ad

ad

MASHAUZI CLASSIC YATIMIZA MIAKA MITATU

Keki iliyoandaliwa kwa ajili ya sherehe hiyo ya kutimiza miaka mitatu.
 Ndugu pamoja na marafiki wa Isha wakikata keki kwa pamoja.
 Wanenguaji hao wakifanya yao jukwaani kama wanavyoonekana.
BENDI ya muziki wa taarabu Mashauzi Classic inayoongozwa na mwanadada Aisha Ramadhani Makongo 'Isha Mashauzi' usiku wa kuamkia leo (Ijumaa) imetimiza miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake.
Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi mtendaji wa bendi hiyo Isha Mashauzi alisema kuwa anamshukuru Mungu kwa kumfikisha miaka mitatu tangu kuanzisha bendi yake hiyo.
"Kiukweli napenda kuchukuwa fursa hii kumshukuru Mungu, mama yangu mzazi mdogo wangu Saida Ramadhani 'Sungura mjanja' kwa kuwa pamoja kulisukuma gurudumu hili la kuisimamia bendi ya Mashauzi kikamilifu hadi leo kufikia hatua ya kutimiza miaka mitatu" alisema Isha.
Powered by Blogger.