ad

ad

ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’ ATWAA TUZO HII SWAHILI FASHION



Maonyesho ya mitindo ya mavazi ya Swahili Fashion Week 2016 yalianza jijini Dar es salaam, ambapo wabunifu kutoka sehemu mbali mbali Afrika wamepata fursa ya kuonyesha ubunifu wao.


Maonyesho hayo ambayo yalianza siku ya tar 2 Desemba nakuendelea mpaka tarehe 4 Desemba 2016, yamekuwa na mafanikio makubwa kutoa fursa kwa wabunifu kutoka nje ya mipaka ya nchi yao na kukutana pamoja kuonyesha vipaji vyao vya ubunifu.

Good news ni kwamba, Kwenye tukio hilo lililofanyika usiku wa tar 4 Desemba 2016, muigizaji Elizabeth Michael (Lulu) alijinyakulia tuzo ya mtu maarufu kwenye mitindo (Most stylish icon).

Sambamba na hayo tukio lililoibua hisia kubwa ni pale tuzo ya ‘Life achievement’, ambayo ilikwenda kwa mwandishi na mpiga picha maarufu hapa nchini, Muhidi Issa Michuzi.

No comments

Powered by Blogger.