Diamond, Kiba pasu kwa pasu, mashabiki wao meno nje!
Ali Kiba baada ya kusaini mkataba na Kampuni ya Sonny.
HUKU mashabiki wa Ali Saleh Kiba
wakifurahia mafanikio ya msanii huyo kutokana na kulamba shavu la
kusaini mkataba na kampuni ya kimataifa ya Sony Music pamoja na kupewa
‘coverage’ na jarida maarufu la Marekani la The Source, mashabiki wa
Diamond Platnumz nao meno nje!
Diamond na Ne-Yo
Hiyo imefuatia baada ya Diamond naye
kutangazwa hivi karibuni kuwania Tuzo za Black Entertainment Television
(BET 2016) kwa mara ya pili mfululizo akiwa katika Kipendele cha Best
International Act: Africa, akichuana na wakali wengine wakiwemo Wizkid,
Yemi Alade (Nigeria), AKA, Cassper Nyovest na Black Koffie wote wa
Afrika Kusini.
Mafanikio ya mastaa hao yanawapa nguvu wasanii wengi wanaochipukia na waliopo kwenye gemu kuamini kuwa inawezekana.
Post a Comment