Wachina wakutwa na kiganja cha mfanyakazi wao
WACHINA wawili wa Kiwanda cha Urafiki Plastic cha jijini Dar es
Salaam wanashikiliwa na polisi wa Kituo cha Magomeni kwa tuhuma za
kukutwa na kiganja cha mfanyakazi wao, Jumanne Rashid, kilichofukiwa
kwenye eneo la kiwanda hicho.
Mmiliki wa kiwanda hicho, Lee Sliim, akiwa ndani ya gari la Polisi kuelekea kituoni kwa mahojiano zaidi.
Akielezea tukio hilo kwa waandishi wa habari jana, ndugu wa Jumanne
aliyejitambulisha kwa jina la
Rehema Rashid, alisema Novemba 17 mwaka
huu majira ya saa 3:00 usiku walipata taarifa kuwa ndugu yake alipata
ajali ya kukatwa mkono na mashine kiwandani hapo.
Alisema baada kupata ajali hiyo, Wachina hao kwa kusaidiana na
wafanyakazi wengine walimpeleka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa
ajili ya matibabu, ambapo ndugu wote waliendelea na huduma ya kumuuguza.
Mkono wa mtu uliopatikana kandokando ya Kiwanda cha kutengeneza mifuko ya Viroba na Plastiki, Mababi jijini Dar.
Rehema alisema jana wakiwa katika pilikapilika za kwenda kumjulia hali ndugu yao, walipata taarifa kwa wasamaria wema kwamba kiganja cha mkono wa ndugu yao kimeonekana kikiwa kimefukiwa pembezoni mwa kiwanda hicho.
Rehema alisema jana wakiwa katika pilikapilika za kwenda kumjulia hali ndugu yao, walipata taarifa kwa wasamaria wema kwamba kiganja cha mkono wa ndugu yao kimeonekana kikiwa kimefukiwa pembezoni mwa kiwanda hicho.
“Leo asubuhi tukiwa katika maandalizi ya kwenda kumwona Jumanne,
tulipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ambao wanafanya shughuli za
kufua vyuma chakavu karibu na kiwanda hicho wakitutaka twende kutambua
kama kiganja kilichofukiwa ni chake,” alisema Rehema.

Post a Comment