TIKETI TAMASHA LA P-SQUARE ZAANZA KUUZWA
P-Square.
Uuzwaji
wa tiketi za tamasha la kundi maarufu zaidi la muziki wa kizazi kipya
barani Afrika, P-Square, umeanza kufanyika jijini Dar es salaam ambapo
zitauzwa kwa awamu tatu kwa bei tatu tofauti.
Wadhamini wakuu wa tamasha hilo, kampuni
ya simu ya Vodacom Tanzania, wamekuwa wa kwanza kuuza tiketi hizo ambapo
kupitia M-pesa wanauza tiketi kwa shilingi 30,000, zoezi litakalodumu
hadi tarehe 17 mwezi huu.
Akiongea na gazeti hili, Alex Galinoma,
Afisa masoko wa kituo cha EATV, amesema baada ya tarehe 17 tiketi
zitapanda bei na kuuzwa shilingi 35,000 ambapo safari hii zitakuwa
zikiuzwa kwenye maduka mbali mbali jijini Dar es salaam ambayo
yatatangazwa.
"Bei hii itaendelea mpaka mchana wa siku
wa tamasha ambapo sasa, ukienda eneo la tamasha(Leaders Club) kununua
tiketi mlangoni zitakuwa zikiuzwa shilingi 50,000, alifafanua Galinoma.
Mara ya mwisho kundi hilo lilipokuja jijini Dar, walikuja kwenye
tamasha liloandaliwa na kituo cha EATV, tamasha hilo lilipewa jina la
kibao chao kilichokuwa kikitamba wakati huo "Do Me".
Katika tamasha
hilo lililofanyika Agost 31, mwaka 2008, katika viwanja vya Leaders
Club, kiingilio kilikuwa ni 20,000 ambapo walifanya onyesho la dakika 45
huku wakitumia mtindo wa Playback.
Kwa mujibu wa Galinoma, safari hii wanamuziki hao watakuja na bendi nzima na watatumia mtindo wa ala na watakuwa jukwaani kwa masaa mawili bila kupumzika.
Kwa mujibu wa Galinoma, safari hii wanamuziki hao watakuja na bendi nzima na watatumia mtindo wa ala na watakuwa jukwaani kwa masaa mawili bila kupumzika.
Galinoma alisema
tamasha hilo la P-Square litaanza rasmi kuanzia saa moja jioni mpaka
saa 7 usiku, ili kuwapa mashabiki muda wa kupumzika na kuendelea na
mambo mengine.
Milango ya Leaders club itakuwa wazi kuanzia saa 12 jioni na mashabiki wataweza kuingia. Washabiki wanashauriwa kufika mapema Leaders club kwa sababu kutakuwa na ukaguzi wa kutosha na ulinzi mkubwa kwenye tamasha hili.
Milango ya Leaders club itakuwa wazi kuanzia saa 12 jioni na mashabiki wataweza kuingia. Washabiki wanashauriwa kufika mapema Leaders club kwa sababu kutakuwa na ukaguzi wa kutosha na ulinzi mkubwa kwenye tamasha hili.

Post a Comment