‘Tajiri’ nyumba za Lugumi adai ameanza mchakato kurudisha fedha zake
Sakata la Dk. Louis Shika.
Dk. Shika amesema malipo hayo ya kiwango hicho kwa ajili ya bima, yatawezesha kurejesha fedha zake zilizo nje ya nchi kwa sababu alikuwa akishindwa kuzipata kwa sababu ya kukosa bima kama alivyoelekezwa.
Waandishi wa habari waliokuwa katika ziara ya Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye aliyeenda Shirika la Posta kuzungumza na wafanyakazi, walimkuta Dk Shika akiwa katika shirika hilo na walipozungumza naye alisema alifika hapo kwa ajili ya malipo.
Dk Shika, ambaye alishikiliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano akituhumiwa kuvuruga mnada wa nyumba hizo za mfanyabiashara wa jijini Dar es Salaam, Said Lugumi, alisema ametumia shirika hilo kulipa fedha hizo za bima kwa benki moja iliyoko Bangkok, Thailand.
“Kama mnavyoona hii karatasi,” alisema akionyesha fomu ya malipo.
“Nimelipa dola 100 za bima ili kukamilisha fedha zangu zije na nilipie zile nyumba. Hili la bima lilikuwa ni muhimu sana.”
Post a Comment