ad

ad

AMANDA POSHY NA KING MAJUTO HAPATOSHI NDANI YA NYUMBA NNE.

MWIGIZAJI wa filamu wa kike Bongo Amanda Poshy amefungua mwaka wa 2013 kwa kuingia na komedi akishirikiana na mwigizaji mkongwe katika tasnia ya filamu na komedi King Majuto, Amanda ameshiriki katika Komedi ya Nyumbana nne.
“Nimekamua sana katika komedi na Mzee King Majuto haikuwa rahisi unajua Majuto anachekesha sana kwa sababu mimi ni msanii nilionyesha jinsi nilivyokomaa katika kuigiza nikahakikisha nakwenda sambamba na Mzee Majuto na kuifanya kazi hiyo kuwa ya ukweli,”anasema Amanda.
Filamu ya Nyumba nne King Majuto anajikuta akiwa katika wakati mgumu baada ya kuoa wanawake wanne na kila mwanamke ana tatizo lake King Majuto anajikuta akiwa na matatizo na kuwa mtu kati mwenye kutatua matatizo kila kukicha, hiyo ndio komedi ya Nyumba nne.

Msapoti kwa kulike page yake Amanda Poshy link hii hapa bofya hapa www.facebook.com/pages/Amanda-Poshy-Fanpage
Powered by Blogger.