Mwili wa Ndesamburo wafanyiwa uchunguzi
Katibu
wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Bazil Lema amesema mwili wa aliyekuwa
mbunge wa jimbo la Moshi mjini Phillemon Ndesamburo unafanyiwa uchunguzi
ili kubaini chanzo cha kifo chake cha ghafla.
Lema amesema Ndesamburo alifika ofisini kwake asubuhi kama ilivyo kawaida yake lakini aliugua ghafla mnamo saa nne asubuhi.
Bazil
alisema baada ya Ndesamburo kujisikia vibaya, alichukuliwa na
kukimbizwa katika hospitali ya rufaa ya KCMC na wakati madaktari
wanakifanya jitahada za kumpa matibabu alifariki dunia.
“Baada ya mwili kufanyiwa uchunguzi taarifa rasmi kuhusu kifo chake zitatolewa na uongozi wa chama pamoja na familia,” amesema
Post a Comment