Diamond na Zari Wamepata Mtoto wa Kiume Leo Des. 6, Bofya Hapa Kuona Picha
Pretoria, Afrika Kusini: TAARIFA
njema kwa mashabiki wa msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, Nasbu Abdul
“Diamond Platnumz” ambaye leo leo Desemba 6, 2016, mpenzi wake Zarina
Hassan “Zari The Boss Lady” amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali
ya Netcare iliyopo mjini Pretoria nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Diamond
kupitia ujumbe aliouandika kwenye akaunti yake ya Instagram ameeleza
kuwa mtoto wao huyo amezaliwa majira ya saa 8:35 usiku kwa saa za Afrika
kusini ambazo ni sawa na saa 10:35 alfajiri kwa saa za Afrika
Mashariki.
Zari amejifungua leo saa 10:35 alfajiri katika hospitali ya Netcare Pretoria South Africa lakini Diamond Platnumz amepost kutumia ukurasa wake wa instagram na kueleza furaha yake ila bado hawajampa jina mtoto wao huyo wa kiume.


Post a Comment