ad

ad

UKAWA ZANZIBAR INATISHA WAITEKA ZANZIBAR KIWANJA CHA KUBANDA MAITI LEO


Hadi sasa watu wameshonana uwanjani kutoa sapoti yao kubwa kwa UKAWA katika kupigania Katiba inayotokana na maoni ya wananchi.

Ameshasimama Prof. Abdul Sheriff kutokea kundi la 201 ambaye amesema wazi kuwa wahuni wa kuhujumu hawatafanikiwa mbele ya UKAWA.

Katibu wa Shura ya Maimamu na Taasisi za Kiislamu amesema taasisi zote za Kiislamu zinaunga mkono Shirikisho la Serikali Tatu na kwamba walitoa maoni yao mbele ya tume na wanaungana na UKAWA kulidai hilo. Hakuna atakayeweza kuhimili vishindo vya UKAWA na wapenda haki na matumaini kwa ajili ya amani ya kweli nchini kwetu, Tanzania.

Ameishambulia Serikali na CCM kwa uchochezi wa kidini, kuwachonganisha Watanzania, kutokana na kauli ya uchochezi iliyotolewa na Waziri wa Serikali ya CCM, aitwae William Lukuvi tena kanisani akiwasema waislamu. Amehoji je mashehe nao wakifanya hivyo, nchi itatawalika?

Ametoa rai kwa viongozi wa UKAWA kuimarisha UKAWA na kuhakikisha kuwa UKAWA haufi.

mambo yanazidi kunoga

Jussa alipanda kuwakilisha wabunge wote wa UKAWA kutokea Zanzibar. Amewaambia Wazanzibar wawe tayari kuwasaliti na kuwazomea wale wote wanafiki wanaowasaliti wanapofika Dodoma kama Asha Bakari.

Amesema Wazanzibar wawashukuru watu kama akina Freeman Mbowe, James Mbatia, Tundu Lissu, John Mnyika na UKAWA nzima kwa kuwa wamesimama kidete kuitetea Zanzibar tofauti na Wazanzibar wengine kama akina Asha Bakari, Balozi Seif Idd na wawakilishi wote wa CCM kutoka Zanzibar.

Amemtangaza Balozi Seif Idd kuwa adui namba moja wa Zanzibar kwa ububu wake bungeni kama kiongozi mkuu kutoka Zanzibar ndani ya Bunge Maalum la Katiba.

Akaongeza kusema ujanja ujanja wanaotaka kufanya wa kubadilisha sheria ya mabadiliko ya katiba kuondoa sharti la 2/3 anasema wafanye wafanyavyo lakini hawataweza kwa kuwa mtarimbo umeganda.

Jussa akasema yeye alikuwa anaweza uwanja sawa tu lakini mchezaji hasa ni anayekuja punde ambaye ni Tundu Lisu.

Lisu;

Jussa alipanda kuwakilisha wabunge wote wa UKAWA kutokea Zanzibar. Amewaambia Wazanzibar wawe tayari kuwasaliti na kuwazomea wale wote wanafiki wanaowasaliti wanapofika Dodoma kama Asha Bakari.

Amesema Wazanzibar wawashukuru watu kama akina Freeman Mbowe, James Mbatia, Tundu Lissu, John Mnyika na UKAWA nzima kwa kuwa wamesimama kidete kuitetea Zanzibar tofauti na Wazanzibar wengine kama akina Asha Bakari, Balozi Seif Idd na wawakilishi wote wa CCM kutoka Zanzibar.

Amemtangaza Balozi Seif Idd kuwa adui namba moja wa Zanzibar kwa ububu wake bungeni kama kiongozi mkuu kutoka Zanzibar ndani ya Bunge Maalum la Katiba.

Akaongeza kusema ujanja ujanja wanaotaka kufanya wa kubadilisha sheria ya mabadiliko ya katiba kuondoa sharti la 2/3 anasema wafanye wafanyavyo lakini hawataweza kwa kuwa mtarimbo umeganda.

Jussa akasema yeye alikuwa anaweza uwanja sawa tu lakini mchezaji hasa ni anayekuja punde ambaye ni Tundu Lisu.

Lisu;

Wazanzibar wanamwita Lissu Christiano Ronaldo. Wananchi wameshangilia balaa alipoanza kwa kuwasalimia kwa jina la Zanzibar Huru na Tanganyika Huru na Shirikisho lenye hadhi kuu ya nchi.

Kwa miaka 50, anasema Tundu Lisu, Zanzibar imekuwa koloni la Tanganyika, Zanzibar imefungwa minyororo na Tanganyika na sio huru tena.

Kwa miaka 50 masuala yote ya nje yamekuwa yakiamriwa Dar es Salaam, Mambo ya Ulinzi yanaamriwa na Dar, masuala ya fedha ya Zanzibar yamekuwa yakifanywa na Dar na kwa hiyo ni koloni la Tanganyika.

Anasema mtia minyororo kwa mtu mwingine naye pia hawezi kuwa huru. Akatolea mfano wa mfunga minyororo wa magereza kuwa naye hawezi kuondoka., hivyo Tanganyika iliyoifunga Minyororo Zanzibar nayo haiko huru.

Akasema Tanganyika ilikana jina lake na kuliondoa kwenye katiba ili iendelee kuinyonya Zanzibar, anasema ilikuwa na Tanganyika huru ni kuwa na Zanzibar huru.

Anamkaribisha sasa Maalim Seif;

Maalim Seif jukwaani sasa; kaanza kwa kumtambulisha Mzee Moyo ambaye alikuwa Waziri wa Katiba wa Mzee Abeid Amani Karume, Mzee Moyo kasema 'ni tatu, tatu, tatu bila mzaha'. Kasema leo anaacha majembe yazungumze.

Maalim amesema kama wanaogopa Shirikisho la Serikali Tatu, basi yeye yuko tayari kuunga mkono serikali mbili kwa maana ya Zanzibar huru na Tanganyika huru, tofauti na hapo kila mtu na lwake.

Maalim anawatambulisha viongozi wa UKAWA nje ya bunge, akianza na Mosena Nyambabe- Katibu Mkuu wa NCCR Mageuzi.

Maalim Seif akaongeza kusema kuwa kama Kikwete anao uwezo wa kuwadhibiti Wazanzibar basi aende na cha moto kitaonekana.

Amesema kuwa kuna magari yameletwa kwenye mkutano na vikosi vya KMKM, akaasa kuwa ole wake aguswe mtu akasema anazungumza kama Makamu wa Rais, watajua jini liliko Zanzibar, uwanja ukalipuka kwa shangwe na nderemo.

Akapanda Emmanuel Makaidi mzee wa 'Moto moto motoooo...uwachome CCM'...

Dkt. Slaa amesema kuwa Jeshi la Tanzania halijakosa uzalendo kama walio nao mafisadi wa CCM na serikali yake. Kutokana na uzalendo ambalo JWTZ linao kwa wananchi na nchi, haliwezi kupindua serikali eti tu kwa sababu ni Shirikisho la Serikali Tatu.

Anasema kuwa wanajeshi wetu wamekuwa wazalendo kiasi cha kuvumilia kukosa mishahara, maslahi yao madogo na shida nyingine iweje wafanye hivyo kwa serikali tatu, amesema Kikwete halijui jeshi ndiyo maana amepotoka...

Maalimu Seif aliendelea ambapo aliwasihi viongozi wa UKAWA kujiimarisha na kuulinda UKAWA kwani wabaya wao wanajipanga.

Akasema kuwa wakati wa kutishana tishana umeshapita. Kuendelea kutisha Wazanzibar ni kuwaongezea ari na hamasa.

Makaidi amesema kuwa Watanganyika wamebakia bila serikali kwa sababu Mwalimu Nyerere Baba wa Taifa aliitupa serikali yote ya Tanganyika kwenye Muungano na Karume hakuitupa yote na ndiyo maana wamekuwa ngaringari leo.

Amewaomba Wazanzibar kuungana na Watanganyika kudai serikali zao...

Makaidi anasema CCM hakuna wanasiasa bali wajasiriamali na ndiyo maana hawataki kujisahihisha kama Mwalimu alivyotaka. Kisha akapanda Mtikila...


Mtikila; Kinachowasumbua CCM kuhusu serikali tatu ni unywani. Watanganyika wanapumbazwa kuwa uhuru ni mizinga uwanja wa taifa. Anasema kuwa kuwatisha wananchi na majeshi ni ugonjwa wa apedomia. Wanasahau kuwa wanajeshi wana ndugu zao wengi uraiani. Akamalizia kwa kusema saa ya ukombozi ni sasa...

Mbatia; muungano haukuridhiwa kwa sheria za Zanzibar kwa hiyo ni batili. Anasema Zanzibar kujitangazia mamlaka yake ni kuikomboa Tanganyika. Amesema kuwa wajumbe wa UKAWA kutoka Zanzibar wamewanyima turufu majiCCM huko BMK hivyo asitokee mtu wa kuisaliti Zanzibar.

Amesema kuwa chokochoko za udini zinapandikizwa na CCM, lakini hazitafua dafu. Anasema huwezi kuwa muislamu safi halafu ukahubiri udini na ubaguzi wa aina yoyote, huwezi kuwa Muislam safi kisha ukahubiri matusi na kejeli. Vivyo hivyo kwa mkristo safi.
Mbowe; maandamano nchi nzima ya kudai Katiba Mpya na bora inayotokana na maoni ya wananchi yanakuja baada ya mikutano ya Zanzibar. UKAWA haitarudi bungeni kushiriki dhambi ya kupingana na maoni ya wananchi, dhambi ya kuhubiri matusi kwa wananchi.

Amesema kuwa UKAWA huu si kwa ajili ya Katiba tu bali ni kwa ajili ya maslahi halisi ya wananchi. Ametangaza rasmi kuvunja Baraza Kivuli na sasa ataliunda upya kwa ushirika na NCCR, CUF CHADEMA.

Wananchi wamelipuka kwa furaha baada ya Kamanda Mbowe kutangaza kuwa UKAWA utaendelea hadi uchaguzi.;

Prof. Lipumba; wanaopinga serikali tatu kwa kigezo cha gharama hawajielewi. Anasema nchi inaingizwa kuzimu kwa matumizi ya hovyo na mabovu ya serikali kila siku.

Amesema ofisi ya rais inaongoza kwa matumizi ya hovyo. Anatoa mfano ambavyo imekuwa ikitumia mabilioni kwa Rais Kikwete kujitangaza Vasco Da Gama kwa kuzurura ughaibuni.

 

WAKAZI WA KUTOKA KISIWA CHA TUMBATU WALIFIKA KWENYE UKAWA NA MABANGO YAOKIWANJA CHA KIBANDA MAITI

MUASISI MZEE NASORO MOYOALIFIKA KWENYE UKAWA
MAKAMU WA KWANZA WA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIFF HAMADI AKIKUMBATIANA KATIBU MKUU WA CHADEMA DR WILBROD SLAA KULIA KATIBU MKUU WA NCCRMAGEUZI MUSONA

MAKAMU WA KWANZA ZANZIBAR SHARIFF HAMAD AKISALIMIANA NA KATIBU MKUU CHADEMA DR  SLAA

KATUIBU MKUU WA CUF MAALIM SEFU HAMADI AKIWASALIMIA WANANCHI
WANANCHI WAKISHANGILA

WANANCHI WAKIWA KATIKA MKUTANO WA UKAAWA

WENYEVITI WA UKAWA  JAMES MBATIA NCCR MAGEUZI KUSHOTO PROFES IBRAHIM LIPUMBA CUF KATIKATI NA KULIA NI MWENYEKITI FREEMAN MBOWE CHADEMA WAKIWASALIMIA WANANCHI

ASKARI  WA KIKOSZI CHA FFU AKIWA KATIKA ULINZI

WANANCHI WAKIWA NA MABANGO YENYE UJUMBE WA KUONYESHA SERIKALI TAU

EMMANUEL MAKAID AKIWA ANASALIMIANA NA MZEE NASORO MOYO MUASISI

WANANCHI WAKIWA MABANGO YAO

MWANANCHI HUYU AKIONYESHA PICHA ALIYOIWEKA MGONGONI KWA YA RAIS MSTAAF WA ZANZIBAR NAYE ANATAKA TATU

No comments

Powered by Blogger.