ad

ad

JOSE MOURINHO AIZUNGUMZIA MANCHESTER UNITED: “Tunajua tunaweza kuwafunga. Tunajua wanaweza kutufunga


JOSE MOURINHO ameupamba mpambano wa Ligi ya Mabingwa kati ya Real Madrid na Manchester United kama “mechi ambayo dunia inataka kuiona.”
Kocha huyo wa Real alikuwapo Old Trafford Jumapili akiipeleleza United wakati ikicheza na Liverpool, kuelekea mechi yao itakayopigwa Februari 13 – ikiwa ya kwanza katika hatua ya mtoano ya timu 16.
“Hii ni mechi ambayo dunia inataka kuiona. Real Madrid dhidiya Manchester United.Sir Alex dhidi ya rafiki yake Mourinho.
“Ubaya pekee ni kwamba si mechi ya fainali,” alisema Mourinho aliye maarufu kwa jina la Special One.
Mourinho, anayepigana kuiwezesha Real kubeba taji la kumi katika michuano hiyo, aliongeza: “Tunajua tunaweza kuwafunga. Tunajua wanaweza kutufunga — lakini tutakuwa tayari.”
Mreno huyo hata hivyo anaamini kuwa Madrid inayoongozwa na staa wa zamani wa United, Cristiano Ronaldo, iko vizuri zaidi baada ya kufuzu hatua hiii kitokea ‘Kundi la Kifo’.
“Kulikuwa na makundi ambayo ulijua yupi atakwenda kuwa wa kwanza na wa pili baada ya mechi mbili au tatu.
“Lakini kundi letu lilijumuisha timu tatu kati ya tano bora katika mashindano — Borussia Dortmund, Manchester City na sisi. Sasa tumepata mpinzani mgumu katika mechi kubwa ya timu 16 za mwisho,” alifafanua.
Powered by Blogger.