Kijana mmoja aendesha maisha yake kwenye handaki
Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Chacha Makenge anaishi na
kuendesha maisha yake katika handaki alilolichimba katikati ya pori
lililopo katika eneo la chuo kikuu jijini Dar es Salaam kwa miaka minne
sasa,huku akiitaka serikali kuwa na utaratibu wa kuratibu shuguli za
vijana ili kulinda amani na usalama wa taifa.
Mara baada ya kukaribishwa katika nyumba anayoishi bwana Chacha Makenge mwenye umri wa miaka 36 na kutakiwa kusaini katika kitabu cha wageni, mwenyeji wetu anaanza kwa kuwataka watanzania kutokuwa na moyo wa visasi kwa wale ambao wametutendea vibaya na kuharibu maisha yetu huku akimtaja rafiki yake kuwa chanzo cha yeye kuishi maisha hayo baada ya kumchomea nyumba yake miaka minne iliyopita.
Mara baada ya kukaribishwa katika nyumba anayoishi bwana Chacha Makenge mwenye umri wa miaka 36 na kutakiwa kusaini katika kitabu cha wageni, mwenyeji wetu anaanza kwa kuwataka watanzania kutokuwa na moyo wa visasi kwa wale ambao wametutendea vibaya na kuharibu maisha yetu huku akimtaja rafiki yake kuwa chanzo cha yeye kuishi maisha hayo baada ya kumchomea nyumba yake miaka minne iliyopita.
Pia anailalamikia serikali kwa kutokuwa na
utaratibu mzuri wa kuwahudumia wananchi wenye shida pale wanapokwenda
katika ofisi za umma kwa ajili ya kuelezea matatizo yao.
Pia bwana Chacha anailaumu serikali kwa kushindwa
kukusanya kodi jambo ambalo limesababisha uwepo wa maisha duni na
upatikanaji duni wa huduma za kijamii kwa madi kuwa hakuna fedha za
kutoa huduma hizo ipasavyo kwa wananchi.
VIDEO IPO HAPA

Post a Comment