Pluijm awapa mtihani wa kwanza Yanga
KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, raia wa
Uholanzi, ameupa mtihani wa kwanza uongozi wa klabu hiyo baada ya kusema
anahitaji benchi lake la ufundi liboreshwe.
Hans ameanza kukinoa kikosi cha Yanga hivi karibuni baada ya
kukifuata kikosi hicho nchini Uturuki akibeba mikoba ya Mholanzi
mwenzake Ernie Brandts aliyetupiwa virago. Hans amesaini mkataba wa
miezi sita.
Akizungumza Mwenyekiti wa
Kamati ya Usajili ya Yanga, Abadallah Bin Kleb, alisema kocha
amefurahishwa na kikosi alichokiona lakini amehitaji marekebisho kadhaa
katika benchi lake hilo la ufundi.
“Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata kutoka Uturuki, hali ya kikosi
inaendelea vizuri na kocha amefurahia viwango vya wachezaji tofauti na
alivyofikiria ambapo amefanya tathmini ya mchezaji mmojammoja.
“Ila amehitaji kuongezewa nguvu katika benchi la ufundi, vitu vingine anavyohitaji viboreshwe ni vidogovidogo ili kukiimarisha zaidi kikosi.
“Ila amehitaji kuongezewa nguvu katika benchi la ufundi, vitu vingine anavyohitaji viboreshwe ni vidogovidogo ili kukiimarisha zaidi kikosi.
“Timu inatarajia kurudi nchini tarehe 23 (Alhamisi ijayo) mara baada
ya kumaliza kambi yao nchini humo tayari kwa kuanza mzunguko wa pili wa
ligi,” alisema Bin Kleb.
Yanga itafungua pazia lake la mzunguko wa pili Januari 25, kwa kuvaana na Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga itafungua pazia lake la mzunguko wa pili Januari 25, kwa kuvaana na Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Post a Comment