ad

ad

Wanafunzi waliofukuzwa vyuo vikuu nchini wamuangukia Rais Jakaya Kikwete

Wanafunzi waliofukuzwa vyuo vikuu nchini wamemuomba Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati tatizo lao ili kuwawezesha kuhitimu masomo katika fani mbalimbali.

Wanafunzi hao chini ya muungano wao wanaouita Umoja wa Wanafunzi waliofukuzwa Vyuoni wanasema kurejea katika masomo na kuhitimu kutaongeza idadi ya wataalamu katiki sekta za uzalishaji nchini.

Wanasema awali walibisha hodi ofisi za Bunge kusaka muafaka wa tatizo lao bila mafanikio huku safari hii wakimuomba Rais kuingilia kati…

Umoja huo wa wanafunzi unahusisha wanafunzi kutoka Chuo Kikuu Dodoma, Chuo Kikuu Cha Muhimbili, Mwalimu Nyerere na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha IFM.

Wanafunzi hao zaidi ya 50 ni miongoni mwa walifukuzwa Chuo mwaka 2011 baada ya kugoma kwa lengo la kuishinikiza serikali kuwaongezea fedha za kujikimu.
Powered by Blogger.