OKWI ATUA DAR KIMYAKIMYA SAMBA SC YATAJWA, AFICHWA DAR
Na Saleh Ally
HUKU kukiwa na taarifa kuwa uongozi wa Yanga umeamua kuachana naye, kiungo mshambuliaji Emmanuel Arnold Okwi, ametua jijini Dar es Salaam kimyakimya.
HUKU kukiwa na taarifa kuwa uongozi wa Yanga umeamua kuachana naye, kiungo mshambuliaji Emmanuel Arnold Okwi, ametua jijini Dar es Salaam kimyakimya.
Okwi ametua kimyakimya kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), hali inayosababisha mkanganyiko wa mambo.
Wakati watu wengi wanaamini Yanga imeamua kuachana naye, kumekuwa na
taarifa kuwa watani wao, Simba wako katika harakati za kumrejesha katika
kikosi chao.
Okwi alitua nchini juzi saa 5:30 usiku kwa ndege ya Shirika la Ndege
la Kenya (KQ) na kupokewa, halafu akaingia kwenye gari huku akiwa hataki
kuzungumza lolote.
Mganda huyo alikuwa amevaa kofia ambayo alijaribu kuiziba asipigwe
picha. Baadaye aliingia kwenye gari la kifahari na kuondoka uwanjani
hapo. Imeelezwa amejichimbia kwenye moja ya hoteli za kitalii za jijini
Dar es Salaam.
Akipokewa na wenyeji wake.
Hofu inazidi kwamba huenda kuna mpango wa kujiunga na Simba, lakini
rafiki yake wa karibu ameliambia Championi Jumamosi kuwa, Okwi amekuja
kumalizana na Yanga kujua kama wanamhitaji au la kwa kuwa siku zote
amekuwa akitaka kuja lakini ikawa inashindikana.
“Okwi ameamua kuja huko kwa nauli yake mwenyewe. Unajua Yanga
hawajatoa hata senti, lakini kiustaarabu amewafuata ili wamueleze kama
wanamhitaji aendelee au la, basi ajue la kufanya.
“Okwi hataki ugomvi kabisa, nakuambia kuna timu moja ya Misri
inamhitaji, lakini amekuwa akikataa kufanya mazungumzo na akawaambia
wawasiliane na Yanga. Yeye anafuata taratibu, wao Yanga ndiyo hawataki
kumsikiliza,” alisema rafiki huyo na kusisitiza:
“Kama Yanga hawamtaki, wangemuambia ili achukue njia nyingine.
Mwenyewe ni mtu anayetaka kuendelea kufanya kazi na hao Yanga, ila
hawaelewi.”
Kuhusu hilo, jana mchana Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alikiri kuwa na taarifa na ujio wa Okwi.
“Kweli amekuja na hatujamlipia nauli, tunajua Fufa (Shirikisho la Soka Uganda) ndiyo wamemlipia. Hata kwa (Hamis Kiiza) ilikuwa hivyo. Unajua sisi (Yanga) tuliwakatia tiketi za kwenda na kurudi Uganda.
“Kweli amekuja na hatujamlipia nauli, tunajua Fufa (Shirikisho la Soka Uganda) ndiyo wamemlipia. Hata kwa (Hamis Kiiza) ilikuwa hivyo. Unajua sisi (Yanga) tuliwakatia tiketi za kwenda na kurudi Uganda.
“Likatokea tatizo, Shirika la Ndege la Uganda likafungiwa na tiketi
zetu zimefia huko. Sasa Fufa wameamua kutusaidia. Suala la Okwi
litashughulikiwa na kamati ya mashindano iliyo chini ya Seif Ahmed
‘Magari’, ambao walikuwa safarini lakini kesho (leo) wanaweza kukutana
na kulishughulikia na kupata mwafaka,” alisema Njovu.
Lakini baadaye mchana Championi Jumamosi lilimpata na kuthibitisha
haya: “Nisingependa kuzungumza mengi kwa sasa, lakini nimekuja
kuzungumza na Yanga. Sikuwahi kukataa kuja, ila kuna mambo lazima
yawekwe sawa. Tukimalizana, mtapata taarifa.”
Kama Okwi atashindwana na Yanga, maana yake atajiunga na timu hiyo ya
Misri inayomtaka na kwa mzunguko huo, maana yake zile fedha Sh milioni
480 ambazo Simba inaidai Etoile du Sahel ya Tunisia, itakuwa basi.
Kwani inaonekana atakuwa ameuzwa zaidi ya mara moja na fedha hizo
ambazo mwenyekiti wa wakati huo, Ismail Aden Rage alishindwa
kuzichangamkia, zitakuwa zimepotea
Post a Comment