YANGA CHINI YA LWANDAMINA YAANZA KWA KICHAPO KWA MABAO 2-0
Yanga imepoteza mechi yake ya kwanza chini ya Kocha George Lwandamina.
JKU ya Zanzibar ndiyo iliyoitia njaa Yanga kwa kuichapa mabao 2-0 katika
mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar.
Yanga ilikuwa nyuma kwa mabao 2-0 hadi mapumziko ndipo Lwandamina akabadili kikosi chote kwa asilimia 95.
Hata hivyo, bado hakuweza kuabdilisha lolote kwa kuwa hadi mwisho, JKU iliibuka na ushindi.
Post a Comment