BARCELONA WAWEKA MSISITIZO KWAMBA HAWATAWAPIGIA MADRID MAKOFI YA HESHIMA
FC
Barcelona wameweka msisitizo kwamba hawatawapigia makofi ya heshima ya
ubingwa wa Kombe la Dunia wapinzani wao Real Madrid timu hizo
zitakapokutana katika El Clasico Jumamosi hii.
Barcelona imesema haiwezi kufanya hivyo kwa Madrid kubeba ubingwa wa dunia.
Wameeleza,
wanatambua kama ingekuwa wamebeba ubingwa wa La Liga au Ligi ya
Mabingwa na mechi inayofuatia wakawa wanakutana, wangeweza kufanya
hivyo.
Kwa kuwa wamechukua ubingwa wa dunia, huo hauko katika utararibu wa kufanya hivyo na wao watashikilia hilo.
Post a Comment