MAN MOYES YACHAPWA 2-0 UGIRIKI
MAMBO
yamezidi kumuendea kombo kocha David Moyes baada ya kuambulia kipigo
cha mabao 2-0 mjini Athens Ugiriki. Nyota wa Arsenal anayecheza kwa
mkopo Olympiacos, Joel Campbell alifunga bao la pili dakika ya 55 katika
ushindi huo dhidi Manchester United kwenye mchezo wa kwanza hatua ya 16
Bora Ligi ya Mabingwa.
Campbell
hakuwahi kugusa mpira The Gunners tangu aliposajiliwa mwaka 2011,
lakini usiku huu alionyesha kiwango cha juu akiwa na jezi ya Olympiacos.
Alejandro
Dominguez aliwafungia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 38 na sasa
United inatakiwa ishinde 3-0 katika mchezo wa marudiano mjini Manchester
ili kusonga mbele.
Katika mchezo mwingine, wenyeji Zenit wamefungwa mabao 4-2 na Borrussia Dortmund. Mabao ya Dortmund yemefungwa na Mkhitaryan, Reus na Lewandowski mawili, wakati ya Zenit yamefungwa na Shatov na Hulk.
Katika mchezo mwingine, wenyeji Zenit wamefungwa mabao 4-2 na Borrussia Dortmund. Mabao ya Dortmund yemefungwa na Mkhitaryan, Reus na Lewandowski mawili, wakati ya Zenit yamefungwa na Shatov na Hulk.
![]() |
| Wa mkopo; Campbell akishangilia baada ya kuiangamiza Man United usiku huu |
Sherehe: Dominguez (katikati) akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la kwanza
Mchezaji wa Olympiacos, Leadro Salino (kushoto) akigombea mpira na Ashley Young wa United
Wayne Rooney akilalamika kwa refa Gianluca Rocchi baada ya bao la pili
Wachezaji wa United wakisikitika uwanjani

Post a Comment