ad

ad

FUMANIZI LA JB UTATA MTUPU



STAA wa filamu Bongo, Jacob Steven ‘JB’ hivi karibuni  amedaiwa kufumaniwa hotelini na mke wa mtu wakivunja amri ya sita.

 Jacob Steven ‘JB’
Tukio hilo lilitokea wikiendi iliyopita katika hoteli ya Royal Village iliyopo Dodoma ambapo JB alikutwa na mke wa mtu aliyetambulika kwa jina la Sara wakivunja amri ya sita.

ISHU ILIKUWA HIVI
Akizungumza kwa masikitiko mume wa Sara ambaye ni dj maarufu Dodoma, Dj Rama alisema alifuatilia nyendo za mkewe huyo kwa siku nzima na mawasiliano yake ambapo ambapo kwa muda mrefu alikuwa akiwasiliana na JB ambaye waliagana kukutana katika hoteli hiyo.

Ilipofika saa tatu usiku Dj Rama alifika ndani ya hoteli hiyo na kuingia na kwenda kugonga kwenye chumba alichokuwa amelala na mwanamke huyo ambapo aligonga kwa muda mrefu baadaye sana ndipo mlango ukafunguliwa.

JB ASHUSHIWA KIPIGO
Baada ya mlango kufunguliwa JB alipokea  kipigo cha haja kutoka kwa dj huyo ambapo wahudumu wa hoteli na polisi waliokuwa wanafanya doria katika shoo ya Jahazi iliyokuwa ikiendelea kwenye ukumbi wa hoteli hiyo  walienda kumuokoa huku mwanamke aliyekuwa naye akitoroshwa kimyakimya.

Baada ya kuokolewa JB na mume wa mtu huyo walipelekwa katika kituo cha polisi cha Area D ambapo maelezo yalichukuliwa na kutakiwa kesho yake warudi.
Dj Rama aliendelea kueleza kuwa kesho yake waliporudi polisi alishinikizwa kuwa akubali yaishe ambapo walilazimishwa kuelewana.

WALIKUTANAJE NA JB?
Kwa mujibu wa mume alisema alipojaribu kumuuliza mkewe huyo walikutana vipi na JB alimweleza kuwa walikutana club ambapo walibadilishana namba na kuendelea kuwasiliana.
Mwanamke huyo aliyeshikwa ugoni hakurudi nyumbani tangu siku hiyo mpaka leo ambapo mumewe alieleza kuwa amuhitaji tena kwani alikuwa mchumba wake bado hawajafunga ndoa.

“Mimi simuhitaji tena japokuwa ana mimba ya miezi mine na sina uhakika kama ni ya kwangu kwani tabia zake sizielewi kabisa bora niachane  naye naamini Mungu atanipatia mwanamke sahii kwangu,”alisema Dj Rama.

JB ALIFUATA NINI DODOMA?
Dj Rama alieleza kuwa JB alienda Dodoma kwa mwaliko wa wasanii wa filamu waliokuwa 
wanazindua filamu yao na kumfanya yeye kuwa mgeni rasmi ndipo akapata nafasi ya kufanya ufuska huo.

JB ANASEMAJE?
Mapaparazi wetu walimtafuta kwa hali na mali JB kwa njia ya simu lakini baada ya mwandishi kujitambulisha na kabla hajazungumza chochote JB alisema amuache kwanza kwani yupo bize na shooting.
Habari na  Mapaparazi wetu.
Powered by Blogger.