ULIWAHI KULIJUA HILI, KWA NINI PLUIJM HUKAA JUKWAANI, HATA SIMBA ANAIFANYIA KAZI!
Wakati Simba ikiwa katika mbio za
kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara, upande wa pili, Mkurugenzi wa Ufundi
wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amekiri kuwa anazifuatilia timu za ligi
kuu ikiwemo Simba ili kujua mbinu zao na kuiwezesha Yanga ifanye kweli
pindi itakapokutana nazo.
Chanzo cha swali kwa bosi huyo ni
kutokana na uwepo wake uwanjani wakati Simba ilipoifunga JKT Ruvu bao
1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Jumamosi iliyopita, ambapo Pluijm alikuwa
bize akiandika mambo kadha awakati mchezo ukiendelea akiambatana na
Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh.
Akizungumzia uwepo wake uwanjani hapo
wakati wapinzani wao wakicheza, alisema: “Moja ya majukumu yangu kwa
sasa ni kuhakikisha nafuatilia timu nyingine.
“Ninatakiwa kuangalia mechi nyingi
kadiri iwezekanavyo na nitaendelea kufanya hivyo kwa kuangalia viwango
vya wachezaji kwa mmojammoja, sifanyi hivi kwa timu moja, ni kwa timu
zote. Wachezaji wengi wamekuwa wakishindwa kudumu kwenye viwango vyao na
jinsi wanavyocheza.”
SOURCE: CHAMPIONI
Post a Comment