelini, tulipofika nilikuwa bado na hasira kwa kauli za dada kuwa nitamla nyama baba yangu aliyefariki kwa ajili yao wenyewe. Nilijikuta njia panda katika maamuzi yangu ya kwenda kwenye msiba wa baba. Nilijikuta nikipata ujasiri wa kwenda kwenye msiba wa baba.
“Aisee wacha niende kwenye msiba wa baba,” nilimwambia mpenzi wangu.
“Masalu nakuomba usiende.”
“Hapana lazima niende.”
“Panaweza kutokea ugomvi.”
“Na utokee, tena nakwenda kuwapa makavu.”
“ Nakuomba usiende mtatiana aibu.”
“Nisipokwenda watu hawatanielewa.”
“Bora wasikuelewe kuliko aibu itakayowakuta.”
“Hakuna aibu, mganga amesema hawatafunua midomo yao kusema lolote kwa kuiogopa aibu.”
“Mmh! Lakini ningekuwa mimi nisingeenda.”
“Lazima niende na leo watanitambua, siwezi kuishi na maadui zangu na kuwachekea.”
”Hayo ndiyo ninayokukataza, kama huwezi kuzuia hasira zako hakuna haja ya kwenda.”
“Nitajitahidi lakini moyo unaniuma baada ya kujua ubaya waliotaka kunifanyia usiku wa kuamkia leo.”
“Lakini si umepata kinga?”
“Ni kweli, lakini kama nisingepata ingekuwaje?”
“Ungepotea, lakini nakuomba ulimalize jambo hili kwa busara.”
“Nimekuelewa.”
Nilijiandaa na baadaye tuliondoka na mpenzi wangu ambaye nilimuacha nyumbani kwao na mimi kwenda kwetu. Nilipofika nilikuwa watu wengi wamekusanyika nje ya nyumba yetu wakiwepo wafanyabiashara wenzetu.
Sehemu kubwa ilikuwa imejaa magari ya watu, nilipoteremka kwenye teksi na kutembea kwenda ndani, kila aliyenitazama alinishangaa. Wengi walinipa pole ya kifo cha baba, niliwaitikia na kuingia ndani. Nilipofika ndani ndugu zangu walishtuka kuniona.
Sikujali hali ile, niliingia chumba alichokuwa mama, aliponiona aliacha kulia na kunitazama kama kiumbe cha ajabu. Kwa vile kila kitu nilikuwa nakijua sikuijali hali ile na kumsalimia.
“Shikamoo mama.”
“Marahaba.”
“Poleni.”
“Asante.”
“Mnazika saa ngapi?”
“Sijajua mipango yote wanafanya ndugu zako.”
“Kwani Masalu ulikuwa wapi?” Mama wa jirani aliniuliza.
“Nilikuwa safari.”
“Ooh! Pole sana kwa kumpoteza kipenzi baba yako, najua kiasi gani alivyokuwa akikupenda.”
“Ni mapenzi ya Mungu.”
“Na kweli, ni yeye aliyetoa na ndiye aliyetwaa.”
“Kila neno litatimia.”
“Masalu,” sauti kali ya dada iliniita.
“Unasemaje?”
“Njoo nje.”
“Kufanya nini?”
“Nimekwambia njoo au nitakutoa kwa nguvu.”
“Jeuri hiyo huna.”
“Salome hebu zungumzeni kwa ustaarabu hamjui hapa ni msibani?” Mama aliingilia kati.
“Kafuata nini? Namuuliza kafuata nini, aliyotaka yamekuwa anataka nini tena?”
“Tena wewe malaya wa kike funga domo lako,” Kwa mara ya kwanza nilimvunjia heshima dada yangu.
“Jamani mama Salome ni maneno gani hayo?” Jirani alitushangaa.
“Samahani jirani naomba utupishe mara moja,” mama alimtoa nje jirani baada ya kuona tunataka kumwaga mtama kwenye kuku wengi.
Baada ya jirani kutoka nje, tulibakia watatu ndani, mama alisema kwa sauti ya kilio:
“Salome unafanya nini?”
“Mama hujui aliyofanya mwanao, kamuua baba kisingizio eti tulitaka kumuua jana.”
“Una uhakika gani nimemuua baba?” Nilimuuliza.
“Kumbuka ulipokuja kumuona baba alisema tukuondoe kwa vile unataka kumuua.”
“Sikiliza wee malaya,” nilimnyooshea kidole dada.
“Ha! We niliyekushika kinyesi chako unanivunjia heshima?”
“Tena shetani wa kike, yaani nakuapieni yote mliyoyafanya juu yangu hamkuridhika, mkaamua jana kunifutilia mbali kwa uchawi wa kinyonga? Mama nisikilize vizuri tena kwa makini. Sitaisamehe familia yako mpaka naingia kaburini.”
“Usitutishe mchawi mkubwa.”
“Nafahamu kila kitu mnakijua hata mama niliyekuwa nakuamini kwa ajili ya mali unakubali wanao tuishe kwa ajili ya tamaa ya wachache. Nilikuwa na huruma na ndugu zangu na kukubali kuteseka kwa ajili yao, lakini hili la kutaka kuniua sitawasamehe milele.”
“Muongo mkubwa, wewe ndiye uliyemuua baba.”
“Mama nimemuua vipi baba?”
Mama hakujibu alitazama chini kwa aibu, niliendelea kusema kwa hasira lakini sauti ilikuwa ya chini.
“Dada Salome unajua kila kitu wewe ndiye uliyempa dawa mpenzi wangu anipake ili kuua nguvu zangu za kiume mlifanikiwa. Lakini mlisahau mimi si mzimu wa familia nilijua mlitaka kunitoa kafara kama dada Monika lakini mambo hayakwenda hivyo.
“Niliweza kupita chini juu na kuweza kuidhibiti hali hiyo, baada ya hapo hamkuridhika mkataka kunigeuza ndondocha mkashindwa na mwisho mkataka kuniua matokeo yake mmemuua baba. Mnakosa haya kunishtumu, hivi uchawi wenu wa kinyonga ungefanikiwa mimi ningekuwa wapi?
“Nasema hivi naondoka si hamnitaki, naondoka ila nawatahadharisha mkiendelea na mchezo wenu mtapukutika wote kama mlivyomtanguliza baba. Mimi si Monika ni Masalu,” nilisema nikiwa nimebadilika, sikuwa Masalu wa kuonewa tena.
“Masalu,” Dada Monika alitaka kusema kitu.
“Kwanza kabla sijaondoka nataka niione maiti ya baba yangu kwa mara ya mwisho.”
“Hapana Masalu baba huwezi kumuona,” dada Monika aliweka ngumu.
“Unajua nawastahi sana, najua kila kitu, kama mnataka siri yote nikaitoe kwa watu nje nikatazeni,” nilipiga mkwara mzito.
“Maiti ya baba yako imeharibika,” mama alisema kwa sauti ya upole.
“Hata kama iweje ni baba yangu nina haki ya kumuona.”
“Masalu acha tu baba yako azikwe, ameharibika sana,” mama aliendelea kunibembeleza.
“Mama mimi si mtoto wako?”
“Mtoto wangu.”
“Aliyekufa si baba yangu?”
“Baba yako.”
“Basi nipeleke nikamuone.”
Walitazamana kwa muda kisha mama alisema kwa sauti ya chini.
“Salome mpeleke mdogo wako akamuone baba yake.”
“Mama tulizungumza nini?”
“Salome sitaki ubishi hebu maliza hili kwa nini tuwafaidishe watu?”
Nilipelekwa chumba ulicholazwa mwili wa baba, nilikuta amefunikwa shuka, niliifungua upande wa kichwani. Kidogo nikimbie baada ya kukuta kiumbe cha ajabu kilichokuwa kama mnyama chenye manyoya na meno ya kutisha. Nililivuta shuka lote, sikuamini nilichokiona. Baba alikuwa amebadilika na kuwa kiumbe wa ajabu, mwili mzima akiwa na manyoya kama mnyama.
Nilimgeukia dada Salome.
“Baba yupo wapi?”
“Si huyo mbele yako.”
“Hapana huyu si baba yangu, naomba unioneshe baba yangu,” nilijikuta nikipandwa na hasira.
“Masalu huyu ndiye baba, tangu alipoanguka kila siku alikuwa akibadilika na kuwa kiumbe cha ajabu mpaka mauti yalipomkuta,” dada Salome alinipa maelezo ya sababu ya hali ya baba kuwa vile.
“Jamani mmeona mwisho wa ubaya aibu kama hii.”
Mara mlango ulifunguliwa na kuingia kaka zangu walioonekana wanatoka kunywa.
Jamani huyu mchawi amefuata nini?”
“Mama ndiye kampokea,” dada Salome alijibu.
“Toka nje, hebu kalete panga amfuate baba.”
“Kama jana mlishindwa kuniua kwa uchawi wa kinyonga na matokeo yake mkamuua baba, hamtaweza kuniua kamwe. Nitaondoka kwa kupenda si kwa kulazimishwa na familia ya wanga.”
Baada ya kusema vile niligeuka na kutoka nje, bila kuzungumza na mtu niliwapita watu ambao hawakuelewa kinachoendelea. Nilielekea barabarani na kukodi teksi iliyonipeleka nyumbani. Nilimpigia simu mpenzi wangu anifuate nyumbani. Alishangaa na kuniuliza:
“Vipi mbona unasema upo nyumbani kwako wapi, msibani?”
“Noo, kwangu kabisa.”
“Utani huo, si ulikwenda msibani au baba yako hakufa?”
“Amekufa.”
“Sasa mbona upo nyumbani?”
“Ni hadithi ndefu njoo mara moja nyumbani.”
“Nakuja.”
Nilikata simu na kujilaza kwenye kochi nikiwa bado hasira imenijaa moyoni. Baada ya muda mpenzi wangu alifika nyumbani na kunikuta katika dimbwi la mawazo. Hata alipoingia sikumuona alinishtua kwa kuniita.
“Masalu....Masalu.”
“Ee..eeh.”
“Jamani mbona hivyo?”
“Aah, umekuja saa ngapi?”
“Ndiyo naingia, mbona umerudi mapema mmeshazika?”
“Bado.”
“Sasa mbona umerudi?”
“Wee acha tu.”
“Kuna nini tena?” Aliniuliza kwa mshtuko kidogo.
“Wee acha tu.”
“Niache nini Masalu! Hebu nieleze kuna nini?”
Sikuwa na budi kumueleza niliyokutana nayo msibani, mpenzi wangu aliniangalia kwa huruma na kusema:
“Lakini Masalu we mbishi sana, si nilikueleza usiende ukabisha.”
“Ilikuwa lazima niende kwenye msiba wa baba yangu kwa vile unanihusu.”
“Japo unakuhusu lakini mazingira yake hayakuwa mazuri.”
“Yawe mazuri vipi ikiwa aliyekufa ni mzazi wangu?”
“Sawa mzazi wako lakini unajua kifo chake kilitokana na nini, Na dada yako baada ya kifo cha baba yenu maneno aliyokuambia, sasa nini kigeni kwako?”
“Nimekuelewa, lakini watanitambua.”
INAENDELEA...

Post a Comment