ad

ad

Mwili wa Ndesamburo wafanyiwa uchunguzi


Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Bazil Lema amesema mwili wa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Moshi mjini Phillemon Ndesamburo unafanyiwa uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo chake cha ghafla.
 
Lema amesema Ndesamburo alifika ofisini kwake asubuhi kama ilivyo kawaida yake lakini aliugua ghafla mnamo saa nne asubuhi.
 
Bazil alisema baada ya Ndesamburo kujisikia vibaya, alichukuliwa na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa ya KCMC na wakati madaktari wanakifanya jitahada za kumpa matibabu alifariki dunia.
 
“Baada ya mwili kufanyiwa uchunguzi taarifa rasmi kuhusu kifo chake zitatolewa na uongozi wa chama pamoja na familia,” amesema

No comments

Powered by Blogger.