Matumizi mabaya ya dawa za binadamu
Kwa muda sasa nimekuwa nikisikia matumizi ya dawa za binadamu kwa
wanyama na ndege. Katika pita pita zangu kwenye duka la dawa baridi leo
nimabaini ukweli.
Anaingia dada mmoja na kuuliza:
" kuna tetracyline."
Muuza dawa:"hakuna"
Dada:"Hivi zinapakina kweli?"
Dada:"Mi mwenyewe nazitafuta kwa ajili ya kuku wangu."
Nilikuwa pembeni nikugana na kumueleza kuwa hizo dawa zimetengenezwa kwa
ajili ya binadamu na anaweza kupata dawa za kuku kwenye maduka ya
wanyama.
Tetracycline ni antibiotic inayotumika kutibu bacteria wa aina tofauti.
Dawa hii imechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa ugonjwa wa
kipindupindu na pia hutumika kutibu chunusi na trachoma.
Tanzania ni mojawapo ya nchi ambayo matumizi mabaya ya madawa yameelezwa kuwepo.
Zimekuwepo habari za matumizi ya dawa za kupunguza makali ya ukimwi kwa
kuku pamoja na nguruwe.Pia imeripotiwa matumizi ya vidonge vya majira na
antibiotics nyingine kwenye kuku. Dawa hizi zimekuwa zikitumiwa na
wafugaji kutibu magonjwa ama kukuza haraka mifugo yao.
Hii ni hatari kwani ni mojawapo ya vitu vilivyochangia kuibuka kwa
usugu wa dawa. Sababu nyingine ni kuuzwa dawa bila cheti cha daktari,
kutokumaliza dozi ama kutofuata taratibu za kutumia dawa.
Nchini Afrika Kusini imeripotiwa matumizi ya dawa za kukata makali ya
ukimwi kuchanganya na dawa za kulevya. Na matumizi ya namna hii
yanatokwa katika nchi mbalimbali.
WHO imetoa taarifa ya kuwa nchi za Afrika mashariki zimekumbwa na tatizo
la Usugu wa antibiotics kwa kiasi kikubwa. Tatizo hili husababisha
kuongezeka kwa gharama za afya ikiwemo kuhatarisha uhai.
Nini kifanyike
Serikali lazima ichukue hatua za ziada Mosi, kuimarisha huduma za kilimo
mijini na vijijini. Dawa za mifugo zipatikane kwa urahisi na kwa bei
nafuu.
Pili, usajili wa mabanda ya mifugo kwa serikali za mitaa.
Tatu,ukaguzi wa mabanda ya kufugia ili kufanya utambuzi wa kemikali
zinazotumiwa na wafugaji. Hii iambatane na adhabu kali kwa wale
watakaobainika kutumia dawa za binadamu.
Nne, ukaguzi wa maduka ya dawa baridi uimarishwe ikiwemo maduka kutakiwa kuonesha vyeti vya dawa zilizouzwa.
Kama tukitilia msisitizo mambo hayo tutaokoa afya za watanzania wengi.

Post a Comment