WASANII SERENGETI FIESTA 2014 NDANI YA BREEZE FM
Wasanii
wanaotarajiwa kufanya shoo kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 leo
wakisubiria kufanyiwa mahojiano ndani ya kituo cha Redio cha Breeze FM
cha mjini Tanga mapema hii.
Msanii
kutoka Kundi la Yamoto Band, Dogo Aslay akizungumzia namna watakavyotoa
burudani kwa mara ya kwanza mjini Tanga katika Tamasha la Serengeti
Fiesta 2014 ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.
Nay wa Mitego akizungumzia namna atakavyoendeleza historia ya kuwakalisha wenzake leo usiku kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
Mo
Music akiwapanga wakazi wa Tanga ili waelekee katika Uwanja wa
Mkwakwani Tanga tayari kwa kumshuhudia akifanya makamuzi kwa mara ya
kwanza mjini hapo.
Chege
naye hakuwa nyuma kuwakaribisha wakazi wa Tanga ili waweze kuhudhuria
kwa wingi kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 tayari kwa kujionea
staili mpya ya wimbo wake wa Wauwe.
Mwanadada Rachel kutoka THT akieleza namna atakavyowakosha na nyimbo zake za mahaba wakazi wa Tanga.
Ommy
Dimpoz akiimba moja ya kipande cha wimbo wake mpya wa Ndakushima wakati
wa mahojiano mafupi juu ya Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 mapema leo
kwenye kituo cha Breeze FM mjini Tanga.
PICHA NA 2JIACHIE, TANGA








Post a Comment