ad

ad

Michirizi Ya Damu - 16


Mauaji ya Bwana Belleck yaliyokuwa yametokea nchini Ufaransa yalimshtua kila mtu, watu hawakuamini kile kilichokuwa kimetokea, ni ndani ya siku tatu mabilionea wawili walikuwa wameuawa na kwa jinsi alama za mauaji zilivyokuwa zikionyesha, kila mtu akagundua kwamba muuaji alikuwa mmoja.
Polisi walichanganyikiwa, wakawasiliana na polisi wa nchini Misri na kuwaomba kuwatumia picha ya mtuhumiwa, hilo halikuwa tatizo, picha ikatumwa na ilipowafikia, wao wenyewe walishangaa.
Alikuwa mtu yuleyule aliyekuwa akitafutwa sana na FBI kwa kosa la kulipua kituo cha treni cha Pennsylvania. Hawakujua sababu ya mwanaume huyo kufanya matukio yote hayo. Wengi walihisi kwamba alikuwa gaidi, lakini gaidi na mabilionea wale kulikuwa na kitu gani kilichokuwa kikiendelea?
Hakukuwa na aliyekuwa na majibu, kila mmoja alikuwa na hamu ya kumkamata Fareed na kuweka wazi kile kilichokuwa kikiendelea mpaka kufanya matukio yote hayo.
“Atafutwe kila kona, wekeni picha zake katika vituo vyote vya televisheni duniani, sambazeni kadiri mnavyoweza mpaka kuhakikisha huyu mtu anatiwa mikononi mwa poli,” aliagiza mkurugenzi wa FBI nchini Marekani, Bwana Sandal Peters.
Mawasiliano yakafanyika kwenda nchini Ufaransa, polisi wa huko hawakujua mahali alipokuwa mtu huyo hivyo kwenda hotelini kwa ajili ya kuangalia kamera za CCTV ambazo waliamini kwamba zilimnasa mwanaume huyo.
Hilo halikuwa tatizo, wakapata picha ya mwanaume huyo, wakafuatilia kumfahamu zaidi mtu huyo, picha zake zikasambazwa kwenda sehemu nyingine, walijua kwamba mwanaume huyo alivyokuwa ameingia nchini Ufaransa alipitia sehemu katika bandari au uwanja wa ndege hivyo kwenda huko.
Walitafuta kila kona, walichukua picha za wasafiri wote waliokuwa wameingia katika sehemu hizo lakini hawakufanikiwa kuipata picha yake. Walipohamia kwa watu walioingia humo kwa ndege binafsi wakafanikiwa kuipata picha ya mwanaume huyo, maelezo yalisema kwamba aliingia ndani ya nchi hiyo kwa kutumia ndege binafsi iliyokuwa ikimilikiwa na bilionea kutoka nchini Marekani, Peter Williams.
“Is this Williams’ jet?” (hii ni ndege ya Williams) aliuliza polisi mmoja.
“Yeah! Why did he do this?” (ndiyo hii! Kwa nini amefanya hiv?) aliuliza polisi mwingine.
“We don’t know! We have to arrest him,” (hatujui! Tumkamateni) alisema polisi huyo.
Kwa msaada wa interpool, Bwana Williams akakamatwa, akawa mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ya mauaji yaliyotokea nchini Ufaransa. Na kwa sababu alikuwa amemsafirisha mtu aliyehusika katika ugaidi, akapewa kesi hiyo nyingine kwa kuwadhamini magaidi kulipua kituo cha treni cha Pennslyvania.
“Simfahamu kijana huyo,” alisema Williams wakati akiwa katika chumba cha mahojiano.
“Na alifikaje ndani ya ndege yako? Nani alimtafutia vibali? Kwa nini aliingia nchini Ufaransa kwa ndege yako na kuondoka kwa ndege yako?” yalikuwa maswali kadhaa ambayo alishindwa kuyajibu. Kila mtu akajua kwamba alihusika katika mauaji ya Bilionea Belleck lakini pia alihusika katika tukio la kigaidi lililotokea hapo Pennslyvania.
****
Fareed alikuwa akilia, maumivu ya tumbo yaliongezeka, alijua kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake. Siku hiyo hakula kitu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea tumboni mwake. Mawazo yake yakamwambia kwamba yale matunda aliyokuwa akila ndiyo yaliyomsababishia hali ile.
Siku hiyo ilipita huku akiwa kwenye maumivu makali, aliumia kupita kawaida. Usiku hakulala, alikesha akilia kwa maumivu makali, aliendelea kukohoa na kutoa madonge ya damu.
Ilipofika majira ya saa tano asubuhi ndipo kwa mbali akaiona meli moja kubwa ikielekea kule alipokuwa. Hakuwa na nguvu za kutosha lakini akasimama na kuanza kupunga mikono yake juu huku akijitahidi kutoa sauti ili asaidiwe pale alipokuwa.
Hiyo ilionekana kuwa nafasi pekee ya yeye kuondoka kisiwani pale. Meli ile ikaendelea kusogea, kwa mbali akawaona watu kutoka kwenye meli ileile wakipunga mikono kuashiria kwamba walimuona.
Vijana wawili wakafungua mtumbwi uliokuwa katika meli yao na kisha kupanda, hapohapo wakaanza kuelekea kule alipokuwa Fareed kisiwani ambapo baada ya kumfikia, wakaanza kumuuliza maswali kadhaa kuhusu sababu iliyomfanya kuwa mahali pale.
“Tumbo linauma…” alilalamika Fareed huku akilishika tumbo lake, hata maswali aliyoulizwa akashindwa kuyajibu kabisa.
Wakamchukua na kumpakiza ndani ya mtumbwi na kuelekea naye kwenye meli ile. Alikuwa akiugulia kwa maumivu makali, wakati mwingine aliwaambia watu hao kwamba alikuwa akifa na kitu kilichomuuma zaidi ni kwamba alikuwa akifa hata kabla hajamuua padri Luke ambaye alimbaka badala ya kumuongoza sala ya toba alipokwenda kuungama kwenye kanisa lake.
Hiyo ilikuwa meli kubwa ya wavuvi waliokuwa wakivua samaki katika eneo la kimataifa, walitokea nchini Marekani na miaka mingi kazi yao ilikuwa hiyo, walishinda kwenye meli na ni mara chache sana walikuwa wakitoka na kwenda kuzurura sehemu mbalimbali.
Hawakujua kitu chochote kuhusu Fareed, wakati dunia ikimtafuta kwa mauaji aliyokuwa ameyafanya, wao hawakuwa na habari hata kidogo. Walimkaribisha katika meli yao, wakampa dawa ya tumbo na kuondoka naye.
Kidogo dawa hiyo ikampunguzia maumivu makali. Wakati meli ikiendelea kuvua kama kawaida, alichokuwa akikifikiria ni kutoroka mara baada ya meli kufika nchi kavu.
Fareed akapata nafuu, akawa muongeaji mkubwa, alitaka kuwazoea watu hao ili wasiwe na maswali mengi. Alipoulizwa kuhusu sababu iliyomfanya kuwa mahali pale, hakutaka kuwaambia ukweli, aliwadanganya kwa kuwaambia kwamba alikuwa akisafiri kwa meli na wezake, ghafla bahari ikachafuka, meli ikapasuka na maji kuingia, kilichoendelea ni meli hiyo kuzama.
Ilikuwa rahisi kumwamini kwa kila kitu alichokuwa akikiongea, alizungumza huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikisema mbele yao. Sura yake ilivyokuwa, ilifanana na maneno aliyokuwa akizungumza hivyo kumwamini kwa asilimia mia moja.
Zoezi hilo la uvuaji liliendelea kwa siku kadhaa na ndipo wakarudi nchi kavu tayari kwa kuuza samaki wao waliokuwa wamewavua katika kipindi walichokuwemo huko.
Japokuwa walimzoea Fareed na waliahidi kumsaidia lakini baada ya meli kufika nchi kavu walishangaa kuona mtu huyo akiwa amewapotea katika mazingira ya kutatanisha. Hawakujua alikuwa wapi, walijaribu kumtafuta kila kona, mwanaume huyo hakuwepo kitu kilichowapa maswali mengi yasiyo na majibu.
Fareed alikuwa njiani akielekea kulipokuwa na mgahawa wa McDonald, alikuwa akitaka kula, kwa kiasi cha pesa alichokuwa nacho mfukoni mwake aliamini kingemsaidia.
Wakati akiwa kwenye mgahawa huo, akiwa ameagiza chakula ndipo macho yake yakatua katika televisheni ambapo kulikuwa na habari iliyokuwa ikizungumzia kuhusu kukamatwa kwa Bilionea Williams.
Alishangaa, alipoangalia sababu ya kukamatwa huko akaona ni kwamba alikuwa akihusika kushirikiana na magaidi katika kulipua kituo cha treni huko Pennsylvannia na pia alihusika kumtuma mtu kwenda kuwaua mabilionea wawili kwa kumtumia mtu aliyeonekana kwenye picha.
Fareed alipoangalia picha ile, alikuwa yeye, alionekana vilivyo alivyokuwa ameingia kwenye piramidi kwenda kumuua Bilionea Keith, alipoingia hotelini kumuua bilionea Bellck mpaka pale alipokuwa akikimbia katika kituo hicho cha treni.
Sura yake ikaanza kuwa maarufu, hapo mgahawani hakutaka kukaa sana, akasimama, akalipia na kisha kuondoka. Alijua fika kwamba ilikuwa ni lazima kukamatwa, hakutaka kuona akikamatwa pasipo kumuuua Padri Luke aliyekuwa amembaka, alitaka kumaliza kila kitu ili pale atakapokuja kukamatwa na kushtakiwa kifo basi afe akiwa na amani moyoni mwake.
“Ni lazima niende kanisani!” alisema Fareed.
Hakutaka kubaki mahali hapo, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenda katika kanisa hilo lililokuwa umbali wa kilometa mbili kutoka hapo alipokuwa. Akakodi teksi ambayo ikaanza kumpeleka huko.
Macho yake yalikuwa chini, aliogopa kuonekana na kugundulika, na hata alipokuwa ameongea na dereva wa teksi hiyo alikiinamisha kichwa chake chini.
Safari iliendelea mpaka alipofika kwenye kanisa hilo, akaingia. Kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma ndivyo ilivyokuwa kipindi hicho, kulikuwa na watu wachache sana kanisani humo, akaelekea mpaka katika sehemu ya kuungamia dhambi na kukaa tayari kwa kuzungumza na padri huyo ambaye ndani ya dakika chache, akaingia humo.
“Nimekuja kuungama dhambi zangu,” alisema Fareed huku akiangalia chini.
Padri Luke hakumgundua kwani alikuwa amebadilika, hakuwa kama vile alivyokuwa kipindi cha nyuma. Alizungumza naye kwa kirefu na kumwambia kwamba angerudi baadaye kwa ajili ya kuzungumza naye.
Akaondoka kanisani hapo, kitu cha kwanza alichokitafuta kilikuwa kisu, akafanikiwa kukinunua katika supamaketi ambayo haikuwa mbali kutoka hapo alipokuwa. Mwanaume aliyemuuzia ndani ya duka hilo alimwangalia kwa makini mno, sura yake haikuwa ngeni, ni kama aliwahi kumuona sehemu fulani.
Fareed akaogopa, akahisi kwamba mwanaume huyo aliliona tangazo la kutafutwa kwake hivyo alichokifanya ni kuondoka harakaharaka huku akiwa na kisu alichokinunua.
Alipofika kanisani, hakuingia katika mlango wa mbele, akapitia katika mlango wa nyuma, ule aliotolewa na padri yule, akafungua nati za kitas, akakitoa na kuingia ndani.
Kulikuwa na giza, akapiga hatua mpaka alipoufikia mlango mwingine ambao ulikuwa ni wa nyuma kuingia katika ofisi ya padri huyo. Akaingia na kutulia katika kochi moja. Padri hakuwepo, alikuwa katika chumba cha kuungamia dhambi akimsikiliza mtu mwingine.
Alikaa hapo kwa dakika ishirini, akamsikia padri huyo akija kule alipokuwa, haraka sana akaelekea nyuma ya mlango na kusimama, padri huyo akaingia. Hata kabla hajafanya kitu, akamkaba kwa nyuma, padri Luke akashindwa hata kupiga kelele, akajikuta akianza kulegea. Hapohapo Fareed akamuacha.
“Do you remember this face?” (unaikumbuka sura hii?) aliuliza Fareed huku akimwangalia padri Luke.
“Please! Don’t kill me,” (usiniue tafadhali) alisema padri huku akipiga magoti.
“Do you?” (unaikumbuka?)
“I saw you a while ago,” (nilikuona muda mfupi uliopita)
“Okey! I came to kill you,” (Sawa! Nimekuja kukuua) alisema Fareed huku akimwangalia padri huyo.
ITAENDELEA KESHO

No comments

Powered by Blogger.