Marehemu Dk. Sengondo Mvungi enzi za uhai wake.
Marehemu Dk. Sengondo Mvungi alipokuwa ICU Muhimbili.
Habari za kusikitisha zilizotufikia jioni hii zinasema kuwa Dk.
Sengondo Mvungi amefariki dunia katika Hospitali ya Milpark Afrika
Kusini alikokuwa akitibiwa. Dk. Mvungi alipelekwa wiki iliyopita Nov. 7
kwa ajili ya kupewa matibabu zaidi akitokea Hospitali ya Muhimbili
kitengo cha Moi ambako muda wote alikuwa hajitambui baada ya
kushambuliwa na majambazi na kuumizwa vibaya sehemu ya kichwani akiwa
nyumbani kwake Kibamba. Wakati Dk. Mvungi anafariki, jana Jeshi la
Polisi, kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi,
lilitangaza kuwakamata watuhumiwa 9 wakiwa na mapanga yaliyotumika
katika uvamizi huo.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI - AMEEN!.
CHANZO NI GPL
Post a Comment